Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,193
- 30,533
TAASISI YA "USHEIKH'' NA FANI YA UIGIZAJI TANZANIA
Written By Mohamed Said on Saturday, March 21, 2015 | 12:14 PM
Masheikh na Maimamu 83 kutoka wilaya nzima ya Bagamoyo wamfuata mhe.lowassa nyumbani kwake dodoma kumshawishi agombee..
LOWASA NI CHAGUO LA MUNGU
SIMAMA NA UHESABIWE
Hii picha nimeipata katika mtandao. Nilipokuwa naitazama kinywa kimenikauka mate. Najiuliza hivi hii taasisi ya usheikh mbona ghafla imekuwa taasisi ya vichekesho? Hawa masheikh wa Bagamoyo wanatoka Bagamoyo ipi? Hawa masheikh wanatoka misikiti au madrasa ipi? Huu usheikh siku hizi imekuwa ya mpata mpatae yaani mtu akivaa kanzu, koti na kofia tayari keshakuwa sheikh?
Sasa wazo jingine likawa linanijia....Tanzania ni mwiko kuchanganya dini na siasa. Sasa vipi tena hawa masheikh wanatoka Bagamoyo hadi Monduli kwenda kufanya siasa? Haya mambo mbona mimi yananikoroga kidogo?
Kweli TANU ya 1950s wakati Tanganyika inadai uhuru kilikuwa chama cha masheikh - Mufti Sheikh Hassan bin Amir, Sheikh Mohamed Ramia, Sheikh Yusuf Badi, Sheikh Issa Nasir, Sheikh Suleiman Takadir, Sheikh Haidar Mwinyimvua na wengine wengi lakini mbona hawa staili yao ya siasa ilikuwa tofauti na hawa masheikh wa miaka hii?
Hakuna popote kwenye historia inapoonyesha Sheikh Hassan bin Amir alitoka mguu mosi mguu pili kwenda kwa Nyerere kumshawishi...nahema...
Bunge la Katiba kasimama Sheikh anasema yeye usiku kucha hakupata usingizi...kisa nini? Anasema Baba wa Taifa katukanwa ghafla akaanza kuangua kilio...huyu sheikh hivi sasa ni "kadhi," wa BAKWATA kapanda cheo. Alikuwa sheikh wa BAKWATA sasa kaongezwa cheo kingine kawa kadhi wa BAKWATA...
Turudi kwa masheikh wa Bagamoyo...mtu yoyote aliyekaribu na masheikh hasa wa vijijini kama Msoga, Msata, Lugoba, utaona hali zao...taaban hali zao ngumu cha kutia mdomoni wanakitafuta.
Masheikh hawa wa Bagamoyo nikiwaangalia kwenye picha...Mashaallah kanzu zinameremeta na wakapata nauli ya kutoka Bagamoyo hadi Monduli na kurudi na masurufu ya njiani na ya kuacha nyuma nyumbani...
Kweli masheikh wa BAKWATA wajanja lakini hawa wa Bagamoyo wamewapiku masheikh wa BAKWATA, hawawawezi hawa... hii ni lligi nyingine kabisa...
Kuna msemo mpya vijana wamekujanao kuna masheikh wanaitwa, "Masheikh Ubwabwa."
Watengenezaji filamu wa Hollywood ni hodari kweli kweli wanaweza kukuwekea kitu kinaitwa "set," wakajenga mji wa Bagamoyo kama ulivyokuwa wakati wa Wajerumani na ukahisi khasa hiki ninachoona sasa hivi kwenye senema ndiyo wakati wenyewe miaka 100 iliyopita...hii ya hawa masheikh wa Bagamoyo nadhani mafundi wa Hollywood wakiiona watalia ngoa.
Hii ni zaidi ya uigizaji wa mtu kuchukua "Oscar." Afrika Kusini unaweza kukodi, "waliaji,'' wakaja "kukulia," kwenye msiba wa mama yako.
Bagamoyo Khalifa wa Tariqa Kadiriyya ni mtoto wa Sheikh Mohamed Ramiya, Sheikh Abdulkadir Ramiyya...sidhani kama Sheikh Abdulkadir ana taarifa ya safari hii ya "murid," wake kwenda Monduli... na hii nasema tu maana huenda hawa, "masheikh,'' si Tarika Kadiriyya...
Piga ua lakini Bagamoyo sheikh gani atakuwa si wa Zawiyya ya Sheikh Mohamed Ramiyya?
Kwa ndugu zetu Wakristo "Zawiya," ni sawasawa na "KIgango."
Sasa kweli Mkristo safi anaweza kutoka nje ya Kigango na akasalimika?
Au siku hizi juu ya kuwa na masheikh kutoka Chuo Cha Sanaa Cha Bagamoyo kuna "masheikh mamluki" kuongeza katika "masheikh ubwabwa?
Sheikh Abdikadir bin Sheikh Mohamed Ramiyya
Khalifa wa Tariqa Qadiriyya Bagamoyo
Written By Mohamed Said on Saturday, March 21, 2015 | 12:14 PM
![10942489_893855877341652_2687773226950844526_n.jpg](/proxy.php?image=https%3A%2F%2Ffbcdn-sphotos-b-a.akamaihd.net%2Fhphotos-ak-xaf1%2Fv%2Ft1.0-9%2F10942489_893855877341652_2687773226950844526_n.jpg%3Foh%3Ddfcdc742c4397b7eef8fd731b46ad065%26oe%3D5572A977%26__gda__%3D1437633478_a42312fb7d2e63ad5611e283b0af561c&hash=5bd5e371c3e246117cad19aa32a4a8da)
LOWASA NI CHAGUO LA MUNGU
SIMAMA NA UHESABIWE
Hii picha nimeipata katika mtandao. Nilipokuwa naitazama kinywa kimenikauka mate. Najiuliza hivi hii taasisi ya usheikh mbona ghafla imekuwa taasisi ya vichekesho? Hawa masheikh wa Bagamoyo wanatoka Bagamoyo ipi? Hawa masheikh wanatoka misikiti au madrasa ipi? Huu usheikh siku hizi imekuwa ya mpata mpatae yaani mtu akivaa kanzu, koti na kofia tayari keshakuwa sheikh?
Sasa wazo jingine likawa linanijia....Tanzania ni mwiko kuchanganya dini na siasa. Sasa vipi tena hawa masheikh wanatoka Bagamoyo hadi Monduli kwenda kufanya siasa? Haya mambo mbona mimi yananikoroga kidogo?
Kweli TANU ya 1950s wakati Tanganyika inadai uhuru kilikuwa chama cha masheikh - Mufti Sheikh Hassan bin Amir, Sheikh Mohamed Ramia, Sheikh Yusuf Badi, Sheikh Issa Nasir, Sheikh Suleiman Takadir, Sheikh Haidar Mwinyimvua na wengine wengi lakini mbona hawa staili yao ya siasa ilikuwa tofauti na hawa masheikh wa miaka hii?
Hakuna popote kwenye historia inapoonyesha Sheikh Hassan bin Amir alitoka mguu mosi mguu pili kwenda kwa Nyerere kumshawishi...nahema...
Bunge la Katiba kasimama Sheikh anasema yeye usiku kucha hakupata usingizi...kisa nini? Anasema Baba wa Taifa katukanwa ghafla akaanza kuangua kilio...huyu sheikh hivi sasa ni "kadhi," wa BAKWATA kapanda cheo. Alikuwa sheikh wa BAKWATA sasa kaongezwa cheo kingine kawa kadhi wa BAKWATA...
Turudi kwa masheikh wa Bagamoyo...mtu yoyote aliyekaribu na masheikh hasa wa vijijini kama Msoga, Msata, Lugoba, utaona hali zao...taaban hali zao ngumu cha kutia mdomoni wanakitafuta.
Masheikh hawa wa Bagamoyo nikiwaangalia kwenye picha...Mashaallah kanzu zinameremeta na wakapata nauli ya kutoka Bagamoyo hadi Monduli na kurudi na masurufu ya njiani na ya kuacha nyuma nyumbani...
Kweli masheikh wa BAKWATA wajanja lakini hawa wa Bagamoyo wamewapiku masheikh wa BAKWATA, hawawawezi hawa... hii ni lligi nyingine kabisa...
Kuna msemo mpya vijana wamekujanao kuna masheikh wanaitwa, "Masheikh Ubwabwa."
Watengenezaji filamu wa Hollywood ni hodari kweli kweli wanaweza kukuwekea kitu kinaitwa "set," wakajenga mji wa Bagamoyo kama ulivyokuwa wakati wa Wajerumani na ukahisi khasa hiki ninachoona sasa hivi kwenye senema ndiyo wakati wenyewe miaka 100 iliyopita...hii ya hawa masheikh wa Bagamoyo nadhani mafundi wa Hollywood wakiiona watalia ngoa.
Hii ni zaidi ya uigizaji wa mtu kuchukua "Oscar." Afrika Kusini unaweza kukodi, "waliaji,'' wakaja "kukulia," kwenye msiba wa mama yako.
Bagamoyo Khalifa wa Tariqa Kadiriyya ni mtoto wa Sheikh Mohamed Ramiya, Sheikh Abdulkadir Ramiyya...sidhani kama Sheikh Abdulkadir ana taarifa ya safari hii ya "murid," wake kwenda Monduli... na hii nasema tu maana huenda hawa, "masheikh,'' si Tarika Kadiriyya...
Piga ua lakini Bagamoyo sheikh gani atakuwa si wa Zawiyya ya Sheikh Mohamed Ramiyya?
Kwa ndugu zetu Wakristo "Zawiya," ni sawasawa na "KIgango."
Sasa kweli Mkristo safi anaweza kutoka nje ya Kigango na akasalimika?
Au siku hizi juu ya kuwa na masheikh kutoka Chuo Cha Sanaa Cha Bagamoyo kuna "masheikh mamluki" kuongeza katika "masheikh ubwabwa?
![Moh%27dSaid_Ramiya_120912_IMG_1367.jpg](/proxy.php?image=https%3A%2F%2Flh5.googleusercontent.com%2F-_m0pR3SIMew%2FVQ43WFPQ2qI%2FAAAAAAAAX6U%2FIjRTZI_NY8Y%2Fw266-h480-no%2FMoh%2527dSaid_Ramiya_120912_IMG_1367.jpg&hash=b035ab021ef264108b3e319c3cb13e86)
Sheikh Abdikadir bin Sheikh Mohamed Ramiyya
Khalifa wa Tariqa Qadiriyya Bagamoyo