Sumu ya kuua kunguru ni ipi?

Sumu ya kuua kunguru ni ipi?

Sio aina hii. Hao wastaarabu na hawana noma kwanza hawapo Dar.

Ni wale weusi mwili mzima. Wale ni wakorofi na hawana faida mazingira yetu haya. Ni wakorofi hata wakitokomezwa hakuna wa kuwamiss.
Hao Wapuuzi watakuwa ni wahamiaji wazawa wa huku ni waoga hence msemo kuwa muoga kama Kunguru upate kuishi maisha marefu
 
View attachment 2418563
Ni hao hapo juu au wa kwako wapo vipi ?...,

Mimi huku wapo wachache na wanafanya kazi yao katika ecosystem ipasavyo kwa kula mizoga ya hapa na pale..., wala hawana shida..

Unajua sometimes nawaza labda binadamu ndio virusi..., kuna mdau alikuja eti tumbili wanamsumbua kwenye shamba lake na nyumba yake, nilivyofanya research kumbe yeye ndio kawavamia kwenye makazi yao...

Nadhani hawa viumbe wengine kama wangeweza kukaa na kujadari mustakabali wa maisha yao wangetuona sisi binadamu kama virusi tu (yaani mchanyato wa Corona na Ukimwi)
Mkuu kunguŕu wa zanzibar ni kama hao lakini tofauti yake hilo baka jeupe wao ni jeusi.
 
Kunguru wa Dar
Wajanja Sana
Wanaweza fanya tukio ukadhani hii mbona akili kubwa kufanywa na ndege uyu
Kuna siku waliiba nyama jikoni tulizubaa kidogo tukakuta nyama hamna
 
Nipe tenda niwaangamize ndani ya siku 4.
Nipe dau lako
 
Naomba msaada wa haraka wadau. Hivi ni sumu gani ya kuua huyu ndege mweusi kama lami na mwenye laana kubwa?

Hawa ndege ni wasumbufu sana kupita maelezo na wanakiburi sana kisicho na mashiko yoyote. Yote kwa yote ni ndege wenye kisasi sana pale wanapogundua umejaribu kuwadhuru au kuwashambulia.

Changamoto ni hapa kwenye eneo ninaloishi upande wa pili kuna mnazi wameweka kiota hapo sasa wamekuwa wasumbufu sana kwa fujo za kuchafua mazingira wanaweza toka na matakataka wameokota huko wanakuja kutupa eneo hili. Au wanaweza parua mtu bila sababu. Tunashindwa kuanika vitu kwa amani kama nguo nyeupe wanazichafua kusudi kabisa.

Wanaweza anzisha fujo juu ya paa asubuhi wakiwa wengi. Ni kero juu ya kero.

Nani anayefahamu sumu ya haraka. Maana nimejaribu kuharibu kiota chao zaidi ya mara tatu ila wanatengeneza kipya. Na nimeona wapo jike na dume ndio wamekomaa.

Sasa muda huu ni kama wamenijua wakiniona tu wanaanza kuitana kwa kelele na kujazana as if kuna mkutano wa kijiji na kufanya fujo.

Sasa nadhani natakiwa kuweka sumu niuwe huyu bibi na bwana kwenye kiota ili biashara ife. Ningeweza kukata mnazi ila sasa upo kwa jirani na jirani mwenyewe ni wale wa mama sio waelewa. Atasema mnazi unamsaidia nazi na madafu.

Naombeni ushauri wa haraka sana.
Kuna pear moja dume na jike katoto kao kaliangukia juu ya paa la gari sasa asubuhi naenda job si nikakatoa kwenye paa nikakaweka pembeni nikasepa zangu, huo ugomvi una mwaka wa tatu sasa hivi yaani ikitokea naondoka bila gari ntasindikizwa na kelele karibia mitaa5 mbele, mwaka jana mwanzoni nikahamia Dom nikakaa wee siku nimerudi bado ninao tu 😅😅😅😅
 
Hao kunguru weusi wa Pwani wasio na baka jeupe asili yao ni India.

Wakati wa awamu ya pili Mzee Ruksa alienda India na kuonana na Aidha Rais au Prime Minister....sasa kule India kuna population kubwa sana mijini na jijini na wakawa wanawatumia hao kunguru kusafisha miji kwa kula mizoga na uchafu

Wakamshauri na Mzee Ruksa awalete jijini Dsm ila kaskazini na kanda zingine hawapo hao, wapo wale wenye baka jeupe shingoni ambao hata kuwaona ni nadra sana mpaka kuwe na mzoga.
Sasa alishindwa nini kuwatumia hao wenye vest nyeupe akatumia haya mandege yaliyojawa laana na mikosi kama rangi zao. Ndege siwapendi hawa yaani kuna muda nawazia niwe na risasi niwatandike.
 
Kunguru wa Dar
Wajanja Sana
Wanaweza fanya tukio ukadhani hii mbona akili kubwa kufanywa na ndege uyu
Kuna siku waliiba nyama jikoni tulizubaa kidogo tukakuta nyama hamna
Ndenge washenzi sana hawa
 
Mwaka 2018 mmoja alidakwa na mbwa wetu akaumizwa sana. Asubuhi nikambeba nikaenda kumrusha nje ya mazingira ya home. Daah, wakaalikana, wakajaa kinoma hadi niliogopa
Sasa uliingilia kwann si ungeacha mbwa amalizane nao.
 
Kuna pear moja dume na dike katoto kao kaliangukia juu ya paa la gari sasa asubuhi naenda job si nikakatoa kwenye paa nikakaweka pembeni nikasepa zangu. huo ugomvi una mwaka wa tatu sasa hivi yaani ikitokea naondoka bila gari ntasindikizwa na kelele karibia mitaa5 mbele, mwaka jana mwanzoni nikahamia Dom nikakaa wee siku nimerudi bado ninao tu 😀😀😀😀😀😀
Hawasahau hawa wapumbavu. Halafu wanashika sura na mavazi. Mimi hapa wananidharau nikitishia narusha jiwe wananitazama tu. Nikigeuka nashtukia wameniparua.
 
Hapo ni sawa na kuitaka Serikali kuanzisha Chuo cha Wizi,
 
Kunguru hawa wanadaiwa kuletwa na serikali ya uingireza kwa ajili ya kusafisha mji Mkongwe mwaka 1890 ambao kazi kubwa ni kula uchafu na kuingia Tanganyika wakati huo kuingia mwaka 1850 wakining’inia kwenye meli na maboti
 
Nimeambiwa hapa kuwa nikitumia sumu ya panya pia inafanya kazi vizuri tu sasa ngoja tu niwawekee sumu ya panya halafu nione. Nitaleta mrejesho.
 
Dawa yao ni manati sisi tuliwahi kuishi sehemu walikuwa wengi tukanunua manati tukawa tunawatungua baadhi so wakiona tu hiyo hali wanaanza kupungua au kuhama kabisa
 
Sasa uliingilia kwann si ungeacha mbwa amalizane nao.
Mkuu asubuhi nilikuwa natakiwa kumrudisha mbwa bandani lakini hiyo siku mbwa alikuwa na heka heka nyingi sana. Nilipomrudisha bandani ndio nikagundua kuna huyo ndege hawezi kutembea amejeruhiwa bawa na linatoka damu. Nikaamua kumbeba nikaenda kumuweka nje ya home. Badae ndo wakajazana eneo lile alilokuwepo majeruhi
 
Back
Top Bottom