Swali la Wikiendi: Bosi akitoka na mdada kazini...

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
women-in-animation-group-combats-workplace-sexual-harassment.jpg
Swali la Kijamii: Watu wenye madaraka (mabosi) - nazungumzia wanaume hapa - na wako kwenye ndoa wanapoanzisha mahusiano na watu walio chini yao (subordinates) na wakazaa nao:

a. Wale kina dada/mama wanaweza kuwa wako huru kuwa na mapenzi na mabosi wao au wametumiwa kwa sababu ya uhusiano wa kikazi uliopo na ilikuwa vigumu kwao kukataa au kuacha?

b. Mwanamke ana njia gani ya kudai malezi ya mtoto kwa njia za kisheria (kupitia ustawi wa jamii) bila wakati huo huo kuweka hatarini ajira yake?

c. Kama bosi anahama kwenda sehemu nyingine kikazi na kusababisha mahusiano yale kuvunjika (au ya mbali) mwanamke mwenye mtoto ana namna gani ya kudai malezi au kuendelea na mahusiano na mtu ambaye siyo bosi wake tena?

d. Mtoto anayezaliwa katika mahusiano ya namna hiyo anaweza vipi kuanza kudai kumjua baba yake hasa kama baba hakumkubali au mama hakumwambia kwa kuhofia ama kumtibua mzazi mwenzie au kujikuta anamdhalilisha?

e. Mababa ambao ni mabosi na wamezaa nje ya ndoa zao, wanatakiwa kulazimishwa na sheria kuhakikisha wanahudumia watoto wao wengine kama vile kukata mishahara yao na kulazimisha watoto wawe kwenye bima zao za afya?

MMM
 
kuwa na mahusiano na boss yawe ya kulazimishwa au ya kimaslai ni jambo moja, na kuamua kubeba mimba ya Boss ni jambo lingine.

kwa mfano chukulia mfalme mmoja 'amemtamani' mwanamke ambaye ameolewa tayari, anaamua kumpa cheo mume wa yule mke kwenye himaya ya ufalme mwingine awe kama mwakilishi wake, ili yeye apate kumfaidi yule mke. katika hilo anaamua kumpa yule mke cheo kwenye uongozi wake wa kifalme, utamu unazidi, hatimaye mwanamke anabeba mimba, wakati mume wake bado yupo uhamishoni..

katika kisa hiki cha kubuni, mke huyu hawezi kusema amelazimishwa na mfalme huyu mwenye uchu.

kumbuka siku zote uamuzi wa kubeba ujauzito upo mikononi mwa mwanamke , labda awe amebakwa kwa nguvu.
 
Kwa mwanamke anayeingia katika mahusiano na bosi wake kwa hiari kabisa - ni ujinga kubeba mimba kwa makusudi au kwa uzembe, huku akijua bosi huyo ana mke na familia. Mama kama huyu anatakiwa kujilaumu mwenyewe kwa kuhangaishwa kuhusu matunzo ya mtoto.
 
We kwanin utembee na bos wako ukijua ana mke na watoto??? Ni ujinga huo
 
2 Samuel; Mlango 11

1 Hata ikawa, mwanzo wa mwaka mpya, wakati watokapo wafalme kwenda vitani, Daudi akampeleka Yoabu, na watumishi wake pamoja naye, na Israeli wote; wakawaangamiza wana wa Amoni, wakauhusuru Raba. Lakini Daudi mwenyewe akakaa Yerusalemu.
2 Ikawa wakati wa jioni, Daudi akaondoka kitandani, akatembea juu ya dari ya jumba la mfalme; na alipokuwa juu ya dari aliona mwanamke anaoga; naye huyo mwanamke alikuwa mzuri sana, wa kupendeza macho.
3 Naye Daudi akapeleka, akauliza habari za yule mwanamke. Mtu mmoja akasema, Je! Huyu siye Bath-sheba, binti Eliamu, mkewe Uria, Mhiti?
4 Basi Daudi akapeleka wajumbe, akamtwaa; naye akaingia kwake; naye akalala naye; (maana yule mwanamke amekwisha kutakasika unajisi wake); kisha akarudi nyumbani kwake.
5 Yule mwanamke akachukua mimba; basi akapeleka na kumwambia Daudi, akasema, Ni mja-mzito.
6 Ndipo Daudi akapeleka kwa Yoabu, akisema, Unipelekee Uria, Mhiti. Naye Yoabu akampeleka Uria kwa Daudi.
7 Uria alipomwendea Daudi, Daudi alimwuliza habari za Yoabu, na habari za watu, na habari za vita.
8 Daudi akamwambia Uria, Haya, shuka nyumbani kwako, ukanawe miguu yako. Basi Uria akatoka katika nyumba ya mfalme, na tunu ya vyakula ikamfuata, iliyotoka kwa mfalme.
9 Lakini Uria akalala mlangoni pa nyumba ya mfalme, pamoja na watumishi wote wa bwana wake, wala hakushuka nyumbani kwake.
10 Watu walipomwambia Daudi ya kwamba, Uria hakushuka nyumbani kwake, Daudi akamwambia Uria, Je! Hukutoka safarini? Mbona hukushuka nyumbani kwako?
11 Naye Uria akamwambia Daudi, Sanduku, na Israeli, na Yuda, wanakaa vibandani; na bwana wangu Yoabu, na watumishi wa bwana wangu, wamepiga kambi waziwazi uwandani; nami niende nyumbani kwangu, kula na kunywa, na kulala na mke wangu? Uishivyo, na kama roho yako iishivyo, mimi sitafanya jambo hili.
12 Basi Daudi akamwambia Uria, Ngoja hapa leo tena, na kesho nitakuacha kwenda zako. Basi Uria akakaa Yerusalemu siku ile, na siku ya pili yake.
13 Naye Daudi akamwalika, akala, akanywa mbele yake; naye akamlevya; hata wakati wa jioni akatoka kwenda kulala kitandani mwake pamoja na watumishi wa bwana wake, lakini hakushuka nyumbani kwake.Daudi Apanga Uria Auliwe
14 Hata ikawa asubuhi, Daudi akamwandikia Yoabu waraka, akaupeleka kwa mkono wa Uria.
15 Akaandika katika waraka huo, kusema, Mwekeni Uria mbele ya watu penye vita vikali, kisha ondokeni, mmwache, ili apigwe akafe.
16 Ikawa, Yoabu alipokuwa akiuhusuru mji, akamweka Uria mahali alipojua ya kuwa pana mashujaa.
17 Watu wa mji wakatoka, wakapigana na Yoabu; na baadhi ya watu, watumishi wa Daudi, wakaanguka; Uria Mhiti naye akafa.
18 Ndipo Yoabu akapeleka na kumwarifu Daudi habari zote za vita;
19 akamwagiza yule mjumbe, akisema, Ukiisha kumpa mfalme habari zote za vita,
20 itakuwa, hasira ya mfalme ikiwaka, akakuambia, Kwani mliukaribia mji namna ile ili kuupiga? Je! Hamkujua ya kuwa watapiga mishale toka ukutani?
21 Ni nani aliyempiga Ahimeleki, mwana wa Yeru-beshethi? Je! Si mwanamke aliyemtupia jiwe la kusagia la juu kutoka ukutani? Hata akafa huko Thebesi? Kwani kuukaribia ukuta namna ile? Ndipo utakaposema, Mtumishi wako Uria, Mhiti, amekufa naye.
22 Basi yule mjumbe akaenda, akafika na kumwonyesha Daudi yote aliyomtuma Yoabu.
23 Yule mjumbe akamwambia Daudi, Watu hao walitushinda, wakatutokea nje hata uwandani, tukashindana nao hata mahali pa kuingilia langoni.
24 Wapiga mishale wakatupiga sisi, watumishi wako, toka juu ya ukuta; na baadhi ya watumishi wa mfalme wamekufa, na Uria, Mhiti, mtumishi wako, amekufa naye.
25 Basi Daudi akamwambia yule mjumbe, Basi, mwambie Yoabu maneno haya, Jambo hili lisiwe baya machoni pako, maana upanga hula huyu kama unavyomla huyu; zidi kutia nguvu vita vyako juu ya mji ukauangushe; nawe mtie moyo.
26 Na yule mke wa Uria alipopata habari ya kuwa Uria mumewe amekufa, akamwombolezea mumewe.
27 Hata maombolezo hayo yalipokwisha, Daudi akatuma mtu, akamtwaa, akamtia nyumbani mwake; naye akawa mkewe, akamzalia mwana.Nathani Amlaani DaudiLakini jambo lile alilolitenda Daudi likamchukiza BWANA.
 
kuwa na mahusiano na boss yawe ya kulazimishwa au ya kimaslai ni jambo moja, na kuamua kubeba mimba ya Boss ni jambo lingine.

kwa mfano chukulia mfalme mmoja 'amemtamani' mwanamke ambaye ameolewa tayari, anaamua kumpa cheo mume wa yule mke kwenye himaya ya ufalme mwingine awe kama mwakilishi wake, ili yeye apate kumfaidi yule mke. katika hilo anaamua kumpa yule mke cheo kwenye uongozi wake wa kifalme, utamu unazidi, hatimaye mwanamke anabeba mimba, wakati mume wake bado yupo uhamishoni..

katika kisa hiki cha kubuni, mke huyu hawezi kusema amelazimishwa na mfalme huyu mwenye uchu.

kumbuka siku zote uamuzi wa kubeba ujauzito upo mikononi mwa mwanamke , labda awe amebakwa kwa nguvu.
Tena unakuta mwanamke ana mastazi au pihechidi.

Kugegedwa ni kawaida, kuzaa ni uamuzi maana hajalazimishwa kuzaa.
 
Na mtoto aliezaliwa aliitwa suleiman, aliyevunja rekodi ya kuwa na wanawake wengi.

Dhambi hufuatilia na hutafuna Suleiman utawala wake ulivunjika mara 2 kwa sababu ya wanawake.
 
Mtoto ni matokeo tu. Tatizo ni wote mwanaume na mwanamke. Kulinda kazi ni kisingizio tu cha kukwepa uhalisia wa matokeo. Wote mwanaume na mwanamke wanapaswa kuwa tayari kuwajibika. And this has to do with moral issues than legal ones.
 
Back
Top Bottom