Na wewe dereva una matatizo kwa nini unajifanya fundi? Kwa nini hutaki kusikiliza au kuamini mafundi kusikiliza ushauri wao? Yaani badala ya wewe kushauriwa wewe ndo unawashauri mafundi, alafu unawaelekeza cha kufanya, na wao kwasababu wanaangalia matumbo yao wanatekeleza unachotaka. Umekuwa mkali fundi akifanya anachofikiri kitafaa, umefukuza mafundi wanaokushauri usichokitaka. Chagua fundi mmoja akushauri vizuri matatizo ya Gari yako. Acha kukurupuka na kuwaachia mafundi wanafunzi kujifunzia katika Gari yako.
Alafu kwanini ulikuwa unatudanganya wateja wako kuwa Gari yako haina matatizo kwamba ni nzima na inaleta hesabu vizuri, hivi unajua kuwa mficha ugonjwa kifo humuumbua?