Taarifa ziara ya rais Kikwete nchini Uingereza

Taarifa ziara ya rais Kikwete nchini Uingereza

Hapa naona wazi rais amepoka kazi ya balozi na waziri wa mambo ya nje.
 
Kwani wewe una matatizo na ushoga? mbona hatukuoni ukipinga wazi wazi kwa kuwapopoa na mawe hadharani?

Kwani kuwapinga sharti uwapopoe na mawe; we m......ge nini? Huoni wanavyofanya viongozi kama Museveni na Mugabe wenye matatizo na ushoga.
 
Nimekaa na kujiuliza kitu nimeshindwa kupata jibu nimekuja na jambo hili ambalo siitaj tulichangie kisiasa bali tuvae viatu vya wanauchumi na tulijadili.
Najiuliza kwanini serekali isiwatume wataalamu wake ambao pengne wana uwezo wa kuwaelekeza hao wawekezaji vizur kuliko kuwapeleka mawazir 7 na mkuu wa kaya ambapo ni gharama kubwa,au kwanin asingeenda membe ambaye ndiye wazir wa kimataifa na jopo la wataalamu toka wizara hizo 7 na ofisi moja ya mkuu wa mkoa? nakumbuka wakati obama akija huku alikuja na wataalamu wake tu na wale wawekezaji akubeba mawaziri?
Je hamna namna inayoweza kufanyika tukawatumia watanzania wenzetu kuwekeza kwenye hii miradi baada ya kuwatafuta wawekezaj wagen ambao wanapewa na misamaha ya kodi juu? Namtakia rais na jopo lake mafanikio katika mwaliko huo walio nao na natumain hata mikataba itakuwa ya waz hao wawekazaj wakipatikana kama ilivyo upigaj wa kura tuloanza kuujaribu hapa nchin

mkuu,hata mke wake nae ameenda,kwan nae anahusika na kutafuta wawekezaji?
 
wamesahau kuandika kuwa kasaini na mjataba wa ushoga...

Hapo yule naibu waziri wetu CHEMBA hawezi kudhubutu kusema rasimu ya Katiba ya CCM inataka kuleta USHOGA Tanzania. Kimyaaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
Mkuu usishangae kuona hilo. Sasa hivi huko serikalini mambo haya ya kuandika yamekosa weledi kabisa maana ni hovyohovyo.
Sasa hicho ni cheo chake na bado anashindwa kukiandika ipasavyo unategemea nini.
Siku moja niliona mkubwa fulani kaandika kisha huku chini katamka cheo chake kama; KAMISHNA MWANDAMIZI WA POLISI MSAIDIZI. Nilichoka kabisa.


Sent from my iPad using JamiiForums

KISWAHILI kigumu jamani! Wabongo wengi hufikiri Kidhungu ndio kigumu na utaona.
 
Mhh nimemsema sana huyu bwana, wacha nikae kimya nisijeonekana nina ghubu!
 
Muda wake uishe tu, kodi zetu zinavyochezewa
 
....ikulu wanapotoa taarifa ya safari za JK wawe pia wanasema atakuwa na mawaziri wangapi na wanakwenda na rais nje kwa majukumu gani....maana imekuwa kawaida kwa rais JK kusafiri nje na lundo la mawaziri....huku serikali yake ikilalamika hawana hela...ama wafadhili hawatoi hela.....Sasa hela zitoke wapi wakati zinatafunwa kwenye ziara kama hizi za JK???....maana nimeona kwenye trip hii kuna mawaziri kamili si chini ya wanne(Mwakyembe, Muhongo, Mwinyi, Makamba)...hapo hujaweka wanaotoka ZNZ....Sasa kwa safari ya siku 3 tu unasafiri na lundo la mawaziri wanini???....wakati amealikwa rais...na yatakayofanyika yanaweza hata kufanywa na maafisa wa ubalozi wa TZ UK.....Inauma jinsi hela za walipa kodi zinavyotafunwa kwa kweli.....Inasikitisha zaidi serikali inaposema haina hela....au bajeti haina hela!!....zitoke wapi hela wakati zinatumika kwa perdiem za JK na msururu wake wa wapambe nje!!
 
Loh! Maskini Kikwete hajui kuwa HAKUNA URAFIKI KATI YA MASKINI NA TAJIRI.............

Unapaswa uelewe kuwa bila maskini hakuna tajiri na bila tajiri hakuna maskini.

Kumbuka kuwa Tanzania si maskini, umaskini walionao Watanzania wengi ni umaskini wa ujinga, kama wewe vile.
 
Kwani kuwapinga sharti uwapopoe na mawe; we m......ge nini? Huoni wanavyofanya viongozi kama Museveni na Mugabe wenye matatizo na ushoga.

Nilijua nina argue na mtu mwenye uwezo wa ku reason na akili timamu kumbe mwenzangu majinuni.

Bora nikuache ukajibizane na watu wenye uwezo kama wako.
 
Kenyatta baada ya miaka 5 ataigeuza kenya kuwa kama south africa ki maendeleo

unaongea ukweli mkuu, jamaa yuko buzy na maswala ya nchi yake,
ila mukulu wetu ni kutalii,
uwezi kuwa ombaomba ukawa tajiri!
 
chonde chonde waingereza wawekeze kwa kila kitu ila SI USHOGA.
hatuna rasilimali za kufanya mashoga. taifa letu linahitaji nguvu kazi ya kutosha kwa maendeleo yetu

Msiwe kama Uganda. Waingereza hawana neno kama mnaunga mkono ushoga.
 
unaongea ukweli mkuu, jamaa yuko buzy na maswala ya nchi yake,
ila mukulu wetu ni kutalii,
uwezi kuwa ombaomba ukawa tajiri!

Kaka ukiwa masikini huwezi kuwa na ndoto ya utajir hata siku moja
 
Alipokutana na hao watanzania aliwaeleza nini juu ya uchakachuaji wa maoni ya watanzania uaofanywa na yeye na chama chake katika uandishi wa katiba mpya?
 
Kwa utawala wa hwa watu na hasa hii regime ya sasa kwao unavyoiona Tanzania wao wanaamini na wameridhika kuwa iko sawa. Kilichopo ni "it is our time to eat" na ndio maana akitoka baba basi anamuachia mtoto au binamu.
Kitu kinaitwa gharama wao ni pale wanapoona kuna makusanyo hazina basi ni lazima ifanyike mbinu yoyote ile pesa 'ziyeyuke', chukulia mfano wa mchakato wa katiba ambapo pesa nyingi zinatumika huku watu wachache wakiwa wanajua majibu katika kile kiitwacho 'utake usitake'.
Japo yote ni ccm lakini tunasikia waliotangulia waliacha balance (B/CF) pale hazina mfano pesa za EPA nk, ngoja tusubirie mwaka mmoja tuone mkulu ataacha balance kiasi gani pamoja na hili deni la taifa linalopanda kila kukicha.

Omujubi; ki uhalisia hawezi kuacha balance yoyote pale hazina kwa kuwa tayari tuna deni la trilio n 20 wakati yeye alipo ingia alikuta nchi haina madeni na fedha za kigeni alizikuta hazina.
 
Hiyo press release inaanza hivi; "Uiengereza inajivunia kuongoza katika uwekezaji nchini Tanzania...". Hivi Ikulu ya Tanzania haikuona kasoro na hiyo paragraph? Hapo ni sawa ma kujigeuza kuwa wasemaji wa serikali Uiengereza!

Halafu rais amekutana na Mstahiki mayor wa London au LORD mayor wa London? Alderman Fiona Woolf ni LORD mayor na sio mstahiki. Mstahiki mayor wa London ni Boris Johson. Rais amekutana na nani?
 
Unapaswa uelewe kuwa bila maskini hakuna tajiri na bila tajiri hakuna maskini.

Kumbuka kuwa Tanzania si maskini, umaskini walionao Watanzania wengi ni umaskini wa ujinga, kama wewe vile.
kwa upande uko sahihi hasa kwa kuutaja umaskini wangu, nakupongeza japo wewe ulishindwa kuuona upuuzi wako pia. Ok kwahio kwakua hakuna maskini bila tajiri and vice versa unahitimisha kuwa ni sahihi huyo nanihii mwenzio kwenda kuwapigia magoti na kujichekesha huko ili ku-prove theory yako ya kipuuzi ya Uwepo wa Maskini na Tajiri? Uwe unawaza kwa kutumia kichwa sio ma'ka'li'o

Hiyo press release inaanza hivi; "Uiengereza inajivunia kuongoza katika uwekezaji nchini Tanzania...". Hivi Ikulu ya Tanzania haikuona kasoro na hiyo paragraph? Hapo ni sawa ma kujigeuza kuwa wasemaji wa serikali Uiengereza!
Halafu rais amekutana na Mstahiki mayor wa London au LORD mayor wa London? Alderman Fiona Woolf ni LORD mayor na sio mstahiki. Mstahiki mayor wa London ni Boris Johson. Rais amekutana na nani?
CC: FaizaFoxy
 
Last edited by a moderator:
kwa upande uko sahihi hasa kwa kuutaja umaskini wangu, nakupongeza japo wewe ulishindwa kuuona upuuzi wako pia. Ok kwahio kwakua hakuna maskini bila tajiri and vice versa unahitimisha kuwa ni sahihi huyo nanihii mwenzio kwenda kuwapigia magoti na kujichekesha huko ili ku-prove theory yako ya kipuuzi ya Uwepo wa Maskini na Tajiri? Uwe unawaza kwa kutumia kichwa sio ma'ka'li'o

CC: FaizaFoxy

Nchi hutembeleana, wanapokuja hapa wakuu wa nchi za nje, hao wa Uingereza wameshakuja hapa pia, unafikiri kwanini?

Dunia hii utafanya maendeleo kwa kutegemea yako tu, hata China wanakaribisha wageni kuwekeza.
 
Nchi hutembeleana, wanapokuja hapa wakuu wa nchi za nje, hao wa Uingereza wameshakuja hapa pia, unafikiri kwanini?

Dunia hii utafanya maendeleo kwa kutegemea yako tu, hata China wanakaribisha wageni kuwekeza.
Nadhani kuna wakati kichwa chako kinapata moto eeehhhhh
 
Back
Top Bottom