Taasisi ya "Usheikh'' na fani ya uigizaji Tanzania

Du hii kwakweli ni zaid ya maigizo.

Kwahili nakubaliana na maulamaa Mohamed Said.

Huu ni utapel wa hali ya juu.
 
Ije mvua lije jua Rais tunayemtaka ni Edward Ngoyai Lowassa hatuko tayari kuona familia ya Rais unatupangia Rais ajaye hapa patachimbika fanyeni masihara

Raisi munayemtaka wewe na akina nani?

Na mimi naomba mgao nikubali halafu nije kusikitika baada ya uchaguzi.
 
Hawa mashehe ni wanaccm na wanajua ndani ya chama zamu hii ni ya Wakristo kutoa Rais na wanaelewa kwa mujibu wa urithi walioachiwa na mwalimu ni AMA Rais atoke Katoliki AU Bakwata. Sasa masheikh wa Bagamoyo wameleta UJUMBE na habari njema kuwa Rais aweza toka kwa Waprotestanti na hii ina maana PANA so tafakari badala ya kukejeli tu na kulaumu! Je wangemwendea Pinda au Membe au Slaa mngesemaje? Amka sasa!
 
Ingekuwa ni Prof. Lipumba au Dr. Slaa ndio ametembelewa na hawa viongozi wa dini kama hivi kuna mtu wa chama fulani tungemsikia akitembea huku na huko akiwaita wadini. Huyu naona yeye ana leseni ya kutumia udini kuusaka urais.
 
Ujumbe wa Masheikh si wa kupuuza.Ni wawakilishi wa waumini wao huko Bagamoyo.Hatujui undani wa mazungumzo yao na Lowassa.Lakini yawezekana hao Masheikh walitaka kujua msimamo au mtizamo wa Lowassa kwa maswala yanayowahusu waumini wao ikiwa EL ataamua kugombea uraisi.Hawataki kushutukizwa,wao wanataka kujua jinsi gani EL atasimamia matakwa yao ili wakubaliane nae au waachane nae kungali mapema.
 
Mimi nikajua wanafanya Bongo Movie kumbe wamechukua pesa za michango ya madraasa bagamoyo wakaji sevia kidogo toka kwa lowasa ..eti wanamchangia ?!1 :pound:..wote hao masheikh ubwabwa na ngoja wenzao kesho watavyowajibu wa Dar
 
Sidhani kama ni sahihi kusema wamenunuliwa, hao masheikh kama wanaccm wengne wanauhuru wa kumshawishi mtu wanayeona anafaa kugombea urais kupitia chama chao. Wewe kama humtaki pia ni sawa hakuna matusi wala ugomvi hapo mwisho wa siku kura ndio zitaamua.
 
ila jamaa aliye andika uzi huu ameniamsha na kujiuliza maswali mengi kichwani mwangu.kubwa zaidi ni kutaka kujua kama kweli hao masheikh wameenda kwa kofia ya usheikh au kama wafuasi binafsi wa lowassa?kama walienda kwa kofia ya usheikh jumuia wanazo ziongoza zimewabariki kufanya hiyo safari?je sheikh mkuu wa bagamoyo ni miongoni mwao?na kama simiongoni mwao ni kwa nini yeye hakuenda?kwa kweli maswali ni mengi.nakushukuru kuni bumbulua.
 
Mohamed Said
Angalia ile picha ya mwisho. Uwepo wa Prof. Juma Kapuya ndio umetoa taswira nzima ya nini kinaendelea. Alianzia kwao Tabora ambako walimtawaza Lowossa kuwa chifu wa Unyenyembe na hilo limeacha vidonda kule watu hawaelewani. Kapuya ni mmoja wa watu wa karibu sana na Lowassa kwenye harakati zake za kutaka urahisi (sijakosea hilo neno). Wanatafuta urahisi lakini urais hawataupata!
 
Mwalimu Julius,
Uko sawa ni Dodoma si Monduli mimi nimekosea niwie radhi.

Naomba sana FaizaFox asilione hilo kosa. Unakumbuka alivyomshambulia Prof Hirji kwa kukosea majmaji na kuandika Maumau? Yule dada balaa. Huwa haelewi kitu kinaitwa apology. Sijui ni dini gani yule dada.
 
Hawa mashehe ni wanaccm na wanajua ndani ya chama zamu hii ni ya Wakristo kutoa Rais na wanaelewa kwa mujibu wa urithi walioachiwa na mwalimu ni AMA Rais atoke Katoliki AU Bakwata. Sasa masheikh wa Bagamoyo wameleta UJUMBE na habari njema kuwa Rais aweza toka kwa Waprotestanti na hii ina maana PANA so tafakari badala ya kukejeli tu na kulaumu! Je wangemwendea Pinda au Membe au Slaa mngesemaje? Amka sasa!

Kama wangemwendea Membe, ingekuwa sawa na kumwendea sheikh mwenzao
 
Waislam huwa wana msimamo kwa mambo yao tu, lakini kwa mambo mengine wako laini sana, sasa hawa Mashekhe mpaka wamehongwa pesa kwenda Monduli, imekuwaje. Waislam acheni kuwa laini, mpaka sasa katiba pendekezwa imepatikana kihuni, viongozi wa Kikristo wametoa tamko kwamba ipigwe kura ya hapana, lakini Waislam wamekaa kimya tu.
 
Mimi nimeipenda picha ya tatu kutoka juu kuja chini. Kuna dada kasimama(na hisi ni mwandishi wa habari) yaani ameshika tama na peni yake mkononi' anawatizama hao masheikh waliokaa na muheshimiwa Lowassa na anawasikitikia sana tena sana!! Naomba na nyinyi wanajamvi muingalie hiyo picha tena na muipe maneno.

Hajui aandike nini, maana nae ni mmoja wao katika payroll....
 
Back
Top Bottom