Taarifa: TRA kugawa mashine za EFD jijini Dar

Taarifa: TRA kugawa mashine za EFD jijini Dar

Kweli mtu aliyekuuzia kukufundisha na kwanini TRA wasifundishe walipa kodi ili aya malalamiko yasijirudie tena?

Hiyo nadhani itakua ngumu kidogo, ila wana idea nini cha ku expect kutoka kwako. Mashine zipo za aina nyingi na zinatofautiana kwenye jinsi ya kutumia, ila mwisho wa siku matokeo ni yale yale kwa maana report zinazohitajika.
Ni sawa na kuomba TIGO wakufundishe wateja kutumia simu zao,

Ni jukumu la supplier, aliyemuuzia mteja mashine kumfundisha kutumia mpaka aelewe kabisa, kwa maana mteja amelipia huduma hiyo. Hela aliyolipa kununulia mashine, ina jumuisha mafunzo na service kwa mwaka mzima.
 
Mashine zote za phaze II (kuanzia 2013) zinaingiza manunuzi pia, sema watu wenyewe hawatumii au hawajui. Ila manunuzi lazima yawe na risiti za EFD, so ukinunua mzio dai risiti. Kama hufahamu jinsi ya kuiniza, nenda kwa aliye kuuzia akuelekeze. kuiniza manunuzi ni rahisi kuliko hata kutoa risiti.

Na kitu kingine, mpaka sasa hivi, mfumo wa kodi ni ule ule, hamna kilichobadilika. unaweza uliza walioanza tumia mashine tokea 2013, hamna aliyeongezewa kodi kwasababu ametumia mashine, labda kama mtaji wake umekua.


Hivi unaweza kwenda singida kununua kuku wakakupa risiti hiyo unaisema?
 
Hauko sahihi boss.. nadhani kama kuna mfanya biashara mwenye VAT experience atujuze.

Pili mfanyabiashara mwenye VAT, yeye halipi VAT, anayelipa ni mnunuzi wa mwisho kabisa, ndio mana yeye anadai (claim) VAT TRA mwiho wa siku. kwa mfano wako uliotoa. bidhaa ya 8000 VAT yake ni 1440, na ameuza kwa 10,000 ambayo VAT yake ni 1800. Kiasi anachotakiwa kupeleka TRA ni 1800 - 1440 = 360 tu,

Pia kwa wafanya biashara wanachofanya, anaweka faida yake then juu yake anaweka kodi. kwa mfano wako, kama anataka kupata faida ya 2000. basi atauza 10,000 plus VAT. yaani 11800. Vininevyo watu wangefunga maduka, isingekua biashara.
Hapa kikubwa ni kupata elimu ya kodi, kutoka kwa watu wanaohusika na kodi. kama kuna wataalam watusaidie
kuna wakati biashara inakuwa ngumu mtu unaamua kuuza bei ya kununulia ili mradi usishinde njaa.. inakuwaje hapo?
 
Mkuu hizo hesabu za wapi?, TRA wanakata 18% ya mauzo yako na siyo 18% ya faida yako na ndiyo ugomvi na wafanyabiashara unapoaanzia
ndio mahesabu yalivyo boss, uliza mtu mwenye VAT. Ndio mana unasikia kila mwisho wa mwezi wanafanya kitu wanaita returns. na unaweza fanya hata online. Na ndio maana siku zote mtu mwenye VAT analazimika kununua kwa mtu mwenye VAT. wanaoingiza bandarini pia wana claim. jaribu kuuliza mtu mwenye VAT au kama una mhasibu unamfahamu.
Kama ulikua ufahamu na una VAT, please tafuta tax consultants akupe elimu ya VAT, otherwise utapata hasara.

Au jiulize, umeshawahi sikia mtu ambaye tayari yupo kwenye VAT akipiga mahesabu kama yako? au akilalamikia mfumo wa VAT kwamba unamnyonya?
 
Kuwakamata wakamatwe tu, hakuna namna.

Mimi ugomvi wangu ni kwa kanuni ya kuipata hiyo kodi. TRA wameshindwa kuainisha ni 18% ya kitu gani. Wao wanakata 28% ya mauzo ambayo ukiitafakari inakula hadi mtaji.

Mfano mauzo ya pukipi 1,800,000/-, hata kabla ya EFD, hiyo ndo bei. Na mfanyabiashara anafukuzia 50,000/- hadi 100,000 kwa mfano. Lakini 18% ya 1,800,000= ni 324,000/- ambayo imeingilia hadi mtaji. Hivyo wafanya biashara watafunga maduka yao.

Kwa nini hawafungi maduka?

1. Hujitahidi kutotumia mashine za efd. Baadhi ya maduka ukidai risit hiyo, uteja unaisha. Anachukua mali yake, anakurudishia pesa yake.
2. Huziharibu machine za efd ili zifanye yale watakayo.
3. Ni kuandika thamani ndogo kulinganisha na thamani halisi ya bidhaa iliyonunuliwa. Hii ndo inayotumika kwa wafanya biashara wengi.

Mfano, hiyo pkpk ya 1,800,000/- ambapo yeye anatafuta faida ya 50,000- hadi 100,000/-, ukinunua kwenye receipt ataandika let say 80,000/- ambayo kodi yake ni 14,400/-. Ukitoa kwenye 50,000/- atabaki na 35,600/- au ukitoa kwa 100,000/- atabaki na 85,600/- ili alipie chumba, leseni, wasaidizi, kodi ya anakoishi n.k

Hapo tra walifikiria kwa kutumia Masaburi.


Umeongea ukweli mkuu, ili mfanyabiashara asifunge biashara hapo kwenye pikipiki alipoweka 50,000/= kama faida itabidi aweke faida 1,000,000/= ili iuzwe 2,800,000/= VAT 504,000/= faida iwe 496,000/=
 
Tokea mwanzo mashine ni bure, tatizo elimu haikutolewa ya kutosha, na pia kutokua na tabia ya kuuliza wahusika sahihi, information nyingi tunapata mtaani ambazo zinakua si sahihi na siasa pia zikaingia tena juu yake.

Sheria ya EFD inavyosema, mfanyabiashara anaponunua mashine ya efd (moja au zaidi) kwa mara ya kwanza atarudishiwa pesa yake yote kwa njia ya kodi pindi atakapoanza kuitumia. Mfano alitakiwa alipe kodi milioni moja, na kanunua mashine laki nane basi atatakiwa kulipa kodi laki mbili tu. Kwa wale ambao huwa wanakwepa kodi, ndio watakua hawana namna ya kurejesha hela yao.
Mkuu upo sawa kabisa kisheria, ila Sheria ya kodi inazitaka mamlaka kukata kodi kwenye kipato Na ndani ya kipato kuna mtaji na faida Na ikumbukwe kua mtaji halipiwi kodi, kilio cha wafanya biashara huanzia hapa maana kupitia Sheria uliopo inayotambua EFD inaenda kinyume Na kifungu kinacho zitaka mamlaka zikate kodi kwenye faida ( kipato )Na si mtaji,
Na ikumbukwekwe kua mfanya biashara anapotoa risiti ya mashine za EFD ndani yake kuna mtaji Na faida achilia mbali gharama nyingine za ambazo hazitaingizwa kwenye mfumo huu Na mwisho wa siku inabidi mfanyabiashara akatwe kodi bila kujali mtaji Na faida ambapo inakua ni tofauti Na Sharia ya kodi inayomtaka mfanya biashara alipe kodi kutokana Na kipato anachokipata. Kwa maana nyingine hii ni legal problem inatakiwa kufanyiwa kazi kabla ya kulazimisha mambo,
Najua wapo watokwa povu wasiojua misingi ya kodi itakua ngumu kwa wao kuelewa.
 
ndio mahesabu yalivyo boss, uliza mtu mwenye VAT. Ndio mana unasikia kila mwisho wa mwezi wanafanya kitu wanaita returns. na unaweza fanya hata online. Na ndio maana siku zote mtu mwenye VAT analazimika kununua kwa mtu mwenye VAT. wanaoingiza bandarini pia wana claim. jaribu kuuliza mtu mwenye VAT au kama una mhasibu unamfahamu.
Kama ulikua ufahamu na una VAT, please tafuta tax consultants akupe elimu ya VAT, otherwise utapata hasara.

Au jiulize, umeshawahi sikia mtu ambaye tayari yupo kwenye VAT akipiga mahesabu kama yako? au akilalamikia mfumo wa VAT kwamba unamnyonya?


Hapa Kuna kitu imeniambia ni kipya kwangu hasa huyo ya kununua kwa mtu mwenye VAT
 
Mkuu upo sawa kabisa kisheria, ila Sheria ya kodi inazitaka mamlaka kukata kodi kwenye kipato Na ndani ya kipato kuna mtaji na faida Na ikumbukwe kua mtaji halipiwi kodi, kilio cha wafanya biashara huanzia hapa maana kupitia Sheria uliopo inayotambua EFD inaenda kinyume Na kifungu kinacho zitaka mamlaka zikate kodi kwenye faida ( kipato )Na si mtaji,
Na ikumbukwekwe kua mfanya biashara anapotoa risiti ya mashine za EFD ndani yake kuna mtaji Na faida achilia mbali gharama nyingine za ambazo hazitaingizwa kwenye mfumo huu Na mwisho wa siku inabidi mfanyabiashara akatwe kodi bila kujali mtaji Na faida ambapo inakua ni tofauti Na Sharia ya kodi inayomtaka mfanya biashara alipe kodi kutokana Na kipato anachokipata. Kwa maana nyingine hii ni legal problem inatakiwa kufanyiwa kazi kabla ya kulazimisha mambo,
Najua wapo watokwa povu wasiojua misingi ya kodi itakua ngumu kwa wao kuelewa.

Ni kweli boss, tatizo mpaka sasa hivi, mfumo wa mashine hautumiki ipasavyo especially kwa upande wa watu wasiokua na VAT. Walioko kwenye VAT hawana shida, wanatumia mfumo wa kufanya returns na siku hizi wanaweza fanya mpaka online unainiza risiti za mauzo na manunuzi huko.

Kwa watu ambao hawana VAT, tra inaendelea kuwakadiria kama ilivyokua awali, mahesabu ya mashine so far naona ni pale mfanyabiashara anapoomba kuingia kwenye VAT, ndio wataangalia kama kafikisha mauzo ya 100M ndani ya mwaka.
Ila mashine za sasa hivi zote, zinaingiza mauzo, pamoja na manunuzi as long as manunuzi yana risiti za EFD.
sema sasa, asilimia kubwa ya wafanyabiashara wanaotumia mashine hawajafundishwa kama kuna kuingiza manunuzi na kutuma report za manunuzi, na wanaojua hawafanyi hivyo, ni wafanyabiashara wachache wenye vitabu vya mahesabu, ndio mana weni wanaishia kukadiriwa, na makadirio hayatokani na mauzo ya EFD, mana inajulikana hazitumiki ipasavyo.
ndio maana hakuna mfanyabiashara ambaye ameonezewa kodi baada ya kuanza kutumia mashine.

Mimi nature ya kazi yangu na kutana na wafanyabiashara wengi wa kariakoo ambao wana mashine, na weni nimewauliza sana hilo swali. wenye mashine, wasio na mashine wote wanakadiriwa sawa.

Kwa wale wenye VAT na wanafanya kazi za restaurant, kuna namna yao ya kulipa kodi, mana inajulikana manunuzi yao meni hayana risiti. Hapo kama kuna wataala wa kodi watujuze zaidi.
 
Hapa Kuna kitu imeniambia ni kipya kwangu hasa huyo ya kununua kwa mtu mwenye VAT
Ukinunua kwa mtu mwenye VAT ndio utaweza claim hiyo VAT ukaja kuikata ukija fanya returns. Mfano umenunua kitu cha 1M VAT yake 180,000 hiko kiasi maana yake unakua unaidai TRA, unapokuja kufanya returns una claim. ukinunua kwa mtu asiyekua na VAT, imekula kwako, hela yote hiyo inapotea
 
Mi sijipi presha kila risiti nitoayo kwa bidhaa lazima nimuwekee mteja vat na namweleza kabisa kama hataki basi
 
kuna mfanyabiashara wa kuku ana VAT?
kwa kuongezea tu boss, bidhaa ambazo zinatozwa VAT ni zile ambazo zimeongezewa thamani. Vitu kama, mchele, unga, mahindi etc havina VAT mpaka pale vitakapokua processed. so hao kuku wa singida, hawana VAT ila endapo utawachukua, ukawachinja, ukawapack vizuri ukawapia lebo, ukiuza hapo watakua na VAT.
Kuwa na VAT haimaanishi kila kitu kina VAT, vipo vingine vingi kama madawa, solar equipments, baadhi ya raw materials, vifaa vya kilimo na uvuvi, etc
 
kwa kuongezea tu boss, bidhaa ambazo zinatozwa VAT ni zile ambazo zimeongezewa thamani. Vitu kama, mchele, unga, mahindi etc havina VAT mpaka pale vitakapokua processed. so hao kuku wa singida, hawana VAT ila endapo utawachukua, ukawachinja, ukawapack vizuri ukawapia lebo, ukiuza hapo watakua na VAT.
Kuwa na VAT haimaanishi kila kitu kina VAT, vipo vingine vingi kama madawa, solar equipments, baadhi ya raw materials, vifaa vya kilimo na uvuvi, etc


Tuseme nimewapark hao kuku watanikata kodi kwa mtindo gani ikiwa nimenunua bila risiti?
 
Umeongea ukweli mkuu, ili mfanyabiashara asifunge biashara hapo kwenye pikipiki alipoweka 50,000/= kama faida itabidi aweke faida 1,000,000/= ili iuzwe 2,800,000/= VAT 504,000/= faida iwe 496,000/=
Kweli mkuu kitu ambacho hakiwezekani mkuu. Hapo walishindwa kufikiri. Wangefanya hesabu zao ikawa 18% ya faida tarajiwa.

Hivyo walitakiwa kujua kila bidhaa ikitoka kiwandani inauzwaje, ili wafix hiyo 18% kwenye faida tarajiwa ya kuuza bei ya jumla.

Pia wajue mtu akinunua jumla naye anakuwa semi seper dealer, wajue anafikisha biashara hiyo dukani kwake kwa bei gani na atauza bei gani ili faida yake ijumuishwe na 18% ya serikali.

Then ndo waje kwa sisi wa reja reja. Hapo tutaenda sawa
 
Mkuu upo sawa kabisa kisheria, ila Sheria ya kodi inazitaka mamlaka kukata kodi kwenye kipato Na ndani ya kipato kuna mtaji na faida Na ikumbukwe kua mtaji halipiwi kodi, kilio cha wafanya biashara huanzia hapa maana kupitia Sheria uliopo inayotambua EFD inaenda kinyume Na kifungu kinacho zitaka mamlaka zikate kodi kwenye faida ( kipato )Na si mtaji,
Na ikumbukwekwe kua mfanya biashara anapotoa risiti ya mashine za EFD ndani yake kuna mtaji Na faida achilia mbali gharama nyingine za ambazo hazitaingizwa kwenye mfumo huu Na mwisho wa siku inabidi mfanyabiashara akatwe kodi bila kujali mtaji Na faida ambapo inakua ni tofauti Na Sharia ya kodi inayomtaka mfanya biashara alipe kodi kutokana Na kipato anachokipata. Kwa maana nyingine hii ni legal problem inatakiwa kufanyiwa kazi kabla ya kulazimisha mambo,
Najua wapo watokwa povu wasiojua misingi ya kodi itakua ngumu kwa wao kuelewa.
Ndo udhaifu wa kutumia efd mkuu. Sasa tutalalamika hadi lini? Waathirika wakuu ni super dealers na semi super dealers. Kwa nini kupitia jumuiya zao wasifungue kesi mahakamani kuomba ufafanuzi wa mahakama?
 
Back
Top Bottom