M-bongotz
JF-Expert Member
- Jan 7, 2010
- 1,734
- 405
Waungwana hili jambo linanitatiza sana kwa kweli, kuna hizi taasisi zinazoongozwa na wake wa marais hapa Tanzania, mfano tulikuwa na EOTF enzi za mama Anna Mkapa sasa tuna WAMA inayoongozwa na Shostito Mama Salma Kikwete, kinachonisumbua ni kwamba hizi taasisi huwa zinaanziwa kuwatafutia ajira kina mama hawa au vipi maana najiuliza EOTF imekwenda wapi, inamaana bi mkubwa aliondoka nayo walipohama ikulu ndipo mwenzake akaja na WAMA sasa jamani kwa utaratibu huu si ina maana hizi taasisi ni mali zao binafsi, kwanini mama Mkapa hakumwachia bi Salma ile taasisi aiendeleze?..
Kinachonisikitisha sasa ni kwamba taasisi hizi zinapokea misaada mingi toka kwa wahisani sasa kusipokuwa na uangalizi mzuri wa karibu kina mama hawa si wanaweza kufuja misaada hata isiwafikie walengwa?, nionavyo mie ni kwamba hii ni njia ya kuwatafutia ma-wife kitu cha kuwakeep busy na hakuna lolote jingine, huu ni ulaji wao tu..nyie mwaonaje?
Kinachonisikitisha sasa ni kwamba taasisi hizi zinapokea misaada mingi toka kwa wahisani sasa kusipokuwa na uangalizi mzuri wa karibu kina mama hawa si wanaweza kufuja misaada hata isiwafikie walengwa?, nionavyo mie ni kwamba hii ni njia ya kuwatafutia ma-wife kitu cha kuwakeep busy na hakuna lolote jingine, huu ni ulaji wao tu..nyie mwaonaje?