Synovate: Vinara tisa urais 2015

Synovate: Vinara tisa urais 2015

Utafiti unaofadhiliwa na Ikulu hutayarisha uchakachuaji wa matokeo tu. Mambo siyo hivyo kwa sasa. halafu hawa Wakenya wameikamata Ikulu kea ulaghai kama huo lakini yana mwisho
 
Sikubaliani hata kidogo na matokeo niliyoyaona gazeti la leo la mwananchi kwani hao waliotolewa wote ni kwasababu ya kujuana na urafiki na kupigiana promo, mimi nasema huo ni utafiti feki mimi DEOGRATIUS KISANDU ndiye ninaye ongoza mpaka sasa kwa asilimia 35% lakini ukweli umefichwa.

MODS tafuteni jukwaa maalum la watu kama hawa.
Hii ni Psychiatric case,tusilete masihara,jamaa inabidi awahishwe Mirembe haraka!!!
 
Hahaha... mtu anakaa kwenye keyboard anatengeneza research results...
 
Habari ya gazeti haijakamilika. Gazeti ni kama halina mhariri na muandishi ana "Pass" ya division four ya mkia isiyo na utashi (kuna nyingine zina utashi).

Ripoti unayoisema ni kamili iko wapi?
It is in the public domain now and should be accessible on demand.
Mi nimeipata kwa njia ninazo zijua mimi, ukitaka nitakutumia na wewe
Nimeridhika kua wana 95% of confidence, sample ya 2000 people
Rural and urban area reflective, gender balanced na standards zingine zote
 
Tafiti zisizo na mashiko hizi, inabidi vyuo vyetu vikiongozwa na UDSM vifanye utafiti yakinifu sii huu wa ubabaishaji wa Synovate!
 
Mmh, huo utafiti wa siri kama jando una la maana kweli?

Pamoja na yote, naomba kuuona kama inawezekana?

It is in the public domain now and should be accessible on demand.
Mi nimeipata kwa njia ninazo zijua mimi, ukitaka nitakutumia na wewe
Nimeridhika kua wana 95% of confidence, sample ya 2000 people
Rural and urban area reflective, gender balanced na standards zingine zote
 
Hivi mtu unawezaje kuandika habari yooooote hii, na kuweka asilimia zooote hizo, bila kutoa sample space ilikuwa vipi (watu wangapi, kutoka wapi etc) na methodology iliyotumika ( wamepewa questionnaires, wamepigiwa simu etc).

Gazeti lina mhariri hili?

Tutajuaje kama sample space si madarasa mawili ya shule moja ya sekondari yanayojumuisha wanafunzi waliojichokea na kujaza questionnaires randomly kama sehemu ya adhabu ya utovu wa nidhamu?

Safi saaana. Unajua waandishi wetu wengi ni wale waliishia darasa la 12 au 14 na kuanzia hapo hawajawahi kusikia kama kuna research na jinsi inavyofanyika. Hivyo hata wakipata habari za mtaani tu wanaweza kuzifanya kuwa ni findings za research. Fantastic
 
Mmh, huo utafiti wa siri kama jando una la maana kweli?

Pamoja na yote, naomba kuuona kama inawezekana?
Sio wa siri! umejaribu kwenda site yao? Au kuwaandikia on "contact us"?
Nitumie email yako via PM nikutumie. Mi mshamba, sijui kuu-post humu
Ngoja nimtumie Max mwenyewe aweke ripoti in this thread, as he does.
 
Sikubaliani hata kidogo na matokeo niliyoyaona gazeti la leo la mwananchi kwani hao waliotolewa wote ni kwasababu ya kujuana na urafiki na kupigiana promo, mimi nasema huo ni utafiti feki mimi DEOGRATIUS KISANDU ndiye ninaye ongoza mpaka sasa kwa asilimia 35% lakini ukweli umefichwa.


Kioja Cha Mwaka
 
Ngoja niusubiri auweke

Sio wa siri! umejaribu kwenda site yao? Au kuwaandikia on "contact us"?
Nitumie email yako via PM nikutumie. Mi mshamba, sijui kuu-post humu
Ngoja nimtumie Max mwenyewe aweke ripoti in this thread, as he does.
 
Wamejitahidi kuchakachua asilimia za Dr. Slaa wakabakiwa na 17%! Yaani alipopambana na reigning president alikuwa juu, leo hii ashuke! Synovate acheni kutumiwa bana semeni ukweli halisi maana mmejua tofauti na kuonyesha Dr anaongoza wananchi wangewadharau maana huo ndio ukweli ambao hata kipofu anauona.

Slaa hajawahi kumpiku reigning President hata siku moja labda kwa kura za JF mtandao ambao hauna shaka kuwa ni pro CDM. Hata hivyo ilikuwepo research bureau moja iliyoongozwa na Dr mmoja wa UDSM yeye ndio alifanya kituko cha mwaka kwa kutoa takwimu zikionyesha Slaa kuwa atashinda kwa 75%. Sample hizi za kuchukua hapa Dar es Salaam tena huko Kimara na Kawe au Tegeta au Moshi na Arusha zina bias kubwa na haziwezi kutumika kufikia hitimisho sahihi la kutegemewa ndio maana Slaa kaanguka kwa asilimia hizo alizozipata.
 
Tumeuona utafiti wenu Synovate, ingawa kuna shehemu silidhikinazo
 
KATIKA TAASISI NISIYOIAMINI NI HII SYNOVATE,WALLAH SIWAAMINI KWA LOLOTE HAWA,haswa huyo Bana ninamuona ana damu ya kifisadi na uoga uliojaa usaliti kwa wavuja jasho wa kitanzania.
 
Sikubaliani hata kidogo na matokeo niliyoyaona gazeti la leo la mwananchi kwani hao waliotolewa wote ni kwasababu ya kujuana na urafiki na kupigiana promo, mimi nasema huo ni utafiti feki mimi DEOGRATIUS KISANDU ndiye ninaye ongoza mpaka sasa kwa asilimia 35% lakini ukweli umefichwa.
kweli mkuu! utafiti unaonyesha unaongoza sana tu, hao sinoveti washenzi tu. mkuu 2015 wee ndo mkulu wetu.
 
Nawaomba ADMN wa JF waanze kuchunguza account ya bwana DEOGRATIUS KISANDU uwenda kukawa na hackers wanatumia bila ruhusa yake au kuna mtu katumia jina lake kwa ajili ya kumchafua,"maana si bure kwa mtu mwenye akili timam kupost kitu kama hicho" :frusty:
 
Utafiti huu ni wa kijinga na hauna maslahi kwa umma , jiulizeni ulifanyika maeneo gani , ni methodology gani zilitumika , nani walihusika na ripoti yake iko wapi? Huu ni muendelezo wa REDET , ikumbukwe REDET iliingiza rais wa tano , sasa Synovet ndio wanajiandaa kuingiza rais wa Sita , unapaswa kupingwa .......utafiti wa bar za walevi huu....mbona hawajasema lolote kuhusu katiba mpya? Kenya walifukuzwa ama wako wapi ? Hawa waliitwa Stead man uchaguzi wa Kenya 2007 ......leo wanajiita nani huko........
 
Mkuu Regan Morgans, kama haya ni matokeo ya utafiti, sasa hii ya wewe kuuliza kama jee ni kweli, unamaana unamashaka na utafiti huu wa Synovate?.

Kwa kusaidia tuu, sio tuu ni kweli kabisa kuwa EL anaanza kukubalika zaidi, bali baadhi ya Watanzania wanaanza kuukubali ukweli kuwa EL ni jembe la ukweli!.

Haya maroroso tunayoyashuhudia katika kuporomoka kwa elimu yetu ni baadhi tuu ya matokeo ya serikali dhaifu ya JK kuitelekeza mipango ya EL na shule za kata ili kumkomoa, sasa imejikuta yenyewe ndio inakomoleka na kufikia 2015, EL atakuwa juu kabisa on top of the charts ili kufungua tuu njia na kunyoosha mapito ya "the chosen one!".

" Jiwe walilolikataa waashi, litafanywa kuwa jiwe kuu la pembeni!".

Yeye ndie ule mwamba wa Kaskazini unaozungumziwa kwenye maandiko mbalimbali kuwa
"Wewe ni mwamba, juu ya mwamba huu, nitalijenga taifa langu!".

Pasco.

Nilivyoona kimya hapo katikati nikajua umekata tamaa, kumbe bado upo nae.!?
 
Back
Top Bottom