Swali la Ugomvi: Kwanini unaikataa CCM?

Swali la Ugomvi: Kwanini unaikataa CCM?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
34,097
Reaction score
43,309
_41113236_tanzania_ap_416.jpg

Swali hili ni kwa wale ambao katika fikra zao na mioyo yao wameamua kuikataa CCM. Wameamua kutokujiunganisha wala kujiambatanisha na chama tawala. Kwa hawa CCM ni kinyume nao. Napenda kujua hasa wale wanaoikataa CCM wanaikataa kwa sababu gani hasa? Maana wengine wanaikataa CCM kwa kadiri ya kwamba wako nje lakini wakiingia ndani au wakionjweshwa vya ndani wanakuwa wa kwanza kuitetea. Inawezekana wanaoikataa CCM hawaikatai kwa sababu moja ya msingi isipokuwa sababu nyingi za binafsi?

Je wewe unaikataa CCM? umewahi kujiuliza ni kwanini?
 
NAIKATAA CCM kwa sababu imeshindwa kabisa kuboresha maisha ya Mtanzania wa chini.
CCM imeleta matabaka kati ya walio nacho na wasio nacho.
Usipo kuwa nacho hutukipata kamwe, wanao watasoma shule za hovgyo kabisa zinazoitwa za kata, zisizo na madawati, vitabu, maabara wala maktaba. Waalimu wa shule hizo ni form six leavers waliopewa mafunzo ya miezi miwili, Yaani mtoto anafundishwa na bora mwalimu, sio mwalimu bora.
Wao watoto wao hawasomi huko, wanasomeshwa nje ya nchi, na kama watasoma hapa nchini, basi ndio watasoma kwenye zile shule zenye kutumia mitala ya nje, na wakimaliza wanakuwa wamepewa nafasi nyeti, kwenye mashirika nyeti.
CCM i meshindwa kupambana na rushwa, inakumbatia rushwa na imekuwa ikiita kwa majina mazuri kama takrima. Wanyonge hatuna haki wala stahili kwenye nchi yetu.
CCM imeshindwa kulinda na kutete rasilimali za TAIFA letu, hebu tazama wanyama pori wetu wanavyopandishwa ndege na kutokomea ughaibuni, hamna anayejali. Hili lichama la ukoo wa KIKWETE silipendi kabisa
 
Swali hili ni kwa wale ambao katika fikra zao na mioyo yao wameamua kuikataa CCM. Wameamua kutokujiunganisha wala kujiambatanisha na chama tawala. Kwa hawa CCM ni kinyume nao. Napenda kujua hasa wale wanaoikataa CCM wanaikataa kwa sababu gani hasa? Maana wengine wanaikataa CCM kwa kadiri ya kwamba wako nje lakini wakiingia ndani au wakionjweshwa vya ndani wanakuwa wa kwanza kuitetea. Inawezekana wanaoikataa CCM hawaikatai kwa sababu moja ya msingi isipokuwa sababu nyingi za binafsi?

Je wewe unaikataa CCM? umewahi kujiuliza ni kwanini?


Viongozi wake wa juu si wasafi (wana kashfa nyingi), hivyo inakuwa ngumu kuwawajibisha watu wa chini yao kwasababu nao wanaogopa maovu yao kuibuliwa. Kutokana na hali hiyo rushwa katika chama hicho na serikali yake imekuwa ni mfumo wa maisha.
 
NAIKATAA CCM kwa sababu imeshindwa kabisa kuboresha maisha ya Mtanzania wa chini.
CCM imeleta matabaka kati ya walio nacho na wasio nacho.
Usipo kuwa nacho hutukipata kamwe, wanao watasoma shule za hovgyo kabisa zinazoitwa za kata, zisizo na madawati, vitabu, maabara wala maktaba. Waalimu wa shule hizo ni form six leavers waliopewa mafunzo ya miezi miwili, Yaani mtoto anafundishwa na bora mwalimu, sio mwalimu bora.
Wao watoto wao hawasomi huko, wanasomeshwa nje ya nchi, na kama watasoma hapa nchini, basi ndio watasoma kwenye zile shule zenye kutumia mitala ya nje, na wakimaliza wanakuwa wamepewa nafasi nyeti, kwenye mashirika nyeti.
CCM i meshindwa kupambana na rushwa, inakumbatia rushwa na imekuwa ikiita kwa majina mazuri kama takrima. Wanyonge hatuna haki wala stahili kwenye nchi yetu.
CCM imeshindwa kulinda na kutete rasilimali za TAIFA letu, hebu tazama wanyama pori wetu wanavyopandishwa ndege na kutokomea ughaibuni, hamna anayejali. Hili lichama la ukoo wa KIKWETE silipendi kabisa

ingeweza kushughulikia mambo hayo yote ungeiunga mkono na kuikubali? Vipi kama ikianza kufanya hivyo sasa?
 
Kubwa la kwanza linalojitokeza akilini mwangu kabla ya kutizama mengine ni Uchafu wa viongozi wake huku wakipokezana kuteteana na kujipongeza kwa machafu.
Kubwa la pili ni utawala Usiomjali kabisa mtawaliwa mpaka nyakati za mtawaliwa kuombwa kura
 
Sababu ni moja tu na ya msingi.
CCM imejenga Mfumo dhalimu wa uendeshaji nchi.
Mfumo kandamizi katika mahakama, katika Bunge na ndani ya serikali yenyewe.
Mfumo ambao rushwa ni utaratibu wa kawaida.
Mfumo ambao asie nacho atajiju, labda angoje neema za AHADI za uchaguzi.
Mfumo uliojikita kwenye MAENDELEO kwa AHADI za uchaguzi badala ya MIPANGO kabambe.
Mfumo uliojikita kwenye kushinda chaguzi, uchaguzi mmoja ukiisha, mchakato wa kushinda uchaguzi unaofuata unaanza mara moja.
Mfumo ulipiga roba demokrasia, katiba inasema jambo moja, na mfumo unasema jingine....na ole wako UFURUKUTE, wanaongeza pressure kwenye kabali.
 
ingeweza kushughulikia mambo hayo yote ungeiunga mkono na kuikubali? Vipi kama ikianza kufanya hivyo sasa?
Too late, hawawezi kufanya lolote sasa, maana hamna miiko ya uongozi haipo tena ndani ya chama.
CCM kimekuwa ni chama cha wenye ulafi wa mali, hamna yeyote ndani ya CCM mwenye nia na dhamira ya kweli ya kuinua na kuyaboresha maisha ya Mtanzania wa chini.
 
Kwangu CCM ni shetani naikataa na mambo yake yote. Waende tu kwani hata Marekani walioendelea akimaliza Obama chama chake hakiwezi kurudi tena madarakani ni zamu ya Republican.

Sasa iweje sisi Taifa maskini ( umaskini wa kusadikishwa ) tuendelee kuongozwa na chama kile kile na watu walewale na wenye mawazo yale yale? hell No.
 
Kwasababu CCM imeshindwa kusimamia UTAWALA WA SHERIA. Vigogo wa CCM wako juu ya sheria, Hivyo imejenga mfumo dhalimu kwa wale tulioko nje ya CCM.
 
naikataa ccm kwa sababu inawaua waandishi na wanaodai maslahi bora ya kikazi.na hasa hasa mwangosi na dr. ulimboka.
 
Sababu ni nyingi sana,lakini inatosha kusema miaka zaidi ya 50 ya utawala wao tumeendelea kuwa maskini na tegemezi na hawana vision yoyote wala dalili za kubadilika kwa dhati.
 
Naikataa CCM kwa sababu
1.Ni waongo na wanaamini sisi watanzania ni Mataahira hatuwezi kung'amua uongo wao
2.Tabia ya kulea wezi wakubwa wa mali za umma na kuonea watumishi wanyonge wanaopinga tabia za wizi serikalini
3.Hawana huruma na hawajali haki za binadamu kwao ni potelea mbali punda afe mzigo ufike yaani bora wapate madaraka na heshima kwa gharama yoyote!
4.Wanawachukia watetezi wa haki ndani ya chama chao wenyewe na kuwapa nafasi watu wasio na utu bali wanafiki machoni pa wanyonge!
5.Wameanzisha na wanahimiza mpasuko wa kidini hadi sasa Watanzania wameanza kubaguana kwa misingi ya dini jambo ambalo ni vigumu tena kuliondoa litaendelea kukua kutokana na wengi kutokuwa na uwezo wa kufikiri kwa kina!
 
Asante sana kwa swali zuri , mimi siyo kwamba naikataa tu hii Ccm bali pia nahangaika sana kuhakikisha kwamba naitokomeza kabisa , Sababu kubwa iliyonisukuma kuyafanya haya ni dhuluma iliyofanywa na hawa maccm kwa watanzania , si rahisi kuzianisha dhuluma zote hapa , maana ukweli ni kwamba tumedhulumiwa kila kitu , ukisoma katiba ya ccm , na wakati huohuo ukaangalia yanayotendwa na wanachama wake ( kumbuka siyo viongozi peke yao ) utashangaa ! kama siku moja tungebahatika kufungua vichwani mwa hawa maccm bila shaka tungeona walivyodhamiria 'kutupiga' shortly ni kwamba hakuna anayeingia ccm leo ili kuja kutekeleza matakwa ya katiba yao , wezi karibu wote , matapeli wote , mafisadi wote , maharamia wote wako ccm ili kulinda mambo yao, usitegemee hata siku moja nchi hii kupiga hatua chini ya ccm , tuungane kuitokomeza kabisa .
 
Ccm wamejenga barabara nyingi,shule nyingi, hospitali nyingi, nk. Lakini vitu vyote hivyo walivijenga kwa fedha zetu tulizowapa kwa nia ya kodi. Hata hivyo, ccm wamebaki na chenchi yetu na wamekataa kurudisha chenchi yetu iliyobaki kwao. Wamekataa kunirudishia wakidai hawana. Chenchi waliichukia kwa njia ya ufisadi uliorasimishwa. Na hakuna mtu ndani ya ccm wa kuzuia hali hiyo kwa sababu uchukuaji wa chenchi yetu uko kimfumo. Hi ni mmoja ya sababu ya mimi kuikataa ccm.
 
naichukia ccm kwa sababu ya rangi yao, wamemaliza mimea kwa laana ya kuvaa mavazi ya uhai ilhali wao ni majanga kwa uhai wa watanzania na rasilimali zao.
 
Mimi naikataa CCM kwa sababu akili yangu, fikra zangu, moyo wangu, roho yangu, mwili wangu na chochote nilicho nacho hakiipendi. Toka uchaguzi wa 1995 kabla sijaanza kupiga kura na 2000 nilipoanza kupiga kura sijawahi kukipenda, kuvutiwa nacho kwa namna yoyote ile na hata kukipigia kura. Kama hakuna mgombea wa chama kingine tofauti na CCM kamwe siwezi kupiga hiyo kura, nitakuwa nimejisaliti mimi mwenyewe. CCM wakae wakijua kuwa nawachukia kutoka rohoni whatever wanaweza kufanya jambo gani la kuweza kunifurahisha, fullstop.
 
Naikataa CCM kwa sababu zifuatazo:
1.Imekumbatia matajiri na kuwasahau kabisa maskini.
2.Rushwa iliyokithiri kwenye idara za serikali i.e hospital,Police,mahakama,halmashauri e.t.c
3.Kushindwa kabisa kuchukua hatua za kuwawajibisha mafisadi.
3.Kuua Viwanda vyetu.
4.Viongozi kujimilikisha mali ya umma mf.Benjamin Mkapa na Mgodi wa kiwira.
5.Uongozi dhaifu wa Nchi uliopo hivi sasa na kushindwa kwake kushughulikia mambo ya msingi....
6.Ufisadi uliokithiri kwenye kila kitu mpaka elimu,CCM imetuletea Mawaziri wanaotumia majina ya watu Mf.Philip Mulugo na hakuna hatua zozote zinazochukuliwa.

Kwa Ujumla kwangu CCM ni zaidi ya Kichefuchefu.
 
mkuu kuinga mkono CCM NI UJINGA. MKUU WE HUONI HAYA MASAIBU TULIYOKUWA NAYO? CHINI YA CCM HATUTOKI HAPA KAMWE
 
Mzee Mwanakijiji
Inaonekana siasa si fani yako unalazimisha; naona ungendeelea na kutunga riwaya; tukupe kisa tu cha kuanzia ungeandika habari kuhusu kiongozi aliyepora mke mtu; na kuikimbia na kutekeleza familia yake kina mama wengi wangeipenda sana hiyo habari.

Chama
Gongo la mboto DSM
cc Ritz
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom