Ndiho
JF-Expert Member
- Feb 23, 2013
- 2,306
- 1,535
Watanzania tumetawaliwa na unafiki mkubwa sana. Kwanza kitendo cha Kikwete kwenda kwenye mkutano mkuu wa chama chake na kuzungumzia Sumaye na Lowasa ni UNAFIKI NA KUFILISIKA kisiasa na hata kiuongozi. Hiyo maana yake ni kwamba hotuba iliyotayarishwa iliwekwa Yale majina, kwa faida gani kwa Watanzania? Mtu aliyekaa Ikulu kwa miaka kumi na aliyekuwa mwenyekiti wa chama miaka kumi, halafu anamalizia kwa kutoa vijembe ni kukosa uvumilivu, kutawaliwa na umbea na unafiki ktk maisha. Lakini pili, Sumaye na Lowasa sasa ni wanachama wa Chadema, wao kushika wadhifa wowote ni wajibu na haki yao kama wanachama. Suala la kwàmba mtu aliyewahi kuwa Waziri Mkuu kushika madaraka ya chama ngazi za kawaida kuonekana ni kushuka thamani ni matokeo ya fikra mgando tulizolishwa na tunazoendelea kulishwa na Ccm. Na huo ndiyo UNAFIKI wa wanaccm. Mbona Urusi Putin alishika Urais, akarudi kwenye Uwaziri Mkuu na kisha Urais tenà? Na kwa nini kukaa unamfikiria mtu aliyekwisha kuondoka kwenye chama chenu? Taifa linabaki kushuhudia unafiki kwa watu walioaminiwa na wananchi na kucheza vigodoro tu kama kwamba dunia inatusubiri. Tunavaa mamitumba kwa sababu ya unafiki wenu viongozi, na kamwe hatutakaa tufanikiwe kupata maendeleo.Kutoka Waziri Mkuu wa Tanzania mpaka kugombea Umwenyekiti wa Chama Kanda halafu bado anaiambia CCM ikae chonjo kwa sababu yeye ni mgombea wa Uenyekiti wa Kanda.
Sumaye wa leo anayegombania cheo na Kubenea ndiye anayeiambia CCM ikae chonjo. This is fun to say the least.
Bora hata Mbowe akisema CCM akae chonjo unaweza kumsikiliza kwa makini kwa sababu hajawahi kuwa serikalini.
Kikwete amempiga vijembe kweli kweli na vijembe vimemfanya atoke ndani ya pango na kuanza kupiga kelele.