sajo
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 3,026
- 5,258
Operation imepamba moto, vijana wanahimizana kukataa ndoa kwa kutokuoa ila hakuna anayepinga kuhusu suala la kujaza ulimwengu. Mizagamuano na misuguano inaleta sio tu raha na burudani kwa wafanyaji bali pia inaleta watoto kwenye dunia. Wakishakuja sasa wapenzi wanaanza kukimbiana na wengine kufikishana polisi kwenye madawati ya jinsia. Sasa basi kam yamekukuta ua hayakukuta, usiondoke bure hapa, kaa ujifunze kuhusu sheria ya mtoto na namna ya kuitumia.
SHERIA YA MTOTO YA MWAKA 2009
SHERIA YA MTOTO YA MWAKA 2009
Tunaendelea na masomo yetu ya Sheria kila mwezi. Somo la leo linahusu malezi, uangalizi na matunzo ya mtoto pale wazazi wake wanapokuwa hawapo pamoja kimahusiano. Wazazi wa mtoto wanaweza kumaliza mahusiano yao kwa talaka, kutengana au mapenzi kufa (ikiwa hawakuwa wanandoa) lakini kama walifanikiwa kuwa na watoto bado wana wajibu wa kuwatunza na kuwalea. Jambo hilo limekuwa gumu kufanyika (practical) kwani wazazi wengi wamekuwa na tabia ya kukomoana na matokeo ni madhara kwa watoto wao. Ndipo katika Mazingira haya, Serikali ikatunga sheria ya mtoto ya mwaka 2009 (imerejewa mwaka 2019) ili kuweza kuweka utaratibu wa kufuatwa kuhakikisha mtoto anapata matunzo na malezi vile ipasavyo.
Naitwa Lusajo W. Mwakasege, ni Mwanasheria, namba yangu ya simu ni 0713-368153 (inapatikana whatsapp In WhatsApp teilen na telegram) na telegram) na barua pepe yangu ni mwakasege@gmail.com. Tuanze somo letu:
MTOTO NI NANI?
Mtoto ni mtu yeyote mwenye umri chini ya miaka kumi na nane (18).
👉Kwa sheria ya mtoto ya Tanzania, mtoto anaweza kutambulika tangu akiwa tumboni mwa mama yake (yaani kutambulika kabla hata hajazaliwa).
MALEZI, UANGALIZI, KUMTEMBELEA MTOTO NA MATUNZO
A: NI WATU GANI WANAOWEZA KUOMBA ULEZI (PARENTAGE) WA MTOTO?
Sheria ya mtoto inaeleza kuwa watu wafuatao wanaweza kuiomba Mahakama kutoa amri ya kumthibitisha kupewa malezi ya mtoto -
(a) mtoto mwenyewe;
(b) mzazi wa mtoto;
(c) mlezi wa mtoto;
(d) Afisa Ustawi wa Jamii; au
(e) mtu mwingine yeyote, ikiwa mahakama itatoa amri maalum.
B: JE, NI MUDA GANI MTU ANAWEZA KUFANYA MAOMBI YA ULEZI WA MTOTO?
👉 Kabla ya mtoto kuzaliwa;
👉 Baada ya kifo cha baba au mama wa mtoto;
👉 Kabla mtoto hajatimiza umri wa miaka kumi na nane; au
👉 kwa kibali maalum cha mahakama baada ya mtoto kutimiza miaka kumi na nane.
C: JE, MAHAKAMA INATUMIA VIGEZO VIPI KAMA USHAHIDI KATIKA KUTOA AMRI YA MALEZI YA MTOTO?
Naitwa Lusajo W. Mwakasege, ni Mwanasheria, namba yangu ya simu ni 0713-368153 (inapatikana whatsapp In WhatsApp teilen na telegram) na telegram) na barua pepe yangu ni mwakasege@gmail.com. Tuanze somo letu:
MTOTO NI NANI?
Mtoto ni mtu yeyote mwenye umri chini ya miaka kumi na nane (18).
👉Kwa sheria ya mtoto ya Tanzania, mtoto anaweza kutambulika tangu akiwa tumboni mwa mama yake (yaani kutambulika kabla hata hajazaliwa).
MALEZI, UANGALIZI, KUMTEMBELEA MTOTO NA MATUNZO
A: NI WATU GANI WANAOWEZA KUOMBA ULEZI (PARENTAGE) WA MTOTO?
Sheria ya mtoto inaeleza kuwa watu wafuatao wanaweza kuiomba Mahakama kutoa amri ya kumthibitisha kupewa malezi ya mtoto -
(a) mtoto mwenyewe;
(b) mzazi wa mtoto;
(c) mlezi wa mtoto;
(d) Afisa Ustawi wa Jamii; au
(e) mtu mwingine yeyote, ikiwa mahakama itatoa amri maalum.
B: JE, NI MUDA GANI MTU ANAWEZA KUFANYA MAOMBI YA ULEZI WA MTOTO?
👉 Kabla ya mtoto kuzaliwa;
👉 Baada ya kifo cha baba au mama wa mtoto;
👉 Kabla mtoto hajatimiza umri wa miaka kumi na nane; au
👉 kwa kibali maalum cha mahakama baada ya mtoto kutimiza miaka kumi na nane.
C: JE, MAHAKAMA INATUMIA VIGEZO VIPI KAMA USHAHIDI KATIKA KUTOA AMRI YA MALEZI YA MTOTO?
- Ndoa yoyote iliyofungwa kwa kuzingatia Sheria ya Ndoa;
- Jina la mzazi lililoingizwa kwenye Rejesta ya vizazi na kutunzwa na Msajili Mkuu wa Vizazi;
- Taratibu za kiasili (adoption) zilizofanywa na baba wa mtoto;
- Kutambuliwa na jamii kama mzazi wa mtoto; au
- Majibu ya Vinasaba vya Binadamu (Human DNA).
D: JE, NINI KIFANYIKE IKIWA BABA MZAZI WA MTOTO ANAKATAA UBABA WAKE KWA KUDAI YEYE SIO BABA WA MTOTO?
Mama wa mtoto anaweza kuiomba mahakama itoe amri ya kumlazimisha mtu anayehisiwa kuwa ni baba mzazi wa mtoto kufanyiwa kipimo cha DNA katika maabara ya ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali;
▪️Pia ikiwa ushahidi wa mama haujitoshelezi na haujairidhisha mahakama kuhusu ubaba wa mtu, mahakama yenyewe bila hata ya ombi la mama inaweza kuamua vipimo vya kinasaba (DNA) kifanyike ili kumthibitisha baba wa mtoto.
JE, KATIKA MAZINGIRA HAYO NI NANI ATALIPIA GHARAMA ZA KIPIMO CHA DNA?
Mahakama itaamua yenyewe kuwa nani kati ya mama au baba alipie gharama za kipimo cha DNA.
👉 Kwa sasa, Gharama za kipimo cha DNA ni Tshs. 100,000/= kwa mtu mmoja. Hivyo kwa uchunguzi wa baba, mama na mtoto jumla ya gharama ni Tshs. 300,000/=.
Zingatia:
Maombi ya kipimo cha DNA hayafanywi moja kwa moja na wahusika bali hutakiwa kuombwa na maafisa ustawi wa jamii, mawakili wa kujitegemea, mahakama, jeshi la polisi, madaktari, Wakuu wa Wilaya au taasisi za tafiti zinazotambuliwa kisheria.
E: NINI KITATOKEA IWAPO KIPIMO CHA DNA KITATHIBITISHA UBABA MZAZI?
Ikiwa kipimo cha DNA kitamthibitisha mtu kuwa baba mzazi wa mtoto, Mahakama itatoa amri kwa baba mzazi kuchukua jukumu la kumtunza na kumlea mtoto huyo kama vile mtoto huyo amezaliwa ndani ya ndoa,
Mtoto aliyepata ulezi baada ya baba yake kupimwa DNA na kuthibitishwa juu ya uzazi wake atakuwa na haki zote kutoka kwa baba yake huyo ikiwa ni pamoja na haki ya kurithi mali za baba yake (Lakini hii itategemea imani ya dini ya baba yake).
F: JE, NI KOSA KUKATAA UBABA NA ULEZI WA MTOTO BAADA YA KIPIMO CHA DNA?
NDIYO, Sheria inaeleza kuwa mtu atayekataa amri ya mahakama kwenda kupimwa DNA, au kukataa kumlea mtoto baada ya kipimo cha DNA kufanyika na kumthibitisha kuwa ni baba mzazi wa mtoto, anatenda KOSA LA JINAI.
Mtu huyo atakapotiwa hatiani, adhabu yake ni kulipa FAINI isiyopungua Tshs. 500,000/= au kifungo cha miezi mitatu (3) jela au vyote viwili kwa pamoja, FAINI na KIFUNGO jela.
G: MAOMBI YA ULEZI YANAKUWA DHIDI YA NANI?
▪️ Mtu anayesadikiwa kuwa baba mzazi wa mtoto;
▪️Mwangalizi wa mtoto nk📌
Mama wa mtoto anaweza kuiomba mahakama itoe amri ya kumlazimisha mtu anayehisiwa kuwa ni baba mzazi wa mtoto kufanyiwa kipimo cha DNA katika maabara ya ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali;
▪️Pia ikiwa ushahidi wa mama haujitoshelezi na haujairidhisha mahakama kuhusu ubaba wa mtu, mahakama yenyewe bila hata ya ombi la mama inaweza kuamua vipimo vya kinasaba (DNA) kifanyike ili kumthibitisha baba wa mtoto.
JE, KATIKA MAZINGIRA HAYO NI NANI ATALIPIA GHARAMA ZA KIPIMO CHA DNA?
Mahakama itaamua yenyewe kuwa nani kati ya mama au baba alipie gharama za kipimo cha DNA.
👉 Kwa sasa, Gharama za kipimo cha DNA ni Tshs. 100,000/= kwa mtu mmoja. Hivyo kwa uchunguzi wa baba, mama na mtoto jumla ya gharama ni Tshs. 300,000/=.
Zingatia:
Maombi ya kipimo cha DNA hayafanywi moja kwa moja na wahusika bali hutakiwa kuombwa na maafisa ustawi wa jamii, mawakili wa kujitegemea, mahakama, jeshi la polisi, madaktari, Wakuu wa Wilaya au taasisi za tafiti zinazotambuliwa kisheria.
E: NINI KITATOKEA IWAPO KIPIMO CHA DNA KITATHIBITISHA UBABA MZAZI?
Ikiwa kipimo cha DNA kitamthibitisha mtu kuwa baba mzazi wa mtoto, Mahakama itatoa amri kwa baba mzazi kuchukua jukumu la kumtunza na kumlea mtoto huyo kama vile mtoto huyo amezaliwa ndani ya ndoa,
Mtoto aliyepata ulezi baada ya baba yake kupimwa DNA na kuthibitishwa juu ya uzazi wake atakuwa na haki zote kutoka kwa baba yake huyo ikiwa ni pamoja na haki ya kurithi mali za baba yake (Lakini hii itategemea imani ya dini ya baba yake).
F: JE, NI KOSA KUKATAA UBABA NA ULEZI WA MTOTO BAADA YA KIPIMO CHA DNA?
NDIYO, Sheria inaeleza kuwa mtu atayekataa amri ya mahakama kwenda kupimwa DNA, au kukataa kumlea mtoto baada ya kipimo cha DNA kufanyika na kumthibitisha kuwa ni baba mzazi wa mtoto, anatenda KOSA LA JINAI.
Mtu huyo atakapotiwa hatiani, adhabu yake ni kulipa FAINI isiyopungua Tshs. 500,000/= au kifungo cha miezi mitatu (3) jela au vyote viwili kwa pamoja, FAINI na KIFUNGO jela.
G: MAOMBI YA ULEZI YANAKUWA DHIDI YA NANI?
▪️ Mtu anayesadikiwa kuwa baba mzazi wa mtoto;
▪️Mwangalizi wa mtoto nk📌