Tindo
Platinum Member
- Sep 28, 2011
- 69,593
- 123,091
Maelezo yake yanashangaza hasa kutokana na wakati ambao ameamua kutasema.
Msemajiukweli habari hii umeileta kama faraja ya jinsi mtu akijiunga upi zani atataabika. Ila ukweli ni huu, viongozi walio wengi huwa wanabweteka sana wanapokuwa madarakani, huwa wanaishi maisha ya upendeleo uliopitiliza. Wakipanda majukwaani utawasikia watu wafanye kazi na sio kutegemea serekali!!! Huyo mtu anayezungumza hayo unakuta anapata mshahara tena mzuri, ila kila kitu anapata bure. Ngoja sasa atoke madarakani akutane na yale maisha aliyokuwa anawahubiria wenzake, mbona utamuonea huruma.
Kwa mfano hii sheria ya kuendelea kuwalipa marais na mawaziri wakuu wastaafu maisha yao yote ni upendeleo wa wazi kabisa. Iweje mtu aliyekuwa anahimiza wenzake wafanye kazi aendelee kulipwa muda wote baada ya kustaafu wakati mwingine alipokuwa madarakani wala hakuhakikisha wastaafu wengine wanalipwa stahiki zao kwa wakati? Anacholalamikia Sumaye leo ndio kile alikiona sawa wapinzani kukutana nacho alipokuwa ccm/madarakani. Na kilio hicho ndio kitakuja kusikika kwa wanaccm wengi pindi wakitoka madarakani na wengine wakafanya kwa mtindo huuhuu wanaofanyia wanaccm wapinzani wao.