Sumaye atia neno sakata la Bunge kukataa kufanya kazi na CAG

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Mar 9, 2015
14,243
34,899
Waziri mkuu mstaafu wa Serikali ya Tanzania, Frederick Sumaye, amelishangaa Bunge la Tanzania kukataa kufanya kazi na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

Akizungumza na Mwanahabari Huru Sumaye ambaye ndiye Waziri Mkuu aliyedumu kwenye nafasi hiyo kwa muda mrefu kuliko Waziri Mkuu yeyote nchini Tanzania, amesema angependa kuona Bunge linatengua maamuzi hayo na kurejea kufanya kazi na CAG.

“CAG hukagua hesabu za Bunge, kwa maamuzi haya ya leo ya Bunge ina maana Bunge litakosa haki ya kukaguliwa hesabu zake. Hii itapelekea kama kuna ufujaji wa pesa kwenye Bunge, basi nchi haitafahamu kwa sababu hakuna atakayeibua taarifa hizo.

“Lakini pia CAG akiikagua Serikali na akaona kuna mahesabu hayajakaa sawa, Bunge halitaweza kuisimamia vizuri Serikali kwa kuihoji mahala zilipokwenda pesa,” amesema Sumaye.

Waziri Mkuu huyo wa zamani amesema maamuzi haya ni maamuzi mabaya sana kwa maendeleo ya Taifa na ni udhalilishaji wa ofisi ya CAG.

Naye Mbunge wa Tarime Mjini, Ester Matiko, amewalaumu wabunge wa chama tawala cha CCM ambao kwa wingi wao wamepitisha maamuzi ya kutotaka kufanya kazi na CAG.

“Wananchi ndio waone namna sisi wawakilishi wao tunavyojali matumbo yetu na kusahau maslahi ya nchi. Hapa kuna kitu kinafichwa na wameona CAG ataanika uozo.

“Na sisi Wabunge wa upinzani tunawalaumu na kuwashangaa sana hawa wenzetu wa CCM. Hivi hawaoni hatari ya kukataa kufanya kazi na CAG?” amehoji Ester Matiko.

images-321112074397..jpg
Bunge la Tanzania
Spika wa Bunge la Tanzania alikasirika baada ya CAG kukituhumu chombo hicho cha kutunga sheria kuwa ni dhaifu.

Baada ya kauli hiyo, ambayo CAG aliitoa kwebye chombo kimoja cha habari nchini Marekani, Spika wa Bunge, Job Ndugai, alimuita CAG kwenye kikao cha Kamadi ya Maadili na Mamlaka ya Bunge ili ahojiwe.

Leo Jumanne, Aprili 2, Kamati ya Maadili ilipeleka ripoti yake bungeni ili ijadiliwe. Na wabunge wengi walipiga kura za ndio wakiunga mkono azimio la Bunge kutofanya kazi na ofisi ya mkaguzi huyo.

Maamuzi hayo yamekuja siku chache baada ya CAG kuwasilisha kwa Rais ripoti mpya ya hesabu za Serikali ya mwaka 2018/19
 
Huu no udhaifu mwingine tena kama ule wa kumpiga mtu fimbo kisa ushindani wa kisiasa,kama kuwafungia wabunge wa upinzani muda mrefu kwa kutoa maoni yao yasiyomfraisha mtu fulani,kama kushindwa kuusimamia ukweli upatikane na kufeli kumhudumia mwenzenu aliyepigwa risasi,kujenga mahusiano mabovu kabisa kati ya wabunge wa chama tawala na wa upinzani,kumpoka mbunge kaziyake kwa utoro bila kumuulizia shida yake,kumuachia rais kazi za maamuzi ya bajeti na kubaki kuunga hoja,kuitetea serikali inapokosea badala ya kuikosoa,kusimamiwa na serikali badala ya kuisimamia... Uongozi ni kipaji na elimu lasivyo tutapata taasisi dhaifu mmmno zenye madaraka makubwa na kupelekea watu kuumia/kuumizwa. Tujifunze hata kwa wengine maana tunatia aibu. Ninamuunga mkono CAG.
 
Mtu kama sumae akisema kitu chochote naona kijeli tu , hatakama ni kizuir maana ndiyo waziri mkuu hivyo kutokea na alidumu katika nafasi hiyo sio kwa utendaji bali kwa aina ya uongozi wa Ben , na mambo ya CAG ashukuru mungu hata hayakuwepo kipindi chake
 
Ndugai aaaah Ngudai naona ametekeleza kwa ufasaha kabisa maagizo ya mshamba na limbukeni ,naona plan imeenda kama ilivyopangwa hela za watanzania in kuibwa mpaka basi .
 
Ndugui na Magu ndio masteringi wa hii movie.....ndio maana jiwe limeenda Ntwara ili kuwe na mada 2 za kuzungumziwa. Kila kitu kina mwisho. Naomba Asadi akaze, asijiuzulu. Halafu tuone watafanya nini?

Mammamaae zenu...tukishindwa kuwashitaki kwa kuwa mna kinga za kutoshitakiwa hata risasi tutawapiga tu. Umbwa nyie.

Sent using my Nokia Torch
 
Waziri mkuu mstaafu wa Serikali ya Tanzania, Frederick Sumaye, amelishangaa Bunge la Tanzania kukataa kufanya kazi na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

Akizungumza na Mwanahabari Huru Sumaye ambaye ndiye Waziri Mkuu aliyedumu kwenye nafasi hiyo kwa muda mrefu kuliko Waziri Mkuu yeyote nchini Tanzania, amesema angependa kuona Bunge linatengua maamuzi hayo na kurejea kufanya kazi na CAG.

“CAG hukagua hesabu za Bunge, kwa maamuzi haya ya leo ya Bunge ina maana Bunge litakosa haki ya kukaguliwa hesabu zake. Hii itapelekea kama kuna ufujaji wa pesa kwenye Bunge, basi nchi haitafahamu kwa sababu hakuna atakayeibua taarifa hizo.

“Lakini pia CAG akiikagua Serikali na akaona kuna mahesabu hayajakaa sawa, Bunge halitaweza kuisimamia vizuri Serikali kwa kuihoji mahala zilipokwenda pesa,” amesema Sumaye.

Waziri Mkuu huyo wa zamani amesema maamuzi haya ni maamuzi mabaya sana kwa maendeleo ya Taifa na ni udhalilishaji wa ofisi ya CAG.

Naye Mbunge wa Tarime Mjini, Ester Matiko, amewalaumu wabunge wa chama tawala cha CCM ambao kwa wingi wao wamepitisha maamuzi ya kutotaka kufanya kazi na CAG.

“Wananchi ndio waone namna sisi wawakilishi wao tunavyojali matumbo yetu na kusahau maslahi ya nchi. Hapa kuna kitu kinafichwa na wameona CAG ataanika uozo.

“Na sisi Wabunge wa upinzani tunawalaumu na kuwashangaa sana hawa wenzetu wa CCM. Hivi hawaoni hatari ya kukataa kufanya kazi na CAG?” amehoji Ester Matiko.

images-321112074397..jpg
Bunge la Tanzania
Spika wa Bunge la Tanzania alikasirika baada ya CAG kukituhumu chombo hicho cha kutunga sheria kuwa ni dhaifu.

Baada ya kauli hiyo, ambayo CAG aliitoa kwebye chombo kimoja cha habari nchini Marekani, Spika wa Bunge, Job Ndugai, alimuita CAG kwenye kikao cha Kamadi ya Maadili na Mamlaka ya Bunge ili ahojiwe.

Leo Jumanne, Aprili 2, Kamati ya Maadili ilipeleka ripoti yake bungeni ili ijadiliwe. Na wabunge wengi walipiga kura za ndio wakiunga mkono azimio la Bunge kutofanya kazi na ofisi ya mkaguzi huyo.

Maamuzi hayo yamekuja siku chache baada ya CAG kuwasilisha kwa Rais ripoti mpya ya hesabu za Serikali ya mwaka 2018/19
2017/2018
 
Back
Top Bottom