Swali: Humphrey Pole pole unamtumikia nani?

Swali: Humphrey Pole pole unamtumikia nani?

Ccm wanatumia njaa zetu kututawala ,ipingen njaa popote pale mtakapo isikia
 
Hata aletwe malaika kumchafua Lowasa tutamchagua tuuu. Nguvu Kubwa inayotumika na CCM haitashinda.
 
Hivi Kingunge anamtumikia nani? Gwajima analipwa na nani? Haya maswali nyumbu hawapendi kujiuliza
 
Jamaa Polepole anajikoroga sana hata haaminiki sahvi. Inamaana hadi ile hotuba ya JK alipozindua BMK ya kupinga rasimu iliandikwa na Lowassa ? Asitufanye mazuzu huyu kenye katiba ccm ina hatia
 
Watanzania Wa Leo wameshaujua ukweli dhidi ya Richmond na wanajua bayana kuwa nani mhusika, na ndiyo maana Watanzania hawataki kusikia kuhusu upuuzi wa Richmond na ujinga mwingine, alishasema kuwa Mamlaka za juu ndiyo zinahusika.

Tundu Lissu alishasema pia kuwa JK anahusika nayo

Watanzania wa leo ndio sisi na tunajua kuwa Richmond lowasa alipiga dili hata kikwete alisema kwwnye mkutano wa kampeni
Hata dr slaa alisema anao ushahidi wote kuhusu richmond na lowasa
Dr mwakyembe ndio usiseme kabisaa. Ushahidi upo na kesi itafunguliwa wakati wowote.
Mchungaji mtikila alisema ushahidi anao ndio maana alikuwa anajiandaa kumpeleka mahakamani lowasa., bahati mbaya wamemuwahi.!
Sasa kamanda unatuambia nini
 
Hata aletwe malaika kumchafua Lowasa tutamchagua tuuu. Nguvu Kubwa inayotumika na CCM haitashinda.
Nashangaa unajipa moyo na unakufa na yai shingoni. Kila uchao tuhuma zinapotolewa huwa zinaondoka na wanachama wengi sana huwezi amini. Utashangaa. Utapiga kura wewe usishangae hata mkeo labda atampigia Magufuli.
 
Polepole leo ndio umefunguka vizuri jinsi katiba mpya ilivyopondwa na lowasa. Kwanini huwa huzungumzagi haya kwenye mikutano? ? Watu wakaelimishwa? ?? Simamia ukweli na ukweli utakuweka huru.
 
Watanzania wa leo ndio sisi na tunajua kuwa Richmond lowasa alipiga dili hata kikwete alisema kwwnye mkutano wa kampeni
Hata dr slaa alisema anao ushahidi wote kuhusu richmond na lowasa
Dr mwakyembe ndio usiseme kabisaa. Ushahidi upo na kesi itafunguliwa wakati wowote.
Mchungaji mtikila alisema ushahidi anao ndio maana alikuwa anajiandaa kumpeleka mahakamani lowasa., bahati mbaya wamemuwahi.!
Sasa kamanda unatuambia nini

Huwa napenda sana kujadili hoja (issues) na sio kujadili personalities, JK akiwa Kigoma aliwaambia wananchi wamuulize Lissu kuwa anayetembea nae yaani Lowassa ndiye Mhusika wa Richmond.

Kesho yake Lissu akiwa Dom alisema tena wazi kuwa Kikwete ndiye mhusika wa Richmond, sasa wewe unayekuja hapa huna hata vielelezo nakushangaa sana.

Rudi kwa wenye Ccm wakuambie cha kuja kujibu hapa maana naona huna hoja unaleta mihemko tu.
#MabadilikoNiLazima2015
 
Wananchi tuwe macho mchana na usiku tusije chagua mtu yeyote ambaye alihusika kukataa maoni yetu ya Katiba mpya kwani anatudharau na hatutakii mema. Hasa waie wahusika wakuu.
 
Wengine wote wameshaikimbia hii midahalo.Kabaki Butiku na Polepole.
Hicho kigoda kilipaswa kujikita katika mambo ya kitaifa zaidi na sio kujipambanua na CCM.
Mwalimu alikuwa baba wa taifa zima na si wana CCM tu.
 
Wananchi tuwe macho mchana na usiku tusije chagua mtu yeyote ambaye alihusika kukataa maoni yetu ya Katiba mpya kwani anatudharau na hatutakii mema. Hasa waie wahusika wakuu.

kwa hiyo tumkatae samia?
 
Hivi Kingunge anamtumikia nani? Gwajima analipwa na nani? Haya maswali nyumbu hawapendi kujiuliza

Gwajima analipwa na sadaka za waumini wake akiwemo ur dearest dr mihogo..Kingunge alivokua ccm alikua anamtumikia nani au ksa kahama??? Ya ukawa tuachie sisi ww fanya yako!
 
Kigoda kikiendelea kwa mtindo kama was Leo kitaongeza kura kwa wapinzani....
 
Nilijua watazungumzia ni jinsi gani kutokushiriki kupiga kura kwa wanachuo kunaweza kuiondoa amani yetu, cha ajabu wanatutisha na kututia woga, serikali imeshindwa kutushughulikia wanafunzi ili tupige kura kila mwaka yamekua ni makusudi kabisa wakijua kabisa hili pia kunaweza kuiondoa amani yetu....
 
Kuna mambo mengi ambayo tunatakiwa kuhoji kama wananchi, mbali na kujiuliza kuwa Humphrey pole pole yupo kwa masilahi ya nani, lakini pia tujiulize, Gen. Davis Mwamunyange yuko wapi?

na makomeo siku ya pili haonekani kwenye kampeni yupo wapi
 
POLEPOLE UNAMTUMIKIA NANI?

Na Ally Rama.

Nimetoka kuangalia mdahalo kuhusu amani; umoja na haki kupitia star TV pale ubungo blue pearl hotel..

Kwa title ya mdahalo; niliamini watajadili kuhusu haki; umoja na amani lakini wakajielekeza kwenye uchaguzi mkuu bila kugusa vipengele husika..

Miongoni mwa hoja zilizotawala mjadala (si kwa Bahati mbaya) ni mjadala Wa urais kati ya wagombea wawili Magufuli na lowassa..

Polepole kwa nafasi yake; aliendelea kuonesha chuki zake kwa lowassa na alitumia mchakato Wa kupata katiba mpya kuelezea namna Lowassa alivyohujumu mchakato ule hivyo hafai kuwa rais na huo ndio ugomvi wake na lowassa ulipoanza..

Polepole kwa maelezo yake anasema; Lowassa ndie aliharibu mchakato na akaratibu harakati za kupinga kupatikana kwa katiba ya wananchi kwa kigezo cha kuwa mapendekezo Yale yanadhoofisha taasisi ya Urais..

Akaendelea kudai; walienda kumuomba akubali maoni yao lakini akakataa..

Nikaanza kuukumbuka mchakato ulivyokaenda na nikaja na maswali yafuatayo..

1: Lowassa ndani ya CCM hakuwa mwenyekiti wala katibu mkuu..
ndani ya serikali hakuwa hata Waziri..
Sasa nguvu ya kuhodhi mchakato ule bungeni aliitoa wapi?

2: hasimu wake kisiasa Mzee Sitta ndie Alikuwa mwenyekiti Wa bunge maalum la kufinyanga katiba ya wananchi..
Nae aliingizwa king na Lowassa??

3: mama Samia Suluhu Hassan ambaye leo ni mgombea mwenza Wa magufuli; nae aliingizwa king na lowassa afinyange katiba?

4: Mwigulu Nchemba; January na Vijana wengine Makini ndani ya CCM waliipinga rasim ya warioba; nao waliingizwa king na lowassa?

5: inajulikana hata adui mwingine Wa lowassa; paul Makonda alishadadia swala la kifinyanga maoni ya wananchi hasa kwenye kipengele cha muundo Wa muungano..
Akampiga Mzee warioba...
Akazawadiwa ukuu Wa Wilaya ya kinondoni..
Nae aliingizwa king na lowassa??

6: membe nae alipinga muundo Wa muungano..
Nae aliingizwa king na lowassa??

7: Mzee kikwete km rais Wa nchi aliishiwa nguvu ya kuhimili mihemko ya wabunge Wa CCM hadi akaelekea kibra..

Nae aliingizwa king na lowassa??
Aliwazawadia ukuu Wa wilaya Akina Makonda kwa kupinga katiba ya warioba..
Nae aliingizwa king na lowassa??

Eti kweli lowassa pekee ndie alikwamisha mchakato ule?

Kakangu Polepole; hebu kuwa mkweli hapa...

Hao unaowapigia kampeni ndio walokwamisha mchakato Wa katiba mpya..

Polepole Vaa uzalendo; Vaa utanzania..
Zungumza ukweli..

La sivyo tuambie unamtumikia nani??

Ni wazi kuwa Pole Pole hana Moral Authority ya kuwaambia Watanzania kuwa Lowassa aliingilia Mchakato wa Maoni ya Watanzania katika kuipata Katiba Mpya, Mchakato wa kuipata Katiba Mpya kama ni kukwamisha nadhani arudi kwa Mwenyekiti wa Ccm ambaye aliridhika na mambo ya kihuni yaliyopelekea kuvunja utu wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Time ya Katiba Jaji Mstaafu Joseph Sinde Warioba.

Pole pole alikuwa mfuasi wa Katiba ya maoni inayoungwa Mkono na Wananchi ya Serikali tatu na aliipigania sana na ambayo inaungwa Mkono na UKAWA. Ni ajabu sana kuona anaegemeza matusi na hoja dhaifu kwa Mgombea Urais wa UKAWA ambaye anatetea Katiba aliyoipigania.
Tumpuuze kwa kuwa in dhahiri kuwa anatumika na Ccm.

Edited by,
pg.

mjomba mbona unakaukwa na kifua?? kwenye hela usiulize wala kushangaa chochote, polepole analipwa hela nyingi sana kumvuruga Lowassa kwa hoja vyovyote iwavyo azijengee mazingira watanzania waone kama anayoongea ni ya kweli.

hii imekuja baada ya ccm kufanya tathmini wakagundua UKAWA wanamkubali sana polepole tokea kwenye mijadala ya katiba michango yake, ccm wakaona watumie garama yeyote atumike polepole kumchagua lowassa.

Na pia saivi kama umemfuatilia Jaji Warioba naye ameingia katikati kutumika upande wa ccm pamoja na matusi yote waliyokuwa wakimtukana na kumdhalilisha ata kutishiwa kupigwa na ccm lakini leo jaji warioba amekuwa kama pamba kwa ccm wanamtumilia pia. ni fedha tu ndio msingi wa yote haya.

CCM ina watu madhubuti sana katika kutafta namna kuichafua jamii ili yao wao yawaendee lakini hufanikiwa kwa kiduchu sana, haitaathiri sana ushindi wa lowassa kutokana na watanzania wa sasa ni kuwa ni waelewa sana.

Wewe angalia tu wajumbe wa ccm waliotoka Zanzibar kwenye bunge la katiba walipoondoka Zanzibar walikuwa na maslahi mbele ya Zanzibar kwanza lakini walipofika Dodoma fedha ilifanya kazi yakapotea yote waliyoyadhamiria itakuwa polepole?

Usije ukashangaa siku 1 Polepole na Jaji Warioba wakaja wakaunga mkono waziwazi katiba inayopendekezwa na kusema yale ndio maoni hasa ya wananchi.

Tanzania ni nchi 1 mbaya sana, mfano mwengine J.Kikwete ndie aliyekuwa na kiu ya kupata katiba mpya alipoingia madarakani lakini nadhani uliona adhma yake hiyo alivyoikamilisha kila mtanzania amemshangaa sana.

Unafkiri wale wasanii kina Diamond katika nafsi zao ni wapenzi kweli wa ccm? ni fedha tu ndio inatumika wale waendelee kuwa watumwa kwa ccm. Africa kupata watu wasafi 100% jambo hili litachukua hata miaka 1000 zaidi kutoka sasa.

Jaji Warioba na Polepole walikuwa wakisema waziwazi kwenye makongamano mbali mbali kwamba chini ya mfumo wa serikali 2 Tz uchumi hauwezi kunawiri na kuwaletea tija watanzania wa sasa. Lakini utashangaa Jaji warioba na Polepole wanaunga mkono ilani za ccm kuelekea uchaguzi na kusema Magufuli ataleta maendeleo ya ajabu kiuchumi. hapa mkuu ni fedha tu inayofanya kazi wamebadilishwa ni fedha.

Saivi ukiisha uchaguzi watanzania turudi kivyetu tusimtegemee polepole kuja kupinga tena katiba pendekezwa wala usimtegemee tena Jaji Warioba ccm wana trick sana.
 
Back
Top Bottom