Strategy ya Lissu Kanda ya Ziwa ina mapungufu kidogo

Strategist/s wa Lissu a/wa/mempotosha kweri kweri kwa kumfanya ang'ang'anie Kanda ya Ziwa. Matokeo yake, atakosa kura za Kanda nyingine maana watahisi hawana umuhimu kwake na atazikosa za Kanda ya Ziwa pia maana sisi tuliishamchagua JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI (JIWE)!!!!!!

Kanda zote amefika, tena mara mbili. Kimbinu, ukiacha mapungufu machache, CHADEMA wanafanya vizuri sana ukizingatia vizingiti walivyowekewa na jicho kali linalowaangalia.

Inaonyesha walifanya maandalizi mengi kimya kimya, ndiyo maana tunashangaa umati wa watu wanaojitokeza kila sehemu tena bila kutangaziwa na media kubwa.
 
Huu unaoshauri hapa ni ukabila mbaya, kabisa, Wasukuma sio wakabila ndio maana Usukumani tumechagua wabunge kibao ambao sio Wasukuma!.
Magufuli atachaguliwa na Watanzania kwasababu amekubalika kwa uchapakazi wake na sio kwasababu ni Msukuma!.
P
Kuna Wasukuma siyo wakabila, na ukitaka nitakutajia wachache, lakini wewe ni Mkabila, Magufuli anayejifanya Msukuma naye ni Mkabila hasa.
 
Kanda zote amefika, tena mara mbili. Kimbinu, ukiacha mapungufu machache, CHADEMA wanafanya vizuri sana ukizingatia vizingiti walivyowekewa na jicho kali linalowaangalia.
Tatizo hawana mikakati ya kisayansi na hapo ndio wanaposhindiwa.
 
Ushauri wangu kwa timu ya kampeni ya Lissu, kama muda bado unaruhusu, na nyie mkiwa mikoa hiyo yenye Wasukuma wengi, anzeni kutwanga lugha yao. Lissu jifunze maneno mawili matatu hata ya kuwachekesha tu, yatasaidia.
Mm nimekuelewa sana mkuu. Asante kwa ushauri.
 
Huu unaoshauri hapa ni ukabila mbaya, kabisa, Wasukuma sio wakabila ndio maana Usukumani tumechagua wabunge kibao ambao sio Wasukuma!.
Magufuli atachaguliwa na Watanzania kwasababu amekubalika kwa uchapakazi wake na sio kwasababu ni Msukuma!.
P

Bro, tatizo siku hizi haueleweki. Unajaribu kula kote kote, matokeo yake kila mtu anakudharau, samahani lakini.

Umetoka kusema huu ni ukabila mbaya wakati huo huo unafumba macho pale mtu wako anapofanya mambo hayo hayo. Mkuu, umejipotezea heshima sana.

At least jaribu kuwa consistent, labda kuna watu watakuamini.
 
Huu unaoshauri hapa ni ukabila mbaya, kabisa, Wasukuma sio wakabila ndio maana Usukumani tumechagua wabunge kibao ambao sio Wasukuma!.
Magufuli atachaguliwa na Watanzania kwasababu amekubalika kwa uchapakazi wake na sio kwasababu ni Msukuma!.
P
Baada ya WAJUMBE kukukata na mwenyekiti alipadhihilisha kuwa ,pamoja na upamne wako wote MaCCM hayakuitaji hata kukuona.

Hatimate sasa nyoka mmeanzi kuchomoza kutoka kwenye mapango mlikojificha,
 
Nianze kwa kusema, wote tunajua strategy ya ushindi wa Magufuli toka uchaguzi wa 2015 na hata uchaguzi huu wa 2020 imejikita kuhakikisha anazoa kura za kutosha kutoka kwa Wasukuma.

Natambua huko Kanda ya Ziwa kunajumusha pia mikoa ya Kagera na Mara ambako nadhani Lissu anaenda kufanya vizuri sana.

Wasiwasi wangu upo kwenye kuwashawishi Wasukuma wamuache yule anayejitanabaisha kama mwenzao. Kila akipata upenyo, Magufuli anakitwanga Kisukuma, na hafanyi hivi kwa bahati mbaya.

Magufuli anaweza kuwa hajui Kiingereza na hana exposure sana ya mambo ya kimataifa ila anayaelewa sana mambo ya makabila. Hata yale aliyoyakwaza amefanya hivyo akiwa anajua anawakwaza. Labda anaona hawahitaji.

Ushauri wangu kwa timu ya kampeni ya Lissu, kama muda bado unaruhusu, na nyie mkiwa mikoa hiyo yenye Wasukuma wengi, anzeni kutwanga lugha yao. Lissu jifunze maneno mawili matatu hata ya kuwachekesha tu, yatasaidia.

Kwenye issue za sera, waambieni hayo hayo mnayowaambia sasa ila katika lugha yao. Watawaamini zaidi. Waambieni pia kuna wanasiasa wanataka kuwatumia tu kama chambo.
Hata kama ataongea kijaruo hatashinda, kwa hizi kanda shida kubwa huwa ni kwa wabunge na hasa wakati wa michakato lakini si nafasi ya uraisi. Kosu hatafikisha kura milioni tatu na hiyo itakuwa historia kwake, na atakuwa kavunja rekodi za wagombea wa chadema, tifauti na mgombea wao ambae ni m CCM Lowasa.
 
Asante kwa ushauri mkuu. Ni mawazo mazuri kutoka kwenye roho yenye heri na matashi mema. Ila mkuu, uchaguzi huu ni wa kihistoria. Magufuli hata Chato hatoboi. Kuna chuki huko imeibuka usiseme. Kweli wahenga walisema "mali za juha huliwa na mweledi" na "maisha bila busara ni hasara".
Mshaulini Lisu akaombe huko kura ili awabadilishe waliobaki, mbona aliwakwepa sasa wakati ilitakiwa akapige bao hapo?
 
Nianze kwa kusema, wote tunajua strategy ya ushindi wa Magufuli toka uchaguzi wa 2015 na hata uchaguzi huu wa 2020 imejikita kuhakikisha anazoa kura za kutosha kutoka kwa Wasukuma.

Natambua huko Kanda ya Ziwa kunajumusha pia mikoa ya Kagera na Mara ambako nadhani Lissu anaenda kufanya vizuri sana.

Wasiwasi wangu upo kwenye kuwashawishi Wasukuma wamuache yule anayejitanabaisha kama mwenzao. Kila akipata upenyo, Magufuli anakitwanga Kisukuma, na hafanyi hivi kwa bahati mbaya.

Magufuli anaweza kuwa hajui Kiingereza na hana exposure sana ya mambo ya kimataifa ila anayaelewa sana mambo ya makabila. Hata yale aliyoyakwaza amefanya hivyo akiwa anajua anawakwaza. Labda anaona hawahitaji.

Ushauri wangu kwa timu ya kampeni ya Lissu, kama muda bado unaruhusu, na nyie mkiwa mikoa hiyo yenye Wasukuma wengi, anzeni kutwanga lugha yao. Lissu jifunze maneno mawili matatu hata ya kuwachekesha tu, yatasaidia.

Kwenye issue za sera, waambieni hayo hayo mnayowaambia sasa ila katika lugha yao. Watawaamini zaidi. Waambieni pia kuna wanasiasa wanataka kuwatumia tu kama chambo.
Yan wewe unawaza Ukabila, ndo akina Magufuli nyie tunataka tuwaondoe!
 
Kanda ya Ziwa aiwezi muacha salama Lissu,ni kanda ambayo inatoa kura nyingi za Urais miaka yote.
 
Ujue hata wasukuma wamefikia wamemchoka msukuma mwenzao na hii nimeikuta chatto 2019 wakijiapiza kuwa watamnyima kura jiwe ..yapo Mambo mengi hajawatekelezea hivyo hiyo kanda Kuna 50/50 tofauti na kanda za nyanda za juu kaskazini na kusini ambapo jiwe ataendelea kupoteza kura ..kifupi huu mwaka ccm andikeni mmeumia kiukweli ..jiwe hawezi vuka 40% ya kura zote
 
Huu unaoshauri hapa ni ukabila mbaya, kabisa, Wasukuma sio wakabila ndio maana Usukumani tumechagua wabunge kibao ambao sio Wasukuma!.
Magufuli atachaguliwa na Watanzania kwasababu amekubalika kwa uchapakazi wake na sio kwasababu ni Msukuma!.
P
Tunataka mfumo wa majimbo (Federation) ili viongozi wetu tuwachague wenyewe kusudi wanapokosea tuweze kuwawajibisha tofauti na sasa ambapo watu walamba miguu ya mtawala ndio hupewa uteuzi na wananchi hawana uwezo wa kuwawajibisha.
 
Msiogope enyi kundi dogo maana Mungu ameamua kuwapa ufalme huu.

Lisu amekuja bila chochote mkononi. Bila majeshi, bila vyombo vya habari, bila matajiri nyuma yake, bila wasomi njaa nyuma yake, bila wasanii nyuma yake.Huyu mtu ana nini basi,? Bila shaka Mungu yupo naye !! Mwaka huu Mungu atajidhihirisha kwa watanzania kuwa yeye ndiye aliyeumba maliasili za nchi hii na sio Polepole wala Bashiru wala wakurugenzi wala NEC. Na yeye Mungu naam, Mungu wa Majeshi ndiye anayewaweka watawala naam ni Mungu wa vita ,alitakalo litafanyika . Yeye Mungu pekee ndiye Alfa na Omega ,naam mwanzo na Mwisho ,anamuiinua huyu na kumshusha, alimuinua JPM na atamshusha akitaka.
Mungu Alizuia Korona isiingie Afrika kwa sababu zake.
Naam ni Mungu aliyemwepusha Tundu Lisu na Mauti baada ya Watu wenye hila kumpiga risasi bila kuwa na hatia yoyote. Mungu akachukizwa akamuokoa na kumrejesha kwenye siasa na sasa amempa kibali mbele ya watanzania.

Sikieni enyi watanzania Magufuli sio Mungu na hatakua Mungu. Magufuli ni mwanadamu kama walivyo wengine. Musikubali kuingia kwenye dhambi ya dhulma na kuua watanzania wenzenu kwa sababu ya binadam ambaye hana amri juu ya pepo ya MTU wala ya kwake.

Kila mtanzania ajue wazi kuwa kupanda mbegu ya dhulma kama Polepole na Bashiru wanavyofanya ili tu familia zao zineemeke ni kumchukiza Mwenyezi Mungu. Laana na Damu zilizomwagwa kutokana na jeuri yao waliyojiapiza nayo hakika zitawafuata wao na familia zao.
Bashiru na Polepole wanatenda uovu ambao wao hawatamani kutendewa. Mwenyezi Mungu amekataza kumtendea mwenzako lile usilotaka kutendewa wewe.
 
Wote mliochangia siwapingi. Ulikuwa tu ni ushauri. Inabidi juhudi za ziada zifanyike ili kuzigawa kura za Wasukuma.

Nimetoka kuangalia video hii hapa chini, nimeona amewasalimu kwa lugha yao, hapo safi. Kilichobaki, wale wanaobaki huko Sukumaland kuendelea na kampeni, wajaribu kuzingatia ushauri wangu.

Ushauri mzuri zaidi ni Lisu kumhakikishia mkubwa wa Polisi nafasi yake mpaka astaafu. Pia Mkubwa wa JWTZ asimame nyutro kwani General ni international rank asijihusishe na siasa.

Kwa sasa Lisu atafute namna ya kuungwa mkono na vyombo vya Dola kwa kuanza safu nzima na sio kuwatisha kuwa atavunja jeshi lile Mara nitalifumua n.k. Wengi wanahofia nafasi zao kwani CCM imekua ikiwatumia kama dili lao ndio maana baada ya uchaguzi hawana habari bao tena .

Mpaka sasa Lisu ameshinda kwenye suala la kura. Cha msingi ni kuanza sasa kuwatafuta watu wenye imani kubwa ili wawe wanaendelea kusoma dua njema kwa wasimamizi wema na mbaya kwa wasomamizi wabaya ili wasije wakafaidika kwa udhalimu wao.
Hata wabunge na madiwani watakaopitishwa kwa dhulma nao pia wasomewe dua mbaya wasije wakanufaika kwa dhulma yao.

Albadir zianze kusomwa sasa kwa Wakurugenzi na wasimamizi waliovuruga uteuzi wa wagombea na kuwaengua watu kwa dhulma bila kufuata sheria kwa haki.
Hakika Mwenyezi Mungu ni Mungu wa Haki.

Lisu atawapiga CCM Nyanda za juu kusini, atawapiga Kaskazini, atawapiga Kigoma na Mpanda ,atawapiga ,Morogoro, DSM,atawapiga ,Lindi na mtwara, atawapiga ,Unguja na Pemba, atawapiga. Atawapiga. Mara, Atawapiga Mwanza, atawapiga. Geita Atawapiga Kagera,Atawapiga Singida .
Kifupi Lisu atashinda kwa kura za kimbunga maeneo hayo. Kwingine watatoka droo na CCM.
 
Back
Top Bottom