It is in the public domain now and should be accessible on demand.
Mi nimeipata kwa njia ninazo zijua mimi, ukitaka nitakutumia na wewe
Nimeridhika kua wana 95% of confidence, sample ya 2000 people
Rural and urban area reflective, gender balanced na standards zingine zote
utafiti wakupika huu
"Izo" ni kitu gani?
Unataka kuongelea elimu wewe? Ungejua lolote kuhusu elimu ungejua utafiti bila sample space, methodology na margin of error ni hadithi tu.
Hivi si vitu vipya useme hamna standards. Gallup has been doing this for over 77 years.
Judging from your comment I doubt you even know what Gallup is.
tehetehe, unajua nyie mnaojiita wasomi mnajichekesha. Owk unajua hesabu so?margin of error and so forth, misamiati mizitomizito unamwambia nan? uko unakowasemea 60% ya population n degree holder, apa form4 hajui kusoma wala kuandika wacha kuelewa. it seems you dont know where and who are you?
Hivi mtu unawezaje kuandika habari yooooote hii, na kuweka asilimia zooote hizo, bila kutoa sample space ilikuwa vipi (watu wangapi, kutoka wapi etc) na methodology iliyotumika ( wamepewa questionnaires, wamepigiwa simu etc).
Gazeti lina mhariri hili?
Tutajuaje kama sample space si madarasa mawili ya shule moja ya sekondari yanayojumuisha wanafunzi waliojichokea na kujaza questionnaires randomly kama sehemu ya adhabu ya utovu wa nidhamu?
NB: The original post has been updated with more details since this post demanded a better explanation.
Unapoandika utafiti wako,kumbuka asilimia lazima ziendane na namba ya sample uliwahoji,otherwise iwe inajulikana na watu unawaandikia utafiti huo.
Mkuu Regan Morgans, kama haya ni matokeo ya utafiti, sasa hii ya wewe kuuliza kama jee ni kweli, unamaana unamashaka na utafiti huu wa Synovate?.
Kwa kusaidia tuu, sio tuu ni kweli kabisa kuwa EL anaanza kukubalika
zaidi, bali baadhi ya Watanzania wanaanza kuukubali ukweli kuwa EL ni jembe la ukweli!.
Haya maroroso tunayoyashuhudia katika kuporomoka kwa elimu yetu ni baadhi tuu ya matokeo ya serikali dhaifu ya JK kuitelekeza mipango ya EL na shule za kata ili kumkomoa, sasa imejikuta yenyewe ndio inakomoleka na kufikia 2015, EL atakuwa juu kabisa on top of the charts ili kufungua tuu njia na kunyoosha mapito ya "the chosen one!".
" Jiwe walilolikataa waashi, litafanywa kuwa jiwe kuu la pembeni!".
Yeye ndie ule mwamba wa Kaskazini unaozungumziwa kwenye maandiko mbalimbali kuwa
"Wewe ni mwamba, juu ya mwamba huu, nitalijenga taifa langu!".
Pasco.
Mkuu Mwakichi, kumbe Pasco wa jf anatumika?!, analipwa milioni 10 ambazo hazimpeleka popote zaidi ya kupata nuksi na mikosi (kama ile ajali!), na na kuirudia familia yake!.Kaka kaka!!acha kutumika kaka, ukila leo mil 10 hizo hazikupelek popote zaid ya kupata nuksi na mikos toka kwa watz na zitarudia familia yako siku moja
Don't expect honestly from cheap people!!don be cheap
Sikubaliani hata kidogo na matokeo niliyoyaona gazeti la leo la mwananchi kwani hao waliotolewa wote ni kwasababu ya kujuana na urafiki na kupigiana promo, mimi nasema huo ni utafiti feki mimi DEOGRATIUS KISANDU ndiye ninaye ongoza mpaka sasa kwa asilimia 35% lakini ukweli umefichwa.
Sikubaliani hata kidogo na matokeo niliyoyaona gazeti la leo la mwananchi kwani hao waliotolewa wote ni kwasababu ya kujuana na urafiki na kupigiana promo, mimi nasema huo ni utafiti feki mimi DEOGRATIUS KISANDU ndiye ninaye ongoza mpaka sasa kwa asilimia 35% lakini ukweli umefichwa.
WAKATI baadhi ya wanasiasa wakiwa wameanza kujiwinda kwa ajili ya kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu wa 2015, Shirika la Utafiti la Synovate limetoa matokeo ya utafiti wake ambao unaonyesha vigogo tisa kuwamo katika mchuano huo.
Utafiti huo umeonyesha kuwa endapo uchaguzi huo ungefanyika sasa, Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Willibrod Slaa angeibuka mshindi baada ya kuongoza orodha hiyo akipata asilimia 17.
Katika matokeo ya utafiti huo uliofanywa Desemba mwaka jana, Dk Slaa anafuatiwa kwa mbali na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ambaye amefungana na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe kila mmoja akipata asilimia tisa.
Hata hivyo, licha ya kuongoza, Dk Slaa ameporomoka kwa asilimia 25 ikilinganishwa na matokeo ya utafiti kama huo uliofanywa na taasisi hiyo mwaka 2011 ambapo alipata asilimia 42.
Kadhalika, umaarufu wa Pinda ambaye anaongoza miongoni mwa wagombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), umeshuka kwa asilimia tatu kutoka 12 za mwaka juzi, wakati Zitto ameendelea na kiwango kilekile cha asilimia tisa alizopata katika utafiti uliotangulia.
Wengine wanaofuata na asilimia walizopata kwenye mabano ni Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli (8), Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa (7) na Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba (5).
Pia wamo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe (4) ambaye amefungana na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe (4) na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta (2).
Ikilinganishwa na utafiti wa 2011, Lipumba ameporomoka kwa asilimia tisa.
Lowassa amepanda kwa asilimia sita, Dk Magufuli asilimia nne, Mbowe na Membe wamepanda kwa asilimia mbili kila mmoja, wakati Sitta amebaki katika kiwango kilekile cha asilimia mbili.
Hata hivyo, utafiti huo umeonyesha kuwa wananchi ambao hawana uamuzi wa kuchagua mtu yeyote kati ya hao kwa sasa ni asilimia 18, likiwa ni ongezeko la asilimia 12 ikilinganishwa na utafiti uliotangulia.
CCM yatamba
Katika utafiti huo, CCM kimeonyesha kuwa ni chama ambacho asilimia 52 ya wananchi wangependa kujiunga nacho, kikiwa kimepanda chati kwa asilimia moja kutoka asilimia 51 mwaka jana.
Kwa upande wa Chadema, wananchi ambao wanapenda kujiunga nacho imeshuka kutoka asilimia 35 mwaka 2011 hadi 31 mwaka jana.
Uwezekano mkubwa wa CCM kupanda chati ni kutokana na ukweli kuwa mwaka jana kilikuwa na uchaguzi ulioanzia ngazi ya mashina hadi taifa na kuibua vuguvugu kubwa masikioni mwa wananchi.
Chadema hakikuwa na harakati kubwa za kisiasa ukiacha kampeni ya Movement For Change (M4C), ambayo kwa kiasi haikuwa na pilika kama uchaguzi wa CCM.
Chama kingine ni CUF ambacho kimeporomoka kwa kupata asilimia 10 mwaka 2011 hadi nne mwaka 2012.
Hata hivyo, asilimia ya wananchi kutokutaka kujihusisha na chama chochote imepanda kutoka asilimia mbili mwaka 2011 hadi 12 mwaka 2012.
Rushwa
Katika suala la rushwa nchini, utafiti huo umeonyesha kuwa kati ya watu 10 waliohojiwa, wanne walikuwa na maoni kuwa rushwa imeongezeka kufikia asilimia 41, asilimia 30 walisema iko palepale, asilimia 23 walisema imepungua na asilimia tano hawajui.
Utafiti huo unaonyesha kuwa mapambano dhidi ya rushwa hayajabadilika tangu 2011katika taasisi za Serikali ukisema haionekani kama kuna utashi wa kisiasa kupambana na tatizo hilo katika taasisi hizo kama Jeshi la Polisi na Mahakama ambazo zimeonekana kuwa nyuma katika mapambano hayo.
Katika utafiti huo, polisi ndiyo inayoongoza kwa rushwa baada ya asilimia 33 ya watu waliohojiwa kulitaja jeshi hilo, ikifuatiwa na Mahakama asilimia 16 na sekta ya afya ikiwa na asilimia 16.
Utafiti huo umeonyesha matatizo makubwa yanayoikabili nchi kwa sasa ni njaa, gharama za maisha, umaskini, migogoro ya kidini na ukosefu wa ajira.
Asilimia 50 wametoa maoni kuwa njaa ni tatizo kubwa ikifuatiwa na gharama za maisha asilimia 44, migogoro ya ya kidini asilimia 43 na ukosefu wa ajira asilimia 34.
Inamaanisha kuwa rushwa na mfumuko wa bei havichukuliwi kama ni tatizo kwa Watanzania wengi kama ilivyojionyesha mwaka 2011, inaeleza taarifa ya utafiti huo.
Wananchi wameeleza kuwa mambo muhimu ambayo yanatakiwa kupewa kipaumbele ni pamoja na sekta ya afya kwa asilimia 24, elimu asilimia 21, ajira asilimia 18, chakula asilimia 17 na miundombinu asilimia 16.
Source: Mwananchi
[FONT=courier
new]WAKATI baadhi ya wanasiasa wakiwa wameanza
kujiwinda kwa ajili ya kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu wa 2015,
Shirika la Utafiti la Synovate limetoa matokeo ya utafiti wake ambao
unaonyesha vigogo tisa kuwamo katika mchuano huo.
Utafiti huo umeonyesha kuwa endapo uchaguzi huo ungefanyika sasa, Katibu
Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Willibrod Slaa
angeibuka mshindi baada ya kuongoza orodha hiyo akipata asilimia 17.
Katika matokeo ya utafiti huo uliofanywa Desemba mwaka jana, Dk Slaa
anafuatiwa kwa mbali na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ambaye amefungana na
Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe kila mmoja akipata asilimia
tisa.
Hata hivyo, licha ya kuongoza, Dk Slaa ameporomoka kwa asilimia 25
ikilinganishwa na matokeo ya utafiti kama huo uliofanywa na taasisi hiyo
mwaka 2011 ambapo alipata asilimia 42.
Kadhalika, umaarufu wa Pinda ambaye anaongoza miongoni mwa wagombea wa
Chama Cha Mapinduzi (CCM), umeshuka kwa asilimia tatu kutoka 12 za mwaka
juzi, wakati Zitto ameendelea na kiwango kilekile cha asilimia tisa
alizopata katika utafiti uliotangulia.
Wengine wanaofuata na asilimia walizopata kwenye mabano ni Waziri wa
Ujenzi, Dk John Magufuli (8), Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa (7)
na Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba (5).
Pia wamo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard
Membe (4) ambaye amefungana na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe (4)
na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta (2).
Ikilinganishwa na utafiti wa 2011, Lipumba ameporomoka kwa asilimia
tisa.
Lowassa amepanda kwa asilimia sita, Dk Magufuli asilimia nne, Mbowe na
Membe wamepanda kwa asilimia mbili kila mmoja, wakati Sitta amebaki
katika kiwango kilekile cha asilimia mbili.
Hata hivyo, utafiti huo umeonyesha kuwa wananchi ambao hawana uamuzi wa
kuchagua mtu yeyote kati ya hao kwa sasa ni asilimia 18, likiwa ni
ongezeko la asilimia 12 ikilinganishwa na utafiti uliotangulia.
CCM yatamba
Katika utafiti huo, CCM kimeonyesha kuwa ni chama ambacho asilimia 52 ya
wananchi wangependa kujiunga nacho, kikiwa kimepanda chati kwa asilimia
moja kutoka asilimia 51 mwaka jana.
Kwa upande wa Chadema, wananchi ambao wanapenda kujiunga nacho imeshuka
kutoka asilimia 35 mwaka 2011 hadi 31 mwaka jana.
Uwezekano mkubwa wa CCM kupanda chati ni kutokana na ukweli kuwa mwaka
jana kilikuwa na uchaguzi ulioanzia ngazi ya mashina hadi taifa na
kuibua vuguvugu kubwa masikioni mwa wananchi.
Chadema hakikuwa na harakati kubwa za kisiasa ukiacha kampeni ya
Movement For Change (M4C), ambayo kwa kiasi haikuwa na pilika kama
uchaguzi wa CCM.
Chama kingine ni CUF ambacho kimeporomoka kwa kupata asilimia 10 mwaka
2011 hadi nne mwaka 2012.
Hata hivyo, asilimia ya wananchi kutokutaka kujihusisha na chama
chochote imepanda kutoka asilimia mbili mwaka 2011 hadi 12 mwaka 2012.
Rushwa
Katika suala la rushwa nchini, utafiti huo umeonyesha kuwa kati ya watu
10 waliohojiwa, wanne walikuwa na maoni kuwa rushwa imeongezeka kufikia
asilimia 41, asilimia 30 walisema iko palepale, asilimia 23 walisema
imepungua na asilimia tano hawajui.
Utafiti huo unaonyesha kuwa mapambano dhidi ya rushwa hayajabadilika
tangu 2011katika taasisi za Serikali ukisema haionekani kama kuna utashi
wa kisiasa kupambana na tatizo hilo katika taasisi hizo kama Jeshi la
Polisi na Mahakama ambazo zimeonekana kuwa nyuma katika mapambano hayo.
Katika utafiti huo, polisi ndiyo inayoongoza kwa rushwa baada ya
asilimia 33 ya watu waliohojiwa kulitaja jeshi hilo, ikifuatiwa na
Mahakama asilimia 16 na sekta ya afya ikiwa na asilimia 16.
Utafiti huo umeonyesha matatizo makubwa yanayoikabili nchi kwa sasa ni
njaa, gharama za maisha, umaskini, migogoro ya kidini na ukosefu wa
ajira.
Asilimia 50 wametoa maoni kuwa njaa ni tatizo kubwa ikifuatiwa na
gharama za maisha asilimia 44, migogoro ya ya kidini asilimia 43 na
ukosefu wa ajira asilimia 34.
Inamaanisha kuwa rushwa na mfumuko wa bei
havichukuliwi kama ni tatizo kwa Watanzania wengi kama ilivyojionyesha
mwaka 2011, inaeleza taarifa ya utafiti huo.
Wananchi wameeleza kuwa mambo muhimu ambayo yanatakiwa kupewa kipaumbele
ni pamoja na sekta ya afya kwa asilimia 24, elimu asilimia 21, ajira
asilimia 18, chakula asilimia 17 na miundombinu asilimia
16.[/FONT][FONT=Times New
Roman]
[/FONT]
Source:
Mwananchi
Wamejitahidi kuchakachua asilimia za Dr. Slaa wakabakiwa na 17%! Yaani alipopambana na reigning president alikuwa juu, leo hii ashuke! Synovate acheni kutumiwa bana semeni ukweli halisi maana mmejua tofauti na kuonyesha Dr anaongoza wananchi wangewadharau maana huo ndio ukweli ambao hata kipofu anauona.