T-Shirts: Gwajimarize Tzii or Gwajimarize Tanganyika

T-Shirts: Gwajimarize Tzii or Gwajimarize Tanganyika

Boreless

Member
Joined
Aug 25, 2009
Posts
67
Reaction score
45
Wakuu Salaam,

Nchi yetu kwa hakika inapitia njia na kipindi cha mseleleko kuelekea kwenye giza totoro. Kwa kila raia ambaye bado ana nuru ya kung’amua yanayoendelea, shime afanye lililo ndani ya uwezo wake kukataa mseleleko huu wa kulekeza nchi gizani.

Nakusudia kuchapicha T-shirts zenye nembo na kauli mbiu “Gwajimarize Tzii” or “Gwajimarize Tanganyika” ili zitusaidie tulio tayari kusimama kuhesabiwa kupeleka ujumbe kwa wanaotuongoza kuelekea gizani.

Naomba maoni yenu juu ya kauli mbiu na njia salama ya kusambaza T-shirts ili ujumbe ufike kwa kishindo.
 
Kwann Gwajima? Ni wangapi wametoka wakazungumzia utekaji na haujafikiri kuwaweka kwenye tshirts? "No reform no election" ingekuwa na maana zaidi.
 
Gwajimanization

Logo weka mkono umekunja ngumi inatazama juu na mkono uwe na rangi ya bendera ya taifa

Nipewe zawadi ya t shirt moja nyeusi kama wazo langu litatendewa kazi
 
Kwann Gwajima? Ni wangapi wametoka wakazungumzia utekaji na haujafikiri kuwaweka kwenye tshirts? "No reform no election" ingekuwa na maana zaidi.
Ni kweli wengi wamejitokeza kulaani utekeaji na mauaji lakini tamko la Gwajima kwa kiwango kikubwa limewapiga kwenye mshono kiasi cha Mkuu wa nchi kutoa kauli. Na kupitia kauli ya Mkuu wa nchi, ndiyo tunatengeneza kauli mbiu ya T-Shirt yetu ili kumuonyesha kwamba tamko la Gwajima ni kauli ya wananchi
 
MWALIMU NYERERE ANAMALIZA KWA USHAIRI KWENYE KITABU CHAKE.

Ole wake Tanzania Tusipoisaidia
Niwezalo nimelifanya kushauri na kuonya nimeonya.

Tahadhali nimetoa ushauri na kuonya nimeshatoka kitini zaidi nifanye nini.

Namlilia Jaalia atumulikie njia Tanzania ailinde WAOVU wasiishinde.

Amina Tena Amina Amina Tena amina

UONGOZI WETU NA HATMA YA TANZANIA.
MWALIMU JK NYERERE
 
Say less.
20250531_1337_Green Tanzania Shirt_remix_01jwjyky38fvqbgch19s37w2js.png
 
Back
Top Bottom