Swali: Kwanini wanamuziki wengi wanaimba nyimbo za mapenzi zaidi?

MTV MBONGO

JF-Expert Member
Feb 18, 2016
1,262
1,220
Msanii ni kioo cha jamii, nakubali. Lakini, kwanini kioo hiki kinaangaza mapenzi zaidi? Mbona mada za kuimbwa ni nyingi? elimu, ajira, amani n.k kuna nini ktk mapenzi? Tena unakuta misong mingine ya mapenzi matusi kibao.

KULIKONI?
 
Mapenzi yametawala dunia. Yanagusa kila mwanadamu bila kujali umri, jinsia, cheo au hali yake kiuchumi. Yaani Tajiri na masikini, wapiga kura na wapigiwa kura n.k. watakimbizana wee lakini mwisho wa mbio zao watagota kwenye mapenzi. Na mapenzi yana uwanja mpana zaidi ambako waimbaji pote duniani wanapata mashairi bila kikomo. Na kwa vile muziki siku hizi ni biashara tofauti na zamani ndiyo maana unaona watu wengi wanaimba sana kuhusu mapenzi kwa sababu mapenzi yanamgusa kila mmoja na kwa maana hiyo huko kuna biashara inalipa.

Binafsi ukiniuliza napenda nyimbo zipi kati ya nyimbo za mapenzi na zile zinazohusu siasa nitakwambia napenda zaidi za mapenzi. Na hisia za mtu hazivutwi kwa kamba au mnyororo.
 
Nyimbo nyingi za wasanii zinahusu mapenzi na lugha isiyoweza kusikilizwa na wazazi au walezi wetu. Hizi nyimbo za mapenzi zina siri gani? Yapo mengi ya kuimba: elimu, afya n.k

WADAU KARIBUNI TUELIMISHANE!

NAVY KENZO WAKIPAGAWISHA JUKWAANI.jpg
 
Hivi kwa nn nyimbo nyingi za vijana wa bongo flava hazina maadili ya kumjenga
Mtu kimaisha nyingi ni zinazungumzia mapenzi na matusi hii ni ishala tosha maadili hayapo kwa vijana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom