mbunge wa mbeya mjini leo majira ya saa 11 jioni aliifanya makambako izizime kwenye mkutano wa chadema alipohutubia wakazi wa makambako, pamoja na mambo mengine amewaambia wakazi wa nyanda za juu kusini kusimama imara kuelekea uchaguzi ujao, kwa kuwaunga mkono makamanda wa cdm katika ukombozi wa tanzania, amewaita ccm wamevuka ufisadi na kuwa chama cha wauaji, amerejea mauaji ya arusha,morogoro,iringa na operesheni tokomeza. sugu amesema wapewe nchi ili warejeshe madaraka kwa umma, akitolea wanambeya walivyorejeshewa madaraka,machinga wanavyofanya biashara kwa uhuru. mh. ameshangaa serikali kunyanyasa wafanyabiashara kwa kuita uchafu watu wanaouza nyanya nk, ameshangaa mji wa kibiashara kukosa maji, amemtahadhalisha zito kuja nyanda za juu kusini maana ataumbuka, amesema kuendelea kumwongelea ni kumpa umaarufu,amesema cdm itaendelea kuwapigania kwa gharama zozote. amesema ccm ya nyerere aliondoka nayo iliyopo ni ya wauaji,wanaozawadiana vyeo kindugu, amesema cdm ndiyo walidai katiba mpya,amemuasa kikwete apig