KIDOLEGUMBA
JF-Expert Member
- Apr 17, 2013
- 498
- 110
Barabara inajengwa Mwenge-Tegeta , Foreman anakaa Mbagala nyumba ya kupanga wakati wajapan wanakaa mlimani city, mshahara wake laki 1 na nusu , nauli , kodi, afya nk , hapo anapata tamaa ya kuiba mafuta na cement aongeze kipato mwishowe barabara ikikamilika miezi sita haifiki mahandaki yanaanza kujitokeza!! Waheshimiwa hawawafikirii kabisa wafanyakazi wazawa ambao wengi wao ndio watendaji kwenye hizo kazi za mabara bara!! Wakitetewa hawa wazawa basi uchakachuaji katika kazi za ujenzi utapungua sana!!