Sunak Waziri Mkuu wa 79 wa Uingereza

Comred Mbwana Allyamtu

JF-Expert Member
Jun 28, 2016
348
847
Kijana mwenye asili ya India Rish Sunak hatimae amefanikiwa kuwa kiongozi wa Chama cha Conservative (Torry party) nafasi itakayo mfanya kuwa Waziri Mkuu wa Uingereza baada ya kuidhinishwa na kuteuliwa na mfalme Charles lll.

Sunak mwenye Miaka 42 ambaye ni mbunge wa Richmond (York) ni Waziri mkuu wa kwanza wa Uingereza asie na asili ya Uingereza ya moja kwa moja, wazazi wake waliwahi kuishi Kenya na Tanzania kabla ya kuhamia Uingereza.

Sunak alifunga ndoa mwaka 2009 na mwanadada Akshata Murty ambae ni Mwanamama tajiri ambae amerithi utajiri kutoka kwa wazazi wake, kwasababu hiyo imemfanya Rushi Sunak kuwa mbunge tajiri zaidi Uingereza.

Utajiri huo unatokana na mkewe ambae ni mtoto wa billionaire N. R. Narayana Murthy, Sunak and Murty ni matajiri wa 222 katika nchi ya Uingereza, utajiri wao wa jumla ni paund milioni £730.

Sunak alizaliwa huko Southampton, huku wazazi wake wakitokea Punjabi India na kuhamia Uingereza wakitokea Afrika mashariki miaka ya 1960s.

Sunak alisoma Oxford na Stanford ambavyo ni vyuo vikuu bora duniani, ni Mara ya Kwanza Uingereza inapata Waziri mkuu asiye Mkristu.

Tarehe 23 Oktoba Sunak alitangaza nia yake ya kugombea Uongozi wa chama, mapema leo baada ya Boris Johnson kujiondoa kwenye kinyang'anyiro baada ya kupata waugwaji mkono wachache na Mordaunt kujiondoa, Sunak alitangazwa kuwa Kiongozi mpya wa Chama cha Conservative nafasi inayomfanya kuwa Waziri Mkuu wa Uingereza.

Anatarajiwa kuwa waziri mkuu wa kwanza wa Uingereza mwenye asili ya Asia, na anakuwa Waziri mkuu wa 79 wa Uingereza.

Ndimi Comred Mbwana Allyamtu CMCA
 
Huu ujinga wa mbuzi wakiwa famous mnaanza kuleta habari za waliwahi kuishi Tanzania sijui mala Zanzibar uwa unan kwaza una tija gan kwa taifa letu
Huu ujinga unazidi kuota mizizi,na Inadhihilisha Tabia ya uchawa na kujipendekeza hambayo inazidi kuenea kama moto wa nyika katika siasa na jamii kwa ujumla,

Sent from my Infinix X660B using JamiiForums mobile app
 
Wenzetu demokrasia imefikia patamu kuelekea uchungu.

Hii mbegu waliyopanga leo muda si mrefu ufalme utaanguka, na UK itakuwa jamhuri.

Wenyeji wazungu wajiandae kisaikolojia

Next year nahamia Iran nikagombee uraisi na ukorintho wangu!
 
Huu ujinga wa mbuzi wakiwa famous mnaanza kuleta habari za waliwahi kuishi Tanzania sijui mala Zanzibar uwa unan kwaza una tija gan kwa taifa letu
Asa si ndo vizuri mkuu! au!........inaonyesha tumelea kitu kizuri sana tunafaaa kwa malezi, hasa kwa awamu ya kwanza! ya julius!...Kenya walitoa Obama sisi tmetoa huyu safii EAC yetu hoyeee! bado Uganda, zaire rwanda burundis/sudani

siku akija hapa tutaongea nae kiswahili, hata wazamiaji wakienda huko wanabonga tu kiswahili mambo swafi! yani mkuu baba downing st ukienda wee ni shikamoo waziri!
 
Kijana mwenye asili ya India Rish Sunak hatimae amefanikiwa kuwa kiongozi wa Chama cha Conservative (Torry party) nafasi itakayo mfanya kuwa Waziri Mkuu wa Uingereza baada ya kuidhinishwa na kuteuliwa na mfalme Charles lll.

Sunak mwenye Miaka 42 ambaye ni mbunge wa Richmond (York) ni Waziri mkuu wa kwanza wa Uingereza asie na asili ya Uingereza ya moja kwa moja, wazazi wake waliwahi kuishi Kenya na Tanzania kabla ya kuhamia Uingereza.

Sunak alifunga ndoa mwaka 2009 na mwanadada Akshata Murty ambae ni Mwanamama tajiri ambae amerithi utajiri kutoka kwa wazazi wake, kwasababu hiyo imemfanya Rushi Sunak kuwa mbunge tajiri zaidi Uingereza.

Utajiri huo unatokana na mkewe ambae ni mtoto wa billionaire N. R. Narayana Murthy, Sunak and Murty ni matajiri wa 222 katika nchi ya Uingereza, utajiri wao wa jumla ni paund milioni £730.

Sunak alizaliwa huko Southampton, huku wazazi wake wakitokea Punjabi India na kuhamia Uingereza wakitokea Afrika mashariki miaka ya 1960s.

Sunak alisoma Oxford na Stanford ambavyo ni vyuo vikuu bora duniani, ni Mara ya Kwanza Uingereza inapata Waziri mkuu asiye Mkristu.

Tarehe 23 Oktoba Sunak alitangaza nia yake ya kugombea Uongozi wa chama, mapema leo baada ya Boris Johnson kujiondoa kwenye kinyang'anyiro baada ya kupata waugwaji mkono wachache na Mordaunt kujiondoa, Sunak alitangazwa kuwa Kiongozi mpya wa Chama cha Conservative nafasi inayomfanya kuwa Waziri Mkuu wa Uingereza.

Anatarajiwa kuwa waziri mkuu wa kwanza wa Uingereza mwenye asili ya Asia, na anakuwa Waziri mkuu wa 79 wa Uingereza.

Ndimi Comred Mbwana Allyamtu CMCA
1666708596203.png


Simple

Sisi hapo tungeandaa majukwaa na mabango makubwamakubwa na vitisho juu
 
Sunak mwenye Miaka 42 ambaye ni mbunge wa Richmond (York) ni Waziri mkuu wa kwanza wa Uingereza asie na asili ya Uingereza ya moja kwa moja, wazazi wake waliwahi kuishi Kenya na Tanzania kabla ya kuhamia Uingereza.

Sunak alifunga ndoa mwaka 2009 na mwanadada Akshata Murty ambae ni Mwanamama tajiri ambae amerithi utajiri kutoka kwa wazazi wake, kwasababu hiyo imemfanya Rushi Sunak kuwa mbunge tajiri zaidi Uingereza.
Leo India hawalali stesheni zote za redio na televisheni zinasimulia Sunak, bado chawa wa kule walikopitia wazazi wake Africa Mashariki 🤣
 


New British PM Rishi Sunak twice as rich as the King | 9 News Australia​

 
Huu ujinga unazidi kuota mizizi,na Inadhihilisha Tabia ya uchawa na kujipendekeza hambayo inazidi kuenea kama moto wa nyika katika siasa na jamii kwa ujumla,
Nimekupenda sana Mkuu umegonga msumari wa moto, akili za kitz Mungu azihurumie tu, subiri siku Rishi akisema Tz ifuate haki za binadamu utawasikia haohao wanaosema ni mTZ watamponda
 
Back
Top Bottom