Suala la Kofia mbili laibuka tena CCM

Suala la Kofia mbili laibuka tena CCM

Inferiority complex ni udhaifu mbaya sana.Source kweli iwe Raia Mwema?
CCM wakiamua jambo lao utajua tu hamna haja ya kubwatuka na kukimbilia uzushi.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Watajuana wenyewe. Mama keshawaambia vitu vyote vitapanda bei.

Tujiandae na kutembea kwenda makazini. Maana kauli nyingine kama kiongozi kuzitoa ni kama kutoa mwanya kwa walanguzi kupandisha bei vitu.

Najua comment yangu ni nje ya mada lakini ndio frustration za maisha tena.
Comment yako sio nje ya mada ni muhimu kwa ustawi wa wananchi kuliko hao wanaogombsnia vyeo!

Matamshi ya Samia kuwa bei za vitu zitapanda ( inflation) ni kwa sababu tu ya bei ya mafuta kupanda inapotosha na kuwapa mwanya wafanyabiashara kupandisha bei za vitu kiholela !
Serikali inatakiwa kithibiti kupandisha huku kwa bei kiholela( price gouging) kama njia ya kupunguza makali ya mfumuko wa bei.
Rais anaweza kuwa na muda na kuwa makini zaidi kuisimamia serikali iwapo ataruhusiwa kuwa na kofia moja na kuachia shuhuri za chama.
 
Hii ni nzuri sana maana ingekuwa ni hivyo hata Mwendakuzimu angekuwa controlled!
hiyo ndio itapunguza uchawa hiyo system mbona hata ANC ndio wako hivyo ndio maana walikua na nguvu ya kuwaondoa maraisi Thabo mbeki na Jacob Zu
 
Wamechelewa!

Kwa mwenyekiti waliyenaye kwa sasa,wanatakiwa wapitishe vyote vilivyoshindikana awali

Kama ANC tu,Rais akiwa na nyendo sizo, chama kinamuita ajieleze kama wanachama wengine halafu kinafanya maamuzi kitu ambacho hakiwezekani ndani ya CCM kwa sasa.
 
Wamechelewa!

Kwa mwenyekiti waliyenaye kwa sasa,wanatakiwa wapitishe vyote vilivyoshindikana awali

Kama ANC tu,Rais akiwa na nyendo sizo, chama kinamuita ajieleze kama wanachama wengine halafu kinafanya maamuzi kitu ambacho hakiwezekani ndani ya CCM kwa sasa.
Kwa wana CCM wenzangu, hakuna mwenyekiti aliyeko madarakani anaweza kukubali eti ajivue uwenyekiti wake- ili iweje? ili tuanze kumwita na kumtisha tisha kwenvye vikao !! kwa sasa Maza yupo gado, hapa ndugu zangu tushanoa, tupangeni jengine.
 
mshikamano wetu ndani ya chama ni ule ule na utamaduni wetu ni ule ule - asiyetaka basi atupishe.
Huo mshikamano wa mwenyekiti kuamua atakavyo hauko ccm, uko pande zenu zile.
 
Huo mshikamano wa mwenyekiti kuamua atakavyo hauko ccm, uko pande zenu zile.
usitukumbushe ya jobo ndugu, unatutia simanzi - nimekosa sana mimi, nimekosa saana.
 
Inferiority complex ni udhaifu mbaya sana.Source kweli iwe Raia Mwema?
CCM wakiamua jambo lao utajua tu hamna haja ya kubwatuka na kukimbilia uzushi.
Katika wenye ccm wewe haumo kabisaaaaa !!!
 
Hayo ya kwenye Chama Chao ni wenyewe na Katiba zao, ingawa mimi kama mwananchi nisiye na Chama kwenye huduma za kijamii sipendi kuona Makada wakifanya hizo kazi sababu badala ya kuhudumia wananchi wanafanya kampeni na kuhudumia chama chao

Mbaya zaidi mimi nakasirika huku kitaa watu wana vipara let alone Kofia hata moja..., Hao waliopo madarakani watengeneze Sera za angalau kila mtu apate hata nuso kofia au ka-leso ka kujifunika kipara chake
Dah! We jamaa umewaza mbali sana
 
Kwa wakati huu naiona hii hoja ikiwa na mashiko sana make akina "hawa" bila spana hatuchelewi kuuzwa Ulaya
 
Taarifa kutoka CCM zinadokeza kwamba katika maandalizi ya chaguzi za ndani yameibuka mapendekezo kwamba Mtu mmoja hapaswi kuwa na vyeo viwili , kwa mfano huwezi kuwa RC halafu ukawa kiongozi wa chama , au ukawa Mbunge halafu uwe tena Mwenyekiti wa CCM popote wilayani au mkoani

Bali kisichofahamika ni iwapo suala hilo litamgusa hadi mwenyekiti wa Taifa au la .

Haya mambo yaliwahi kuibuliwa na kuzimwa wakati wa awamu ya 4 , Je safari hii yatawezekana ?

Chanzo : Raia Mwema

Suala la Kofia mbili laibuka tena CCM kwa sababu Rais tuliye naye ni chaguo la katiba sio wananchi..​

 
Back
Top Bottom