Subtitles za bongo movies ni le majangaz

Subtitles za bongo movies ni le majangaz

Mwanamwana

Platinum Member
Joined
Aug 1, 2011
Posts
9,602
Reaction score
22,707
Hii ni moja ya movie ya wabongo iliyowekewa maneno ya kiingereza na wabongo, kwa mwendo huu tutabakia kuchekwa na wenzetu kwa lugha hii mbovu ya movie zetu.

jf bongo movie.png

jf bongo movie 1.png
 
😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂
 
Hahahahahaa...hua nashangaa sana wanavyochapia
 
Kuna watu humu huwa wanasema kwa mtanzania kuandika kiingereza ni kuendekeza ukoloni.
 
Aliye andika hizo subtitles lazima atakuwa ni Ray tu..!!
 
hv hizi picha si huwa zinakuwa na wahariri imekuaje haikuhaririwa
 
His approach is "to cross the river when he gets there". No clear strategy for now.

Inategemea huyo anayehariri kama anajua lugha au lah

tatizo wanakwepa gharama

wanaojua kiingereza kwa ufasaha wapo wengi sana nchini

walipwe pesa wafanye kazi.....

Lengo la kuweka hzi subtitle ni kufanikisha kuuza nakala nje ya nchi.. Lakn kwa style hii ni dhahiri wanajidharirisha
 
Ukiangalia filamu nyingi za kitanzania, utakuta mwongozaji, mtunzi, mhariri, mzalishaji, n.k ni mtu mmoja (huyo huyo). Kwahiyo si rahisi kugundua makosa madogo madogo. Kama wangelikuwa ni watu angalau watatu tofauti basi uwezekano wa kukosea au kufanya makosa makubwa ungepungua!

wakitaka movie zetu ziwe na soko wabadilike, vijana wachuo hawana ajira wakati ajira zipo kibao no kama hizi.
 
wakitaka movie zetu ziwe na soko wabadilike, vijana wachuo hawana ajira wakati ajira zipo kibao no kama hizi.

Tatizo ni pesa za kuwalipa! Hii ni sababu inayowanya wabane matumizi.
 
Hivi bongo movie bado zinaendelea kutoka?
Kwa mara ya mwisho niliangalia movie inayoitwa sijui ni jeff la mark yule wa shumileta tangu hapo sjui kama kuna bongo movie
 
Ingekuwa live tungewasamehe, hii kitu ni recorded then edited but still. Sucks
 
kuna iyo moja ndio nilichoka kabisa:
"Inabidi ujue kuwa pole pole ndio mwendo = You has to know that slow slow yes movement"
 
Tatizo ni pesa za kuwalipa! Hii ni sababu inayowanya wabane matumizi.

mkuu lakini ujue hatujaamua kuinvest vya kutosha kwenye industry hii, lakini ni among ya sehemu kwenye pesa nyingi sana, sema na wei nao wanaiharibu sana.
 
me dont no english,kisa kajua kushoot camera na ndo director hata english course hataki toka apate jimama lililompatia huto tu camera yeye ndo yeye sa utamwambia nini
 
mkuu lakini ujue hatujaamua kuinvest vya kutosha kwenye industry hii, lakini ni among ya sehemu kwenye pesa nyingi sana, sema na wei nao wanaiharibu sana.

Wakati ndiyo huu wa wenye nia kutumia fursa hizi. Ni suala la uamuzi tu. Wapo wengi wenye uwezo ila bado hawajajitambua.
 
da hii kali sana aisee ni zaidi ya nomaaaa ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha
 
Back
Top Bottom