Hivi punde
JF-Expert Member
- Apr 1, 2017
- 2,554
- 8,627
Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye amesema wananchi kama wataendelea kuichagua CCM, watarajie hali ngumu ya maisha.
Sumaye akihutubia mkutano wa kampeni wa Chadema wa uchaguzi mdogo jimbo la Ukonga leo, alisema: “Sasa hivi sio vyuma vimekaza tu bali vimepinda na hapo bado.”
“Kama tutaendelea na hicho Chama Cha Mapinduzi hii hali tunayoisema mbaya hii ni trela tu, sinema bado.”
mbaya.
“Tusipochagua chama cha upinzani tutazidi kuvumilia, mimi nilikuwa Waziri Mkuu lakini nilipoona tunakowapeleka Watanzania siko nilihamia upande wa pili ili kuwatumikia wananchi,” alisema.
Sumaye ambaye ni Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Pwani aliwataka wananchi wa jimbo hilo wamchague Asia Msangi kupitia chama hicho ili uwe mwanzo wa dalili ya 2020 upinzani kuchukua nchi.
Naye Mwenyekiti Baraza la Wazee Chadema, Hashim Juma alisema: “Imefika muda CCM ikae pembeni iwapishe waishike nchi.
“Wacha wao waende Dodoma, ila watuachie Ikulu yetu, Chadema tukichukua nchi tutarudi Dar es Salaam hapa ndiyo kwenye kila kitu,” alisema.
Sumaye akihutubia mkutano wa kampeni wa Chadema wa uchaguzi mdogo jimbo la Ukonga leo, alisema: “Sasa hivi sio vyuma vimekaza tu bali vimepinda na hapo bado.”
“Kama tutaendelea na hicho Chama Cha Mapinduzi hii hali tunayoisema mbaya hii ni trela tu, sinema bado.”
mbaya.
“Tusipochagua chama cha upinzani tutazidi kuvumilia, mimi nilikuwa Waziri Mkuu lakini nilipoona tunakowapeleka Watanzania siko nilihamia upande wa pili ili kuwatumikia wananchi,” alisema.
Sumaye ambaye ni Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Pwani aliwataka wananchi wa jimbo hilo wamchague Asia Msangi kupitia chama hicho ili uwe mwanzo wa dalili ya 2020 upinzani kuchukua nchi.
Naye Mwenyekiti Baraza la Wazee Chadema, Hashim Juma alisema: “Imefika muda CCM ikae pembeni iwapishe waishike nchi.
“Wacha wao waende Dodoma, ila watuachie Ikulu yetu, Chadema tukichukua nchi tutarudi Dar es Salaam hapa ndiyo kwenye kila kitu,” alisema.