Tabata - Kinyerezi Mwisho jijini Dar ni sehemu hatari sana kwa usalama

mitindo huru

JF-Expert Member
Apr 26, 2016
1,607
1,596
Hizi salam ziwafikie mkuu wa mkoa wa Dar ndugu Paul Makonda, mkuu wa wilaya ya ilala ndugu Mushi, mkurugenzi mtendaji wa wilaya ya ilala ndugu Msongela Nitu Palela na pia meya wa wilaya ya ilala ndugu Charles Kuyeko, kwamba Tabata - Kinyerezi Mwisho ni sehemu hatari na inapaswa kuangaliwa kwa ukaribu kabla hayatokea maafa ya kutisha eneo lile kama ifuatavyo.
Tabata - Kinyerezi mwisho kuna stendi isiyo rasmi na pia kuna soko lisilo rasmi linahudumia idadi kubwa ya watu wa Kinyerezi na pia maeneo ya karibu kama Kifuru, Kibaga n.k.
Na pia ifahamike kuwa Kinyerezi ni moja ya eneo la wilaya ya ilala lililopimwa hivyo kuna eneo la stendi kwenye ramani ambalo hadi leo halijaendelezwa hadi leo bila taarifa na sababu yeyote na pia kwa sababu eneo la kinyerezi lilipimwa hivyo lina eneo rasmi ya soko ambalo limejengwa msingi na kuezekwa ila halina vyoo na hakuna huduma ya maji hali inayowafanya wafanyabiashara washindwe kuhamia katika soko hilo.
Lengo la kuandika taarifa hii ni kuwajulisha hatari kubwa inayoweza kutokea katika eneo la Kinyerezi Mwisho lisilo rasmi ambalo watu wanatumia kama stendi ya basi na pia soko kwa sasa, ilihali eneo hilo ni hatari kwa sababu ni eneo lililo chini ya nguzo za umeme zenye umeme mkubwa unaotoka katika mitambo ya kinyerezi ya kuzalisha umeme kwa njia ya gasi, kwani inakadiriwa umeme unaopita pale ni zaidi ya KWH 200,000 hadi KWH 2,000,000 hivyo endapo waya mmoja ukikatika utaleta maafa makubwa kwa watu wa eneo lile.
Wito wangu ni kuomba serikali ichukulie hili jambo kwa ukaribu sana kabla hayajatokea maafa makubwa pale Kinyerezi sababu kinyerezi imepimwa hivyo kuna eneo rasmi la stendi na soko , kwa hiyo hakuna sababu ya kuwaacha watu waendelee kutumia eneo la sasa kama stendi na soko ambalo ni hatari sababu ya umeme mkubwa unaopita pale juu.
Ni vizuri serikali ichukue mapema hatua ya kuwaamisha watu pale Kinyerezi mwisho ili waende eneo rasmi la stendi na soko ambayo ni salama zaidi kuliko kinachofanyika sasa.
Picha zinaonesha hali halisi ilivyo sasa pale Kinyerezi Mwisho sehemu isiyo rasmi kwa biashara na stendi
 

Attachments

  • 1474488847070.jpg
    1474488847070.jpg
    31.3 KB · Views: 148
  • 1474488854024.jpg
    1474488854024.jpg
    32.1 KB · Views: 111
  • 1474488860500.jpg
    1474488860500.jpg
    33.1 KB · Views: 112
  • 1474488868840.jpg
    1474488868840.jpg
    28.1 KB · Views: 108
  • 1474488884111.jpg
    1474488884111.jpg
    21.8 KB · Views: 104
  • 1474488893263.jpg
    1474488893263.jpg
    19.6 KB · Views: 90
  • 1474488901571.jpg
    1474488901571.jpg
    22.6 KB · Views: 89
  • 1474488915090.jpg
    1474488915090.jpg
    22.4 KB · Views: 85
  • 1474488922900.jpg
    1474488922900.jpg
    20.2 KB · Views: 94
  • 1474488931706.jpg
    1474488931706.jpg
    35.3 KB · Views: 90
  • 1474488943253.jpg
    1474488943253.jpg
    30.4 KB · Views: 88
  • 1474488975840.jpg
    1474488975840.jpg
    28.8 KB · Views: 86
  • 1474488986031.jpg
    1474488986031.jpg
    30.6 KB · Views: 84
  • 1474488997260.jpg
    1474488997260.jpg
    36.9 KB · Views: 90
  • 1474489008941.jpg
    1474489008941.jpg
    24.9 KB · Views: 88
  • 1474489037571.jpg
    1474489037571.jpg
    29.5 KB · Views: 92
Hii ni shida sana, mana kisheria inabidi mtu afanye shughuli zake mita 30 mbali kutoka nguzo zilipo, ila kwa pale Kinyerezi watu wanatumia zile nguzo kama mwamvuli.
Na siku zile nguzo zikipata hitilafu ikiwemo kukatika basi maafa yake yataacha historia kubwa hapa Tanzania.
Serikali inatakiwa iliangalie kwa ukaribu hili tatizo
 
Kukaa chin ya nguzo tushazoea ushawah fika pale kimara mwisho njia ya kwenda bonyokwa
 
Mungu akubariki Sana mleta mada, wewe ni mzalendo wa kweli na unanipenda Sana nchi yako.
Nasikitika kuwa sidhani Kama watakuelewa maana wapo bize kuua upinzani na kuhakikisha 2020 tunafika Tanzania ikiwa ni nchi ya chama kimoja.
Mambo mazito Kama haya hawana muda nayo, zaidi ya kupata Taarifa za intelligence kuwa mikutano ya upinzani itavunja amani.
Tanzania ni yatima.
hakuna anayeipenda hii nchi karibia wote ni wanafiki tu.
Unaipendaje nchi yako wakati pesa zako unaweka nje ya nchi?
Unaipendaje nchi yako wakati hutaki kukaa na wenzako vizuri?? as if Tanzania ni mke wako wakati ni taifa letu sote?
Hapo hadi Yatokee maafa ndo utasikia matamko hewa, ccm ni shida Sana.
 
Kukaa chin ya nguzo tushazoea ushawah fika pale kimara mwisho njia ya kwenda bonyokwa
Njia ya bonyokwa haina stand kubwa wala soko kubwa. ila Kinyerezi hali ya pale inatisha sababu kuna soko kubwa lisililo rasmi na pia kuna standi kubwa isiyo rasmi ya gari zinazoelekea Buguruni, Mnazi mmoja, Majumbasita, Segerea, Mbezi Mwisho, Kifuru, Ubungo n.k.
Hivyo maafa ya Kinyerezi itakuwa ni historia katika hii nchi endapo zile nguzo zikileta shida.
Na pia usipende kuhalarisha vitu vya hatari kama hivi eti kwa sababu sehemu fulani vipo, jifunze kujua namna gani unaweza kutatua.
 
Njia ya bonyokwa haina stand kubwa wala soko kubwa. ila Kinyerezi hali ya pale inatisha sababu kuna soko kubwa lisililo rasmi na pia kuna standi kubwa isiyo rasmi ya gari zinazoelekea Buguruni, Mnazi mmoja, Majumbasita, Segerea, Mbezi Mwisho, Kifuru, Ubungo n.k.
Hivyo maafa ya Kinyerezi itakuwa ni historia katika hii nchi endapo zile nguzo zikileta shida.
Na pia usipende kuhalarisha vitu vya hatari kama hivi eti kwa sababu sehemu fulani vipo, jifunze kujua namna gani unaweza kutatua.
Sijahalalisha swal la.kujiuliza nan alitangulia kufika hlo eneo kwa maana ya nguzo au soko kama ni soko means manspaa ilizembea ikaruhusu umeme mkubwa kupitia hapo....
And speaking of kimara mwisho aisee ile sehem ina movement ya watu sana na kuna stend ya watu wote wa bonyokwa plus soko lisilo rasm mkuu
 
Sijahalalisha swal la.kujiuliza nan alitangulia kufika hlo eneo kwa maana ya nguzo au soko kama ni soko means manspaa ilizembea ikaruhusu umeme mkubwa kupitia hapo....
And speaking of kimara mwisho aisee ile sehem ina movement ya watu sana na kuna stend ya watu wote wa bonyokwa plus soko lisilo rasm mkuu
Kwa ishu ya Kinyerezi serikali ndio imechelewa kutoa mwongozo kwa wananchi.
Asilimia kubwa ya eneo la kinyerezi imepimwa hivyo kuna eneo rasmi la soko na eneo la stand ambalo hadi sasa hayo maeneo yako wazi na hayatumiki, kwa hiyo ni jukumu la serikali kutoa tamko la watu kuhama pale kinyerezi mwisho na kuhamia maeneo rasmi ya shughuli za soko na stand yaliyopo katika ramani ya eneo la kinyerezi ili kuepukana na hatari kubwa ya zile nguzo zilizobeba umeme mkubwa kuliko kawaida kwenye eneo la sasa ambalo si rasmi.
 
Kwa ishu ya Kinyerezi serikali ndio imechelewa kutoa mwongozo kwa wananchi.
Asilimia kubwa ya eneo la kinyerezi imepimwa hivyo kuna eneo rasmi la soko na eneo la stand ambalo hadi sasa hayo maeneo yako wazi na hayatumiki, kwa hiyo ni jukumu la serikali kutoa tamko la watu kuhama pale kinyerezi mwisho na kuhamia maeneo rasmi ya shughuli za soko na stand yaliyopo katika ramani ya eneo la kinyerezi ili kuepukana na hatari kubwa ya zile nguzo zilizobeba umeme mkubwa kuliko kawaida kwenye eneo la sasa ambalo si rasmi.
Hivi kwa pale Kinyerezi soko na stand rasmi vimepangwa kujengwa mtaa au eneo gani?
 
Hivi kwa pale Kinyerezi soko na stand rasmi vimepangwa kujengwa mtaa au eneo gani?
Soko rasmi na stand rasmi vipo karibu barabara iliyokatisha kituo cha corner ukiwa unaelekea ofisi ya mtendaji wa Kinyerezi na hilo eneo ndio kipo Kituo cha polisi Kinyerezi, pia hilo eneo ndio inajengwa mahakama ya mwanzo Tabata Kinyerezi.
Soko limeshajengwa msingi wake na pia kuezekwa kabisa kama lilivyo soko la pale kituo cha mabasi SIMU 2000 - Mawasiliano ila bado manispaa wanasuasua kuhusu ishu ya vyoo na Tank la maji.
Stand ndio bado hata kuchongwa na ni sababu ya uzembe tu.
Unajua kwa ramani ya Kinyerezi ilivyo ilibidi Kinyerezi iwe ni eneo moja la kisasa sana jijini Dar, ila sababu ya usimamizi mbovu ndio uliosababisha serikali iendelee kuwaacha watu wasio na hatia kufanyia biashara sehemu ile ya Kinyerezi Mwisho chini ya zile Nguzo zinazopitisha umeme mzito namna ile.
Ndio mana nasisitiza serikali ichukue uamuzi wa haraka sana kuhusu kuhamisha watu lile eneo chini ya zile nguzo za umeme mana watu wengine bila kujua wanaendelea kujenga frem za biashara bila kujua hatari inayoweza kutokea lile eneo.
Nitakuletea picha za lile soko rasmi na hiyo sehemu ya stendi rasmi.
 
Hivi kwa pale Kinyerezi soko na stand rasmi vimepangwa kujengwa mtaa au eneo gani?
Kwa kinyerezi mwisho soko limepangwa kuwa eneo linaloitwa magengeni ambako tayari limeshaanza kujengwa ila bado alijaanza kufanya Kazi. Kuhusu stand ipo karibu na kanisa LA Roman ambayo kuanzia Jana imeshaanza kufanyiwa ukarabati ambapo muda si mrefu ihope itaanza. Na hii yote imetokana na jitihada za diwani wa sasa ambaye ni kutoka Chadema tofauti na diwani aliyekuwepo kipindi cha nyuma akufanya chochote cha maendeleo hali iliyopelekea kuchelewa mpaka sasa. Big up Chadema .
 
Hongera mleta mada, hizi ndizo habari za GT, Umeonyesha tatizo na suluhisho ukalionyesha pia. Naamin Manispaa inajipanga kumbuka hata Segerea ilikua hivo hivo lkn kwa sasa nadhan unajionea hali ilivyo mambo saafi.
 
Taifa linataka watu kama wewe ambao mnatoa yaliyo moyoni na facts juu..naimani wataliona bandiko lako mana hakuna kitu kibaya kama kukawa na soko bubu halafu hakuna vyoo mnaweza pata ugonjwa kipindupindu kina uafadhali
 
Mkuu, ondoa shaka! Zile waya kuanguka ni ndoto! Engineers wanajua scenarios zote kabla ya kupitisha nishati hatari kama ile. Otherwise ingekuwa kuna uwezekano huo, hizi waya zingewekewa kitu kama 'chandarua' kwa chini ili kuzikinga zikikatika zisifike aridhini!
 
Back
Top Bottom