Smiles
JF-Expert Member
- Aug 24, 2009
- 1,231
- 107
Mbunge wa Mbeya Mjini kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mheshimiwa Joseph Mbilinyi ameainisha baadhi ya mambo muhimu ambayo atayapigania akiwa bungeni ikiwemo:
"Unajua hii sheria inaeleza adhabu ya juu tu (maximum' penalt) lakini haizungumzii adhabu ya chini (mininum penalt). Hii sheria inaeleaelea tu.
"Hii inafanya kwa mfano mtu inapotokea mtu amejaza lori aina ya Fuso kazi za wasanii zenye thamani ya Sh. milioni 10 anaweza kutozwa faini ya sh. 200,000. Sheria hii haiko wazi," anaeleza Sugu, ambaye anahesabiwa kati ya waasisi wa Bongo Fleva kiasi cha kufikia kuitwa `Nyerere wa Rap'.
Anasema muziki unalipa kama wezi wa kazi za wasanii watadhibitiwa na kuongeza yeye alifanikiwa kimuziki baada ya kuamua kusimamia kazi zake mwenyewe na kuuza nakala zaidi ya 40,000 za albamu ya `Ndani ya Bongo' mwaka 1996.
"Tulipeleka maombi yetu mwaka 1995 kwenye Wizara ya Viwanda na Biashara na tuliambiwa maombi yetu yalikubaliwa lakini kukawa kuna urasimu. Kipindi Rais Jakaya Kikwete alipoingia madarakani mwaka 2005 tulipeleka tena maombi yetu, Waziri wa wakati ule Nazir Karamagi alikubaliana na ombi letu na akasaini.
"Kilichobaki ilikuwa kuchapishwa kwenye Gazeti la serikali ili iwe sheria," anaeleza Sugu, ambaye anaongeza baada ya kufikia hatua hiyo walikuja kutaarifiwa faili lao liliibiwa kutoka meza ya Karamagi.
Anasema kuna haja ya baraza hili kusambazwa nchi nzima kwani haoni mantiki ya msanii anayetoka mkoani kufunga safari Dar es Salaam kwa ajili ya kujisajili na anaeleza kuwa sanaa nchi nzima sasa inakuwaje Basata iwe Dar es Salaam pekee.
Kuunganisha wasanii
Sugu anaeleza itakuwa ngumu kwa wasanii kupigania haki zao bila ya kuwa kitu kimoja na ametaka wasanii hao kuwa na chombo cha kuwateta na atapigania kufufuliwa kwa Chama cha Wasanii wa muziki wa Kizazi Kipya (Tuma).
Anaeleza kuwa chama hicho kilisajiliwa mwaka 2004 lakini kilishindwa kuibuka kutokana na wasanii wenyewe wa Bongo Fleva kukosa ushirikiano. Anasema atashirikiana na wabunge wengine kutetea wasanii lakini nao wanatakuwa kuwa kitu kimoja.
Sugu anasema kitendo cha wasanii kukosa umoja ndio maana hata Rais Jakaya Kikwete alipotoshwa wakati alipotaka kusaidia wasanii wa Bongo Fleva. "Rais Kikwete kwa nia njema alitaka kutusaidia lakini kuna watu wakampotosha kuwa eti wasanii tunataka studio
.
"Kaka studio ziko kibao mtaani hadi zinakosa wasanii wa kurekodi," anasema Sugu, ambaye anamshauri Rais Kikwete kutengeneza mazingira mazuri ya wasanii kufanya kazi. Nitaandaa mikutano na matamasha ya kuwaunganisha wasanii. Siwezi kuacha harakati za muziki wa Bongo Fleva," anaeleza Sugu, ambaye amesema hatarudi jukwaani bali ataendeleza harakati za kupigania kuinua maisha ya wasanii ya kutumia njia nyingine.
- Kutumikia wananchi wa jimbo lake
Sugu, ambaye pia anajulikana kwa majina ya utani ya `Mr II' au `II Proud', anasema asilimia 99 ya ajenda yake itakuwa kutatua matatizo ya wananchi wa Mbeya, ambao wana changamoto nyingi.
- Sheria ya Haki Miliki
Anasema itakuwa ni sehemu kubwa ya majukumu yake lakini kuna mambo, ambayo angependa ayafanyie kazi ili asaidie kutatua matatizo ya sanaa ya muziki wa Bongo Fleva, ambao anakiri umemtoa kimaisha.
"Unajua hii sheria inaeleza adhabu ya juu tu (maximum' penalt) lakini haizungumzii adhabu ya chini (mininum penalt). Hii sheria inaeleaelea tu.
"Hii inafanya kwa mfano mtu inapotokea mtu amejaza lori aina ya Fuso kazi za wasanii zenye thamani ya Sh. milioni 10 anaweza kutozwa faini ya sh. 200,000. Sheria hii haiko wazi," anaeleza Sugu, ambaye anahesabiwa kati ya waasisi wa Bongo Fleva kiasi cha kufikia kuitwa `Nyerere wa Rap'.
- Anataka Cosota ipewe meno
Sugu anasema angependa kuona Taasisi ya Kusimamia Haki Miliki (Cosota) ikiimarishwa ili iweze kuwajibika vizuri. Anadai Cosota kwa sasa ni taasisi ndogo kuweza kusimamia kazi za wasanii nchi nzima.
Anasema muziki unalipa kama wezi wa kazi za wasanii watadhibitiwa na kuongeza yeye alifanikiwa kimuziki baada ya kuamua kusimamia kazi zake mwenyewe na kuuza nakala zaidi ya 40,000 za albamu ya `Ndani ya Bongo' mwaka 1996.
- TRA waweke alama kwenye kazi za wasanii
Sugu anapendekeza kuwekwa kwa alama au stika za Mamlaka ya Kukusanya Mapato ya Kodi (TRA)kwenye kazi za wasanii ili kudhibiti wizi. Anatetea utaratibu huo kuwa ni mzuri kwani utasaidia Mamlaka ya Kukusanya Mapato ya Kodi (TRA) kuongeza wigo wa mapato na utadhibiti wenye tabia ya kudurufu kazi za wasanii.
"Tulipeleka maombi yetu mwaka 1995 kwenye Wizara ya Viwanda na Biashara na tuliambiwa maombi yetu yalikubaliwa lakini kukawa kuna urasimu. Kipindi Rais Jakaya Kikwete alipoingia madarakani mwaka 2005 tulipeleka tena maombi yetu, Waziri wa wakati ule Nazir Karamagi alikubaliana na ombi letu na akasaini.
"Kilichobaki ilikuwa kuchapishwa kwenye Gazeti la serikali ili iwe sheria," anaeleza Sugu, ambaye anaongeza baada ya kufikia hatua hiyo walikuja kutaarifiwa faili lao liliibiwa kutoka meza ya Karamagi.
- Mabadiliko ya Basata
Sugu anasema kuwa Baraza la Sanaa Tanzania (Basata) linafanya kazi zake kizamani.
Anasema kuna haja ya baraza hili kusambazwa nchi nzima kwani haoni mantiki ya msanii anayetoka mkoani kufunga safari Dar es Salaam kwa ajili ya kujisajili na anaeleza kuwa sanaa nchi nzima sasa inakuwaje Basata iwe Dar es Salaam pekee.
Kuunganisha wasanii
Sugu anaeleza itakuwa ngumu kwa wasanii kupigania haki zao bila ya kuwa kitu kimoja na ametaka wasanii hao kuwa na chombo cha kuwateta na atapigania kufufuliwa kwa Chama cha Wasanii wa muziki wa Kizazi Kipya (Tuma).
Anaeleza kuwa chama hicho kilisajiliwa mwaka 2004 lakini kilishindwa kuibuka kutokana na wasanii wenyewe wa Bongo Fleva kukosa ushirikiano. Anasema atashirikiana na wabunge wengine kutetea wasanii lakini nao wanatakuwa kuwa kitu kimoja.
Sugu anasema kitendo cha wasanii kukosa umoja ndio maana hata Rais Jakaya Kikwete alipotoshwa wakati alipotaka kusaidia wasanii wa Bongo Fleva. "Rais Kikwete kwa nia njema alitaka kutusaidia lakini kuna watu wakampotosha kuwa eti wasanii tunataka studio
.
"Kaka studio ziko kibao mtaani hadi zinakosa wasanii wa kurekodi," anasema Sugu, ambaye anamshauri Rais Kikwete kutengeneza mazingira mazuri ya wasanii kufanya kazi. Nitaandaa mikutano na matamasha ya kuwaunganisha wasanii. Siwezi kuacha harakati za muziki wa Bongo Fleva," anaeleza Sugu, ambaye amesema hatarudi jukwaani bali ataendeleza harakati za kupigania kuinua maisha ya wasanii ya kutumia njia nyingine.