Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 34,097
- 43,309
Jana hata hivyo nimekuwa na wazo la kuifananisha CCM na kitu kingine kabisa. Ninaifananisha na yule mbwa mwitu wa kwenye simulizi za kale aliyejiingiza kwenye nyumba bibi kizee kumtafuna na kujifanya yeye ndiye bibi kizee yule akivaa miwani yake mikubwa (bado nakumbuka picha za kile kitabu! (Little Red Riding Hood). Mtoto yule alishangaa kuona bibi yake yuko tofauti mno na alivyomzoea akabakia kuuliza:
"Bibi mbona macho yako makubwa hivyo"
"Nipate kukuona vizuri mjukuu wangu" alijibu mbwamwitu yule!
Sijui wewe mwenzangu unaifananisha na nini CCM katika mawazo yako. Kwa uzuri au kwa ubaya!