MINOCYCLINE
JF-Expert Member
- Apr 2, 2015
- 8,011
- 16,748
Mimi ni Shabiki wa Simba SC ila nadhani kama kuna Mchezaji Mzawa ambaye Watanzania tuna Roho Mbaya, Wivu na Unafiki wa Kutomuimba na Kumtukuza inavyotakiwa ni Kiungo Mshambuliaji na Winga Farid Malick Mussa wa Yanga SC.
Kama kuna Mchezaji ambaye leo katika Mechi ya Taifa Stars na Uganda Cranes ndiyo ameupiga mwingi, alikuwa ameishika Timu nzima na nilishangaa kuona akifanyiwa Sub na Kocha ni Farid Malick Mussa.
Na kama kuna Wachezaji ambao leo hawakuitendea Haki Jezi ya Taifa Stars ni Washambuliaji Kibu Denis wa Simba SC na George Mpole wa Geita Gold FC.
Na kama kuna Wachezaji ambao kwa nilivyoona Commitment na Determination yao wangeanza tokea mwanzo badala ya Kibu na Mpole Timu ya Taifa Stars leo ingeibuka na Ushindi hata wa Magoli mengi ni akina Anwar Jabir na Danny Lyanga.
Goli tulilofungwa ni Makosa yale yale ya Beki wa Simba SC Mohammed Hussein Tshabalala ambayo hata akiwa Simba SC huwa anayafanya kutokana na tabia yake ya Kujiamini kunakopitiliza na kupenda Kucheza Mpira wa Kimaonyesho.
Naheshimu mno Uimara wa Golikipa wa Taifa Stars ambaye pia anaichezea Simba SC Aishi Salum Manula ila ana Makosa ya Kufungwa Magoli mepesi ambayo kama angekuwa anazingatia Goalkeeping Skills and Principles kamwe asingefungwa na asingekuwa anafungwa.
Wachezaji ambao pamoja na kwamba Leo Taifa Stars yetu imefungwa na Uganda Cranes ila MINOCYCLINE sina Deni nao lolote na nawapongeza kwa Kucheza vyema ni Beki Kibwana Shomary, Beki Dickson Job na Bakari Mwamnyeto, Viungo Jonas Mkude, Abubakary Salum, Feisal Salum na Farid Mussa.
Najua nia ya Uganda Cranes hata Kimchezo walikuwa wanahitaji tu Sare ( Draw ) hapa Dar es Salaam Tanzania Ili wakatumalize vizuri Kwao Kampala Uganda na tayari naanza kuona na kusikia Watanzania wakikata Tamaa ila Binafsi nina uhakika kama Wachezaji wa Taifa Stars watajengwa na watasaidiwa Kisaikolojia na wakajitambua vyema tuna uwezo wa Kuwafunga Cranes pale Namboole au Nakivubo Stadium Weekend ijayo.
Tujiamini na tuwatie tu Moyo Stars!!!!
Cc: Proved
Kama kuna Mchezaji ambaye leo katika Mechi ya Taifa Stars na Uganda Cranes ndiyo ameupiga mwingi, alikuwa ameishika Timu nzima na nilishangaa kuona akifanyiwa Sub na Kocha ni Farid Malick Mussa.
Na kama kuna Wachezaji ambao leo hawakuitendea Haki Jezi ya Taifa Stars ni Washambuliaji Kibu Denis wa Simba SC na George Mpole wa Geita Gold FC.
Na kama kuna Wachezaji ambao kwa nilivyoona Commitment na Determination yao wangeanza tokea mwanzo badala ya Kibu na Mpole Timu ya Taifa Stars leo ingeibuka na Ushindi hata wa Magoli mengi ni akina Anwar Jabir na Danny Lyanga.
Goli tulilofungwa ni Makosa yale yale ya Beki wa Simba SC Mohammed Hussein Tshabalala ambayo hata akiwa Simba SC huwa anayafanya kutokana na tabia yake ya Kujiamini kunakopitiliza na kupenda Kucheza Mpira wa Kimaonyesho.
Naheshimu mno Uimara wa Golikipa wa Taifa Stars ambaye pia anaichezea Simba SC Aishi Salum Manula ila ana Makosa ya Kufungwa Magoli mepesi ambayo kama angekuwa anazingatia Goalkeeping Skills and Principles kamwe asingefungwa na asingekuwa anafungwa.
Wachezaji ambao pamoja na kwamba Leo Taifa Stars yetu imefungwa na Uganda Cranes ila MINOCYCLINE sina Deni nao lolote na nawapongeza kwa Kucheza vyema ni Beki Kibwana Shomary, Beki Dickson Job na Bakari Mwamnyeto, Viungo Jonas Mkude, Abubakary Salum, Feisal Salum na Farid Mussa.
Najua nia ya Uganda Cranes hata Kimchezo walikuwa wanahitaji tu Sare ( Draw ) hapa Dar es Salaam Tanzania Ili wakatumalize vizuri Kwao Kampala Uganda na tayari naanza kuona na kusikia Watanzania wakikata Tamaa ila Binafsi nina uhakika kama Wachezaji wa Taifa Stars watajengwa na watasaidiwa Kisaikolojia na wakajitambua vyema tuna uwezo wa Kuwafunga Cranes pale Namboole au Nakivubo Stadium Weekend ijayo.
Tujiamini na tuwatie tu Moyo Stars!!!!
Cc: Proved