Sumaye: Tubadili utawala wa vitisho

Sumaye: Tubadili utawala wa vitisho

chama kutawala muda mrefu tatizo ila mbowe kutawala chama muda mrefu sio tatizo?
 
Nimesikia kwenye dondoo za magazeti hapa kisiwani kuwa Sumaye amesema kwamba ataiondoa CCM madarakani kabla hajafa. Amenifanya nimkumbuke mzee mmoja aliyeyasema maneno kama hayo kwamba CCM itakufa ndani ya mika mitatu, baada ya muda tukapata habari kwamba yule mzee kagongwa na gari na kufariki dunia. Mungu huwa ana mipango yake na yeye na sisi tuna ya kwetu!!!


Vipi ule "utabiri wenu wa hali ya hewa" kuwa CHADEMA ingekufa kabla ya 2015 ulitimia?Hicho unachokisema kilitamkwa na mzee wa kijijini kwenu,lakini kifo cha CHADEMA kilinenwa na viongozi waandamizi wa serikali ya ccm na waliandaa mipango mingi miovu ili isaidie kutimiza utabiri wao lakini walishindwa kwa aibu.
 
Sumaye aliwahi kuwaambia wafanyabiashara wakitaka mambo yao yanyooke wawe wanachama wa CCM.
Alikuwa anakitafutia nguvu zaidi chama chake cha CCM wakati huo, na kauli hiyo haikuwa mbaya kwa wana CCM bila shaka waliishangilia. Unafikiri kwa kauli ile ya kisiasa sasa hafai kufanya siasa za upinzani?
 
Mbowe ametusaliti ana amekigharimu sana chama....
 
kwani ameshuka hadhi kivipi, je na viongozi wa CCM wanaong'ang'ania madaraka nao wanataka hadhi zisishuke???


MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!

Kutoka kuwa premier mpaka kugombea m/kiti wa mkoa Chadema kumbuka jamaa alikuwa mgombea urais kama mara mbili na amerudi nyuma.
 
Mbowe ametusaliti ana amekigharimu sana chama....
Moja Kati ya watu ambao sitokaa niwaelewe wanachokizungumza ni huyu waziri mkuu mstaafu ambae alidumu ofisini kwa miaka KUMI yote ya UONGOZI wa MKAPA..

Sijui ataongea nini nimuelewe!
 
Namsubiri Ili achukue form ya uenyekiti taifa ndio utakuwa mwisho wake wa uanachama na ataitwa msaliliti
 
Mr.Ziro katika ubora wake kama hayo unayoyasema ni ya kweli, Je, ni kwa nini uliondoka tu CCM baada ya kunyimwa nafasi ya kugombea Uraisi? kama ulilijua hilo ni kwa nini haukuondoka CCM kabla kwa maana tayari CCM ilikuwa madarakani kwa miaka zaidi ya 30 na bado ulitaka kugombea Uraisi Chama hicho!
Je, CCM wangekupitisha na leo si ungekuwa Raisi wa JMTZ kwa kupitia CCM?

Arrrggghh chadema pleaseeeee fanyeni IQ testing ya hawa viongozi wenu kabla ya kuwapa madaraka, huyu jamaa he so dumb ndiyo maana Kipanya alikuwa anamuita Mr.Ziro, hivi Mzee Mkapa aliwezaje kufanya kazi mtu ki.laza namna hii?
Kwa maandishi yako hapa unaonyesha huna sifa za kumwita Sumaye kuwa ni Kilaza. Mwanasiasa au mwanachama wa kawaida anayo haki ya kikatiba kuhama kutoka chama kimoja cha siasa na kujiunga na chama kingine. Na katiba hiyo haijaweka sababu za mwanachama/mwanasiasa kuhama. Sumaye sio mwanasiasa wa kwanza kufanya uamuzi huo. Wapo wengi tu na orodha yao inaweza kuwa ndefu mno.

Ingawa hata katiba yenyewe haiweki sababu ambazo mwanachama anaweza kuzitumia kuhama chama, wewe mwenyewe huna uthibitisho kama Sumaye alihama CCM kwa sababu ya kukosa urais, maana hata alipojiunga na Ukawa alijua hawezi kupata urais. Lakini angalau tunaweza kuamini kwamba alihama chama hicho baada ya yeye mwenyewe kujiridhisha kuwa kilikuwa kimekithiri kwa rushwa katika michakato ya kupata viongozi. Haya ndio maneno alikuwa akizungumza mara nyingi, na alifikia kusema wazi kuwa angeondoka katika chama hicho kama hali hiyo ingeendelea. Kwamba kwanini Sumaye hakuondoka CCM kabla ni hoja ya kipuuzi kwa kuwa huwezi kumpangia mwanadamu ni wakati gani aamue kufanya jambo hili au lile. Hii inabaki kuwa ni haki ya mtu mwenyewe kuamua.

Kwamba Kipanya alimwita Sumaye kuwa ni Mr Ziro na hivyo unataka dunia iamini kuwa kweli Sumaye ni Mr Ziro nayo ni hoja ya kijinga kabisa. Wewe mwenyewe unafuatilia lugha anayotumia Kipanya kumtambulisha rais wetu wa sasa, kwa hiyo unataka dunia iamini utambulisho wa rais wetu unaofanywa na Kipanya, siyo?

Mwisho, kama unaamini, kwa kiwango chochote kile, kwamba awamu ya tatu ina mambo ambayo inaweza kujivunia basi huna sababu ya kumpuuza Sumaye kama unavyojaribu kufanya hapa. Na kama utang'ang'ania basi wewe ndiye unastahili kupimwa IQ yako na sio akina Sumaye!
 
Vyama Vya Siasa Vipo Ili Watu Wafanye Siasa. Hongera Sumaye Hatimaye Utaonja Adha Ya Upinzani Kwa Vitendo
 
demokrasia pana chadema ....ccm nasikia wanaenda kumkabudhi mfalme kiti hakuna hata form....za kuomba kugombea tehteh....
 
Moja Kati ya watu ambao sitokaa niwaelewe wanachokizungumza ni huyu waziri mkuu mstaafu ambae alidumu ofisini kwa miaka KUMI yote ya UONGOZI wa MKAPA..

Sijui ataongea nini nimuelewe!

Haya ni matokeo ya Mwenyekiti wetu kuwa COMPROMISED....Mnyika yuko sahihi kuondoka....
 
Kulinda masilahi... ni kweli, hata mimi napenda kulinda masilahi yangu, kila mtu anapenda kulinda masilahi yake, nani asiyependa kulinda masilahi yake? Wewe? Sidhani, hata wewe unapenda kulinda masilahi yako.
Ni saw a kulinda lakini lazima ulinzi huo uwe sanjari na kulinda heshima yeye ni mtu mkubwa mno kwa nafasi hiyo
 
Tulikula nyasi wakati wako hebu pata nafasi hiyo baba uwarudishe nyuma 2020 wapate kura 1milion tu maana wana macho ila hawaoni wanapokea kila mgeni tu mwenye kikapu kichwani nakumpitisha hadi chumbani kwa uroho wa vilivyomo bila kujua katoka wapi na kwa nini kaja
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom