Swali Gumu: Kwanini kila ninayemsaidia huwa hana shukrani?

Kichuguu

Platinum Member
Oct 11, 2006
15,570
19,447
Zamani sana bendi moja hapo Dar: ama Dar es salaama Jazz au Western Jazz iliimba kuwa "Tenda Wema, nenda zako, usingoje shukurani". Maudhui ya wimbo huu yamesharudiwa na waimbaji wengi sana siku za hivi karibuni.

Mimi ni mtu wa makamo sana wakati huu na katika maisha yangu nimeshasaidia watu wengi sana, jambo ninalojivunia mno. Kila msaada ninaotoa huwa ina maana ya mimi na familia yangu kujinyima ili tuwasaide wengine, siyo kwamba huwa nina dimbwi kubwa la pesa za kuchota bure bure bure.

Sasa kinachonishangaza ni kuwa ndugu na marafiki wengi niliowahi kusaidia huwa hawaonyeshi shukrani yoyote ukilinganisha na wale ambao huwa sina uhusiano nao. Ndugu na marafiki huwa wanataka zaidi wala hawawezi kutosheka na msaada, na ikitokea nikasema sasa msaada niliokwishatoa unatosha inabidi ajiendeleze mwenyewe, basi wananilaumu kama vile kile nilichokwishawafanyia siyo kitu kabisa. Yaani wanakuwa wananiongea vibaya tu bila shukrani yoyote.

Ni wapi ninapokosea katika kusaidia ndugu na marafiki ili watambue msaada wangu kwao?

Kuna mmoja nilimlipia mtoto wake kwa miaka minne mfulizo chuo kikuu cha dar es salaama wala hakuchukua mkopo wa serikali, akamaliza na 3rd class.

Sasa mtu huyo ananilaumu kwa nini simsaidii mtoto huyo kusoma masters! Kibaya anatumia lugha mbaya kuwa nina wivu sipendi watoto wake waendelee kama mimi wakati bado ninasaidia mtoto wake mwingine ambaye yuko sekondari ninayomlipia mimi!!
 
Binadam hawana Shukran kabisa bora uishi Maisha yako tu ukitaka kusaidia Kasaidie Watoto yatima mashuleni au kwenye vituo, ishanitokea iyo na tena nabadilika Kuwa adui kabisa tofaut na wema nilioutenda kwao, mpaka inafika wakati naisi labda mimi ndo mwenye makosa, ata kama nikijishusha wao wako dont care, aisee Tuishi tu maisha Yetu basi, kujipa Umuhimu kwenye maisha ya watu sometims ni kujiumiza
 
Ukiwa unatenda wema na kutarajia urudishiwe chochote huo hukuwa unatenda wema bali unafanya biashara

Mm kuna jamaa yangu alikuwa anaumwa inatakiwa afanyiwe operations mbili moja ya kongosho na nyingine ya tezi dume na alikuwa na sh 60000 but gharama za pale kcmc hospital ni 2.3ml

Nkaampa bima yangu akafanyiwa operations zote hizo kwa bima yangu,nilijitoa tu kama rafiki wala sikuwa natarajia chochote kutoka kwake

Alivyopona akanitoa na konyagi ndogo ya 3500,
Ila mpaka Leo akiniona ananikimbia cjui ni kwa nn?
 
Ukiona chuki inakuja jua wema ulitangulia, binadamu hana shukrani. Mimi ntasaidia yatima tu kwenye masuala ya ada, sijui mtoto wa mjomba sijui wa kaka mkubwa achana nayo kama hupendi kulaumiwa.
Ukitenda wema usitegemee akurudishie.
 
ndugu ukimpa msaada anaona ni haki yake na pia ni wajibu wako, utafanya kila unaloweza lakini mwisho wa siku hawatoona umefanya kitu extra maana wanachoangalia ni uwezo ulionao na si unajitoa kwa kiasi gani "kiufupi hawajui wala hawajali hilo "..

kwa hiyo jipime tu huruma isizidi uwezo, toa tu pale unapoweza lakini ndio uwe na ngozi ngumu. Maana unaonekana unapenda sana kupendwa na kukubalika, lakini Omba sana Mungu ajaalie usije tetereka kiuchumi maana hakuna rangi utaacha kuiona toka kwao
 
ndugu ukimpa msaada anaona ni haki yake na pia ni wajibu wako, utafanya kila unaloweza lakini mwisho wa siku hawatoona umefanya kitu extra maana wanachoangalia ni uwezo ulionao na si unajitoa kwa kiasi gani "kiufupi hawajui wala hawajali hilo "..

kwa hiyo jipime tu huruma isizidi uwezo, toa tu pale unapoweza lakini ndio uwe na ngozi ngumu. Maana unaonekana unapenda sana kupendwa na kukubalika, lakini Omba sana Mungu ajaalie usije tetereka kiuchumi maana hakuna rangi utaacha kuiona toka kwao
Siyo kuwa ninataka kukubalika, ila sipendi kuchafuliwa jina kwenye jamii yetu. Ni afadhali wawe wananyamaza tu kuliko kunijengea jeshi la uadui dhidi yangu huko nyumbani ambapo ni kwetu sote!
 
Pole mwalimu.

Ila wasaidiaji wengine matata sana, nilippjiunga chuo Dar likizo ndogo nikawa naenda kwa ndugu yangu hapo mjini. Nilipofika mwaka wa 3 nikasikia maneno natembea na mumewe. Nikamkatia.

Nikamaliza chuo, nikaanza kazi, nikachumbiwa na sikumualika harusini. Akalalama tena nimemnyima mwaliko wakati yy ndio alinipokea na kunionyesha mji!

Walimwengu wana mambo!
 
Pole mwalimu.

Ila wasaidiaji wengine matata sana, nilippjiunga chuo Dar likizo ndogo nikawa naenda kwa ndugu yangu hapo mjini. Nilipofika mwaka wa 3 nikasikia maneno natembea na mumewe. Nikamkatia.

Nikamaliza chuo, nikaanza kazi, nikachumbiwa na sikumualika harusini. Akalalama tena nimemnyima mwaliko wakati yy ndio akinipokea na kunionyesha mji!

Walimwengu wana mambo!

Utakua mrembo Sana basi..
 
Pole mwalimu.

Ila wasaidiaji wengine matata sana, nilippjiunga chuo Dar likizo ndogo nikawa naenda kwa ndugu yangu hapo mjini. Nilipofika mwaka wa 3 nikasikia maneno natembea na mumewe. Nikamkatia.

Nikamaliza chuo, nikaanza kazi, nikachumbiwa na sikumualika harusini. Akalalama tena nimemnyima mwaliko wakati yy ndio akinipokea na kunionyesha mji!

Walimwengu wana mambo!
Pole sana, ila kesi yako ni tofauti kidogo na mazingira ninayoongelea hapa.
 
Back
Top Bottom