Ferruccio Lamborghini
JF-Expert Member
- Apr 15, 2020
- 1,664
- 2,517
TAARIFA KWA UMMA
Yah: TUHUMA ZA KULA ADA ZA WATOTO
UMOJA WA WANAUME WENYE KIPATO CHA KATI (UWAWEKIKA)
Tumesikitishwa na kauli za upotoshaji, kashfa, kejeli na matusi, dhidi ya wanachama wake kwa ujumla.
Tunalaani vikali maneno ya:
"Kizazi kilichokula ada wakati kinasoma, kimekula ada tena wakati kikisomesha."
Kwa kuwa maneno haya yamejaa dharau, kutusimanga na kutudhalilisha. Kwamba kukosa kwetu elimu kubwa kunahusishwa na utukutu wa kula ada.
UWAWEKIKA tunapenda kuweka kumbukumbu sawa kwamba:
"Pesa tulizokuwa tulipie ada kwa watoto wetu, tulitumia katika mazingira ya dharula yaliyojitokeza kutokana na COVID-19."
Katika mazingira kama yale, mlitaka tutunze ada badala ya kuokoa uhai wa watu wetu? Mpo timamu kichwani kweli?
Sisi kwa kauli moja tunasema, tulitumia pesa zile kusafirishia watoto kwenda vijijini kwa bibi zao. Na pia pesa hizo hizo tulitumia kununulia akiba ya vyakula.
Mwisho mkae mkijua kuwa pesa ikiwa mfukoni kwa mzazi, hakuna mwenye mamlaka wa kuita pesa hiyo ni ada. Bado itaitwa pesa ya matumizi tu. Na ada ni sehemu ndogo sana ya matumizi ya familia.
Imetolewa na:
Dk Levy (Escobar)
Msemaji wa Umoja wa Wanaume Wenye Kipato Cha Kati.
(UWAWEKIKA)
Dar es Salaam.
Yah: TUHUMA ZA KULA ADA ZA WATOTO
UMOJA WA WANAUME WENYE KIPATO CHA KATI (UWAWEKIKA)
Tumesikitishwa na kauli za upotoshaji, kashfa, kejeli na matusi, dhidi ya wanachama wake kwa ujumla.
Tunalaani vikali maneno ya:
"Kizazi kilichokula ada wakati kinasoma, kimekula ada tena wakati kikisomesha."
Kwa kuwa maneno haya yamejaa dharau, kutusimanga na kutudhalilisha. Kwamba kukosa kwetu elimu kubwa kunahusishwa na utukutu wa kula ada.
UWAWEKIKA tunapenda kuweka kumbukumbu sawa kwamba:
"Pesa tulizokuwa tulipie ada kwa watoto wetu, tulitumia katika mazingira ya dharula yaliyojitokeza kutokana na COVID-19."
Katika mazingira kama yale, mlitaka tutunze ada badala ya kuokoa uhai wa watu wetu? Mpo timamu kichwani kweli?
Sisi kwa kauli moja tunasema, tulitumia pesa zile kusafirishia watoto kwenda vijijini kwa bibi zao. Na pia pesa hizo hizo tulitumia kununulia akiba ya vyakula.
Mwisho mkae mkijua kuwa pesa ikiwa mfukoni kwa mzazi, hakuna mwenye mamlaka wa kuita pesa hiyo ni ada. Bado itaitwa pesa ya matumizi tu. Na ada ni sehemu ndogo sana ya matumizi ya familia.
Imetolewa na:
Dk Levy (Escobar)
Msemaji wa Umoja wa Wanaume Wenye Kipato Cha Kati.
(UWAWEKIKA)
Dar es Salaam.