mjomba mbona unakaukwa na kifua?? kwenye hela usiulize wala kushangaa chochote, polepole analipwa hela nyingi sana kumvuruga Lowassa kwa hoja vyovyote iwavyo azijengee mazingira watanzania waone kama anayoongea ni ya kweli.
hii imekuja baada ya ccm kufanya tathmini wakagundua UKAWA wanamkubali sana polepole tokea kwenye mijadala ya katiba michango yake, ccm wakaona watumie garama yeyote atumike polepole kumchagua lowassa.
Na pia saivi kama umemfuatilia Jaji Warioba naye ameingia katikati kutumika upande wa ccm pamoja na matusi yote waliyokuwa wakimtukana na kumdhalilisha ata kutishiwa kupigwa na ccm lakini leo jaji warioba amekuwa kama pamba kwa ccm wanamtumilia pia. ni fedha tu ndio msingi wa yote haya.
CCM ina watu madhubuti sana katika kutafta namna kuichafua jamii ili yao wao yawaendee lakini hufanikiwa kwa kiduchu sana, haitaathiri sana ushindi wa lowassa kutokana na watanzania wa sasa ni kuwa ni waelewa sana.
Wewe angalia tu wajumbe wa ccm waliotoka Zanzibar kwenye bunge la katiba walipoondoka Zanzibar walikuwa na maslahi mbele ya Zanzibar kwanza lakini walipofika Dodoma fedha ilifanya kazi yakapotea yote waliyoyadhamiria itakuwa polepole?
Usije ukashangaa siku 1 Polepole na Jaji Warioba wakaja wakaunga mkono waziwazi katiba inayopendekezwa na kusema yale ndio maoni hasa ya wananchi.
Tanzania ni nchi 1 mbaya sana, mfano mwengine J.Kikwete ndie aliyekuwa na kiu ya kupata katiba mpya alipoingia madarakani lakini nadhani uliona adhma yake hiyo alivyoikamilisha kila mtanzania amemshangaa sana.
Unafkiri wale wasanii kina Diamond katika nafsi zao ni wapenzi kweli wa ccm? ni fedha tu ndio inatumika wale waendelee kuwa watumwa kwa ccm. Africa kupata watu wasafi 100% jambo hili litachukua hata miaka 1000 zaidi kutoka sasa.
Jaji Warioba na Polepole walikuwa wakisema waziwazi kwenye makongamano mbali mbali kwamba chini ya mfumo wa serikali 2 Tz uchumi hauwezi kunawiri na kuwaletea tija watanzania wa sasa. Lakini utashangaa Jaji warioba na Polepole wanaunga mkono ilani za ccm kuelekea uchaguzi na kusema Magufuli ataleta maendeleo ya ajabu kiuchumi. hapa mkuu ni fedha tu inayofanya kazi wamebadilishwa ni fedha.
Saivi ukiisha uchaguzi watanzania turudi kivyetu tusimtegemee polepole kuja kupinga tena katiba pendekezwa wala usimtegemee tena Jaji Warioba ccm wana trick sana.