Taarifa ya Tume ya haki za binadamu kuhusu mauji ya mwangosi imethibitisha msajili wa vyama vya siasa alikiuka sheria na misingi ya demokrasia katika kushughurikia suala la vurugu za kisiasa iringa.
Suala la msingi ni kuwa, hii sio mara ya kwanza Tendwa kufanya makosa makubwa ya ukiukwaji wa sheria na misingi ya kazi yake kama hivi. Sasa ni wakati muafaka aondolewe ili apatikane msajili mwingine mwenye dhamira ya dhati ya kulea vyama na kukuza demokrasia ya vyama vingi. Kama mkurugenzi wa TPA, TBS, MSD n.k. wameondolewa Tendwa anabaki kwa masilahi ya nani?