Nakubaliana na ww ni hulka ya mtu,unadhani mfumo dume hauhusiki kwenye hili kama alivyosema
Mkoroshokigoli :thinking:
Mfumo dume na wenyewe inawezekana kabisa unachangia hiyo hali.
Na ndo maana mi nadhani vyanzo vyake ni kadhaa, pasipokujalisha jinsia.
Wapo watu ambao kiasili wao ni wagumu sana kukubali makosa yao, hata iweje.
Pia tupo ambao tukiona kama kweli tumekosea basi wala huwa hatusiti kuomba radhi, kwa sababu kufanya hivyo ndo uungwana wenyewe.
Tena huomba radhi bila shurti. Na wala hatupungukiwi na chochote.
Lakini nakubali kuwa mazingira (kama mfumo dume) nayo humjenga mtu kimtazamo. Kama mtu kazaliwa, kakulia, na kulelewa katika mazingira ya mfumo dume usiozingatia usawa kwa watu wote, bila shaka mtu huyo atakuwa na mtazamo kandamizi dhidi ya wanawake.
Mimi sijaoa. Lakini kuna wakati babu yangu aliwahi kuniuliza nani huwa ananipikia nyumbani kwangu. Nikamjibu huwa napika mwenyewe nikipata wasaa.
Ila nilishangaa kidogo kwa nini aliniuliza hivyo. Nikadhani tu kuwa huenda ni utofauti wa kizazi na mazingira aliyokulia yeye. Kwake yeye masuala ya kupika, hususan kama ni nyumbani, ni ya wanawake.
Kwanza sidhani hata anajua kupika maana nyumbani kwake hapajawahi kukosekana watoto wa kike. Wawe wanae yeye au wajukuu zake, wao kupika ndo ilikuwa na inaendelea (kwa wale ambao bado wapo kwake) kuwa wajibu wao.
So in a way you are right. People also are products of their environment(s).