Suppression of Dissent; Mbowe ni Shujaa

Suppression of Dissent; Mbowe ni Shujaa

Yani nimetokea kuwchukia sana huyu mbowe na mamvi ambao wamekuja kuharibu system nzima ya nchi na sasa wanataka kutufanyia biashara hadi kwenye siasa zetu nawapinga vikali na ntazidi kuhamasisha watu wazidi kuwapiga hawa wanaotaka kulitafuna taifa letu. Nchi hii imejnengwa kwenye misingi ya amani toka mwaka 1961 tulipopata uhuru sasa hawa wanataka kuiharibu
KEMEA UKAWA
CHAGUA AMANI YA CCM
CHAGUA MAGUFULI TUENDELEZE AMANI YETU
 
mbowe kweli ni mafia nime mkubali, kila ambaye yeye ana muona kuwa ana falsafa ya kweli kuwatumikia watanzania anapambana nae, mungu kweli hamfichi mnafiki, sasa ameamua kumleta fisadi papa na kuiaminisha jamii atafanya mambo mazuri kwa watanzania, sasa safari hii tuta pambana nae sisi wananchi tunao penda maendeleo yakweli itakua zamu yake yeye na mwizi wake

tena ni mafia wa kisomali kabisa
 
kweli mbowe ni shujaa... amehakikisha mpaka viongozi wenzake amewapiga chini, ni shujaa tena wakupinga maendeleo ya watanzania
 
Kama hamtataka mabadiliko kupitia CCM, mtapata maendeleo ya ufisadi ndani ya CHADEMA, sababu CHADEMA ya sasa imekuwa ni kichaka cha kujifichia watu waovu, waongo na wanafiki.
Tuhesabu tuone ukawa na ccm wapi kuna mafisadi papa wengi.......List ya escrow tu inawamaliza ......pumbav kabisa
 
Hahaha nacheka lakini inasikitisha sana inawezekana vip katika picha hiyo yote hapo juu yeye amebaki peke yake inamaaana yeye ndio msafi kuliko wengine? ama ndio anatumia nguvu ya madaraka kunyanyasa wengine?
Kwa akili ya haraka tu ukiangalia hiyo picha unatambua kabisa hapo zimetumika nguvu za madaraka ambazo zimefanywa na mtu mmoja ambae ni mbowe ,maana haiwezekani wote kwake wakawa wabaya yeye tu ndio mzuri huyu ni Gaidi anaeaplly unyanyasaji kwenye ubinadamu wa viongozi wake na tumeshtuka na tumetambua iliyokweli sasa sisi ni wafuasi wa CCM na MAGUFULI ndio kura yetu

Kabaki mwenyewe coz anayo hela ya kutosha so sio mchumia tumbo...a.k.a hanunuliki.....hao wengine njaaaaa kali...
 
Huu ni udhalirishaji kwangu mie niliyeiamini CDM ya 2005-2014 ..yaani huwezi kujiuliza credibility ya chama na viongozi walioko CDM leo? yaani kwasababu tu chama ni cha mkwe wake ndo anapata kuwaona wenye mtizamo tofauti na yeye kwamba watafukuzwa chama? kwasababu tu yeye anaelewa hawezi kufukuzwa hata avurunde vipi basi anatumia mwanya huohuo kuwaita wenzie eti wanataka kuwa juu ya chama, kwamba yeye ni msafi na hana doa ndani ya chama? kwamba atakayetofautiana naye basi kawa juu ya chama, hii ndo demokrasia? ..na watafukuzwa wengi kwasababu chama kina wenyewe, na ukidai mwongozo unaitwa msaliti ..ni bora hata CCM japokuwa wanafumbafumba lakini demokrasia yao walau inapimwa, tumeona watu 42 walipewa nafasi ya kuchukua fomu na walau tuliona Sera zao ndani ya chama kitu amabcho CDM ni ndoto, wanasubiri mfalme ateue.
slaa amejifukuzisha mwenyewe!
 
Do you believe in tyranny and high churn?

Kama Mbowe angekuwa meneja wa sehemu ambayo key people wanaondoka hivyo, ingebidi aulizwe sana kuhusu management yake.

Inawezekana yeye ndiye mwenye tatizo.

Tatizo lake moja

Hana Price Tag
 
Kuna tatizo gani endapo watu wanaondoka meneja anabaki lakini taasisi inakua kwa kasi ya ajabu? Wenye matatizo ni hao wanaoondoka na si meneja vinginevyo taasisi ingeshaanguka zamani.

Kukua kwa ajabu kunaweza kuwa tatizo kama hakufuati principle.

Hata Ponzi scheme kama ya Bernie Madoff ilikua kwa ajabu, lakini si kwa principle. Matokeo yake yuko jela.

Hili ndilo tatizo. CHADEMA ina uchu wa kukua na kuchukua urais mpaka imetupa principle na kumkubali mtu iliyotuambia miaka yote hiyo kwamba ni fisadi.

Guess what, if you are not principled, growth is nothing.

Huu ndio ukweli mchungu ambao watu wenye cognitive dissonance ndani ya CHADEMA wanapata wakati mgumu kuukubali.

Baada ya uchaguzi huu kupita, Lowassa akishindwa, CHADEMA kama chama kinaweza kubakia a shell of it's former self.
 
Do you believe in tyranny and high churn?

Kama Mbowe angekuwa meneja wa sehemu ambayo key people wanaondoka hivyo, ingebidi aulizwe sana kuhusu management yake.

Inawezekana yeye ndiye mwenye tatizo.


Mbowe hafanyi siasa
Mbowe anafanya 'harakati'...
no one knows exactly hizo harakati zina lengo gani hasa..
kama lengo ni yeye kuwa more powerful so far hajafeli....
 
Hotuba ya mh. Slaa imenisaidia sana kuwajua wanasiasa kwa undani zaidi! Kubwa zaidi hata tukiamini maneno yao, lakini siyo wakutegemea! Hawa watakuacha njiani, lakini kuna ukweli uliofchika, ambao labda hata yeye Slaa hajauona.

Mbowe ni genius! Slaa amenisaidia kumwona Mbowe katika ubora wake, siyo ukabila lakini kuna wakati Wachaga wapewe sifa wanazo stahili. Mbowe anafahamu hesabu na anachanga karata zake na kuzicheza vizuri sana!

Sijui kwa wengine lakini, kusema kweli mimi naona urafiki wa Mbowe na EL siyo wa kudumu. Baada ya October 25, litajengwa 'tofali' jipya katika ujenzi wa democrasia ya vyama vingi Tanzania bila kujali itashinda UKAWA au CCM! Muungano wa UKAWA na EL, una nia moja tu kupunguza absolute power ya CCM na kama siyo CCM kufa basi iwekwe kwenye viwango sawa na vyama vingine.

Anyway u-genius wa Mbowe upo wapi? Ni kwenye 'usajili!' EL, 2015 kama Slaa mwaka 2010, ni 'mchezaji' mkali ambaye unaweza kumtumia sasa kubeba ubingwa wakati ukiendelea kukuza vipaji! Kuna fursa Mbowe ameiona, ambayo hata Slaa hakujua 2010 kwamba alikua 'usajili' wa msimu ule! Mbowe ni 'mtaalamu' hata ukimwita jina gani, au useme ameuza chama, kwa kazi ya mwenyekiti wa chama ni nini?! Uza chama, I mean, uza chama!! Wakati kuna watu vyama vinawadodea na kuwafia mikononi, Mbowe anauza chama.............chema chajiuza!

Hongera Mbowe, wacha EL akusogeze, kama siyo kukamata nchi mwaka huu, lakini mwendo huu, lazima utakua karibu! Mbowe amecheza, ni bonge la kocha, na Lazima tumpe pongezi zake!
Zaidi ya mahaba yako kwa Mbowe of which u have right to feel that way, bado sijaona u - genius wa mbowe. Maamuzi ya kuwaondoa wapinzani wake ndani ya CDm ni ya kawaida sana.
 
Mbowe hafanyi siasa
Mbowe anafanya 'harakati'...
no one knows exactly hizo harakati zina lengo gani hasa..
kama lengo ni yeye kuwa more powerful so far hajafeli....

Beyond reasonable doubt..,MBOWE ni mwanaharakati..

Na sasa hakuna chembe ya shaka kwa sasa kujua lengo la harakati za mbowe...,lengo ni moja tu, kuwahakikishia familia yake maisha bora na ya uhakika.

Ameshatengeneza fedha ya kutosha ambayo akistaafu siasa mwezi wa kumi na moja anaenda kuhamia South Africa akitengeneza maisha yake..
 
Hii ni mara yangu ya tatu kupiga kura:
1. Uchaguzi 2005 Matokeo - Serikali za Mitaa, Diwani, Ubunge na Urais (Kura zangu zote zilipotea)
2. Uchaguzi 2010 Matokeo - Kura ya Urais ilipotea (Serikali za Mitaa, Diwani, Ubunge kura zangu zilianza fanyakazi)
3. Uchaguzi 2015 Matokeo - Serikali za Mitaa nimeshawachinja nasubiri Oct. 25, Safari hii sipotezi kura mpaka ya Urais.

USIPOTEZE KURA YAKO, VOTE FOR UKAWA
 
Unaweza kuitambua sauti ya Ibilisi katika uchaguzi wa Tanzania wa 2015?

Nani anaweza kuwa juu ya mwenye chama! Unaanzaje kumpinga mwenye chama?

Chacha Wangwe alijaribu kumpinga mwenye Chama akashindwa, Walid Aman Kabourou alijaribu kumpinga mwenye chama akashindwa, Brown Ngwilulupi alijaribu kumpinga mwenye chama akashinwa, Mahimbo Kaoneka alijaribu kumpinga mwenye chama akashindwa, Zitto Zuberi Kabwe na Kitila Mkumbo walijaribu kumpinga mwenye chama wakashindwa, Sasa amekuja Dr. Wilibrod Slaa anajaribu kumpinga mwenye chama. Pengine atashindwa kama wenzake waliojaribu kumpinga mwenye chama huko nyuma.

Kwenye hiki chama kila mwenye mawazo tofauti hutafsiri ama anatumika na CCM, ama anataka kuwa JUU YA CHAMA. Kumbe tatizo ni kwamba ukiwa na mawazo yanayotofautiana na mwenye chama, huko ndo kujaribu kuwa Juu ya Chama. Funzo hapa ni kwamba ILI KUWA CHINI YA CHAMA, NA SIYO JUU YA CHAMA, ni lazima ukubaliane na mwenye chama.

Kujua mantiki ya hoja hii watafute hawa waliojaribu kutofautiana na mwenye chama wakaja kujifunza kwa kuchelewa sana kwamba kupinga mawazo ya mwenye chama ni kuwa juu ya chama. Hawa watakuhakikishia kuwa kumbe hiki chama ni MTU; ni mtu ambaye atakaa tu na wale wanaokubali kuwa chini ya Chama kifikra na kimatendo. Yaani atakaa tu na wale wanaokubali fikara za kwake tu.

Orodha ya watu waliojifunza somo hili kwa kuchelewa sana ni ndefu; ila hii hapa ni orodha ndogo nakutangulizia uwatafute kupata undani: Walid Aman Kabourou, Brown Ngwilulupi, Mahimbo Kaoneka, Chacha Wangwe, Zitto Zuberi Kabwe, Kitila Mkumbo, na orodha ni ndefu. Sasa kaja na huyu mpya Dr. Slaa.

Hivi hili tatizo la kuwa juu ya chama manaake nini? Mbona mi naona kama vile ni tatizo la kuwa juu ya mtu?

Kuna sauti mbili katika uchaguzi wa mwaka 2015 Tanzania. Kuna Sauti ya Ibilisi na sauti ya Roho Mtakatifu. Na mara kwa mara sauti ya Ibilisi huwa kubwa zaidi kuliko sauti ya Roho Mtakatifu. Sililiza vizuri sauti hizi kuhusu watu kuwa juu ya chama utaitambua haraka sana sauti ya ibilisi inatoka wapi.

Tunaye ibilisi na roho mtakatifu miongoni mwetu kwenye uchaguzi huu wa Tanzania wa 2015. Mimi nimeshamtambua ni nani huyu mwenye sauti kuu, mwakilishi wa Ibilisi; na ni nani huyu mwenye sauti iliyofifia sana, huyu ambaye kaleta mbele yako sauti ya roho mtakatifu.... Mkatae Ibilisi na hila zake; hata pale anapokuja na Biblia mkononi mwake.

Hebu isome hii picha uniambie wewe unaionaje. Je hii ni sauti ya Roho Mtakatifu?

MWENYE CHAMA KAONGEA.jpg
 
na utawakuta ndio wenye hoja za msingi chamani kwa maana hiyo hawawezi kukaa na wasanii kwenye chama ni sawa na taili la trela halijui linapokwenda
 
Hii ni mara yangu ya tatu kupiga kura:
1. Uchaguzi 2005 Matokeo - Serikali za Mitaa, Diwani, Ubunge na Urais (Kura zangu zote zilipotea)
2. Uchaguzi 2010 Matokeo - Kura ya Urais ilipotea (Serikali za Mitaa, Diwani, Ubunge kura zangu zilianza fanyakazi)
3. Uchaguzi 2015 Matokeo - Serikali za Mitaa nimeshawachinja nasubiri Oct. 25, Safari hii sipotezi kura mpaka ya Urais.

USIPOTEZE KURA YAKO, VOTE FOR UKAWA
Tathmini yako mwenyewe so far it's still ----
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom