Swali kwa Waziri Bashe: Kilimo gani Kitarudisha Hizi Gharama (Heka 1 milioni 17)?

Per Diem

JF-Expert Member
Mar 28, 2018
2,191
3,711
Nimeona mipango ya waziri bashe, mipango imejaa maneno matamu na porojo nyingi. Bahati mbaya wengi hupenda hizi porojo kuliko uhalisia.

Bashe kwenye mipango yake kufikia 2025 wizara imepanga kuwapatia vijana heka milioni 1. Katika hesabu zake bashe anasema kuhudumia heka 1 itagharimu mil 16.7 ambazo roughly ni kama mil 17.

Maswali ambayo hata yeye anapaswa kujiuliza ni je kilimo gani kinaweza kuleta faida ya kurudisha hiyo pesa kwa heka 1?

Ndio maana wengi walikua wakiubeza ule mradi wa BBT maana uhalisia wake ni mdogo sana, Kama mnatumia gharama kubwa hivi hiyo pesa mtarudisha kwa kilimo cha aina gani? Hili kosa pia umelifanya kwenye BBT, gharama ni kubwa mno, Hawa vijana watalima nini ili kurudisha pesa ya uwekezaji? Si ndio baada ya misimu miwili watu wanakata tamaa kila mtu anaenda na njia yake

Ugumu wa kilimo upo hapo, ndio maana tunasemaga kilimo bongo hakilipi sababu unachowekeza na unachopata ni tofauti. Sasa Mimi ninaomba kujua hiko kilimo ambacho kwa heka 1 Kitarudisha zaidi ya milion 17? Ni kilimo gani hiko?

Si ajabu jana niliona nguvu ikitumika kwa vijana mtandaoni kusifia hii hotuba yako, walikuwa busy na hashtags. Hadi nikajiuliza kwa nini hii nguvu ya kutumia watu influential mitandaoni wasifie hotuba yako. Mawaziri wengi wamewasilisha hotuba zao lakini sijaona wakitumia hii nguvu unayotumia. Naamini raisi atakua anajiuliza maswali haya pia.


20230509_112051.jpg
 
Bashe kwenye mipango yake kufikia 2025 wizara imepanga kuwapatia vijana heka milioni 1. Katika hesabu zake bashe anasema kuhudumia heka 1 itagharimu mil 16.7 ambazo roughly ni kama mil 17.

Maswali ambayo hata yeye anapaswa kujiuliza ni je kilimo gani kinaweza kuleta faida ya kurudisha hiyo pesa kwa heka 1??
Labda amekosea hesabu kama yule RC aliyesema daraja lenye urefu wa sm 300 litajengwa kuanzia Fire hadi Magomeni kuondokana na kadhia ya mafuriko
 
Uwekezaji wa awali Kwa hiyo gharama mbona ni kawaida? Hapo Kuna kufyeka pori,kufunga mifumo ya umwagiliaji,kuandaa zana za kazi,Mbegu nk so shamba Moja complete ndio inagharimu hiyo pesa..

Wewe mtoa mada ndio nikushangae nikajua labda umekuja kutuambia kwamba area A gharama Huwa ni kiasi X ila unalalama bila options ,watu dizaini Yako ni WA kupuuzwa na ukiacha kwamba unatamani mambo ya haribike ila huna way forward..

Mwisho baada ya mavuno kuanza ndio hizo pesa zinaweza rudishwa mdogo mdogo ,maana hata banks zinakoesha kwenye Kilimo Kwa miaka 3 au zaidi sio Kwa mwaka mmja..
 
Mimi huyu Jamaa kanifurahisha sehemu moja tu, hapo kwenye Kilimo cha umwagiliaji trust me huo muarubaini.

Hayo mabwawa yanakuja wakati hali ya hewa imebadilika sana mvua hazieleweki zinakuja na ghafla zinakata kama huo mradi hautopigwa na wezi wa CCM utalikomboa raifa hili.

Nyingine porojo.
 
Uwekezaji wa awali Kwa hiyo gharama mbona ni kawaida? Hapo Kuna kufyeka pori,kufunga mifumo ya umwagiliaji,kuandaa zana za kazi,Mbegu nk so shamba Moja complete ndio inagharimu hiyo pesa...
Ekari moja milioni 17 kuandaa kama ni hivyo watu si wangebanana mjini kuuza chupi kuliko kulima. Ekari inakodishwa 50,000 vijiji vingi nchi hii, ukiongeza milioni moja hapo unasafisha shamba na kulima.

Kufunga irrigation system, madawa, mbolea na mitambo mingine ndio itumike zaidi ya milioni 15?

Kwani kila mtu anapewa power tiller?
 
Hicho Kilimo kimefanywa sana kupitia Makanisa 😂😂😂

Pale kwa Askofu Gamanywa kuna papers za kutosha

Watanzania siyo Wajinga by Magufuli
Hicho Kilimo kimefanywa sana kupitia Makanisa 😂😂😂

Pale kwa Askofu Gamanywa kuna papers za kutosha

Watanzania siyo Wajinga by Magufuli
Hicho Kilimo kimefanywa sana kupitia Makanisa 😂😂😂

Pale kwa Askofu Gamanywa kuna papers za kutosha

Watanzania siyo Wajinga by Magufuli
Toa upuuzi wako hapa,wewe ni failure na legacy zako ndio maana unatapatapa subiria matokeo
 
Back
Top Bottom