Bit ni kifupisho cha maneno binary digit, hicho ni kipimio cha chini kabisa cha uhifadhi wa data za computer na byte ndio kipimio kinachokubalika km cha mwanzo ktk uhifadhi wa data za computer km, km vile ilivyo kwa vipimo vya uzito wa baadhi ya bidhaa kuwa miligram, gramu, kilogram,tani na kuendelea.
Hivyo basi, ki kawaida data za computer huwa zinahifadhika kwa ukubwa huo wa byte, na mtirirko wake ni kama nilivyo ainisha hapa chini:-
8 bits = 1 byte
1000 bytes = 1 kilobyte (Kb)
1000 kilobyte = 1 megababite (Mb)
1000 megabyte = 1 gigabyte (Gb)
1000 gigabyte = 1 terabyte (Tb)
1000 terabyte = 1 petabyte (Pb)
1000 petabyte = 1 exabyte (Eb)
1000 exabyte = 1 zettabyte (Zb)
1000 zettabyte = 1 yottabyte (Yb)