Tatizo sio Mashine za EFD ,tatizo ni mfumo mzima wa uendeshaji wa hizi mashine .Hizi Mashine zinatambua mauzo tu na hazitambui gharama ,kwa maana ya kuwa utatozwa kodi ktk mauzo iwe umeuza kwa hasara au kwa faida kiduchu.
Sheria inakutaka mfanya biashara kutoa taarifa ndani ya SAA 24 kama hutofungua biashara,na faini ni mlioni 3 pamoja na kifungo juu au moja kati ya hizo.Sasa tujiulize unapopatwa na dharura zilizo nje ya ubinadamu kama ugonjwa kufiwa au vyovyote vile ni namna gani unaweza kukabiliana na hilo tatizo.
Sasa hivi Kariakoo hapafai ,T.R.A wanakamata wafanya biashara walioandika risiti za mkono(Za kitabu),wanamkamata mnunuzi na wanakamata mzigo...Wageni wamepungua kutokana na usumbufu huu ..
Zipo kero nyingi na Serikali imeziba masikio ,unaweza kuzuka mgogoro tena wa wafanya biashara kama Serikali hii itaendelea kutia pamba masikioni...