Story za Prof. Palamagamba Kabudi

Story za Prof. Palamagamba Kabudi

Historia nzuri sana;

Uhuru wa Zimbabwe ulipatikana kwa wao kutoa kafara Ardhi yao.
 
4 Sep 2019

MSIMAMO WA TANZANIA KUHUSU MAUAJI AFRIKA KUSINI, PROF KABUDI AZUNGUMZA!

Waziri wa Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi, amezungumzia mauaji ya wageni yanayoendelea huko nchini Afrika Kusini...

Source : Global TV online
 
Wednesday, September 25, 2019
New York


TANZANIA KUNUFAIKA NA DOLA ZA KIMAREKANI MILIONI 120 KUTOKA SERIKALI YA MAREKANI

Picha : Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi na Naibu Waziri wa Afya wa Marekani Admiral Brett Giroir.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akiwa Admiral Brett Giroir. baada ya mazungumzo.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI.
MAREKANI KUTOA DOLA ZA MAREKANI MILIONI 120 KUPANDA NA UGONJWA WA SELI MUNDU (SICKLE CELL)

Tanzania ni miongoni mwa baadhi ya Nchi zinazotarajiwa kunufaika na kiasi cha dola za Kimarekani milioni 120 zilizotengwa na Serikali ya Marekani kwa ajili ya utafiti wa kupambana na ugonjwa wa seli mundi (sickle cell).

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya wa Marekani Admiral Brett Giroir wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi jijini New York Nchini Marekani.

Admiral Brett ameutaja mkutano wake na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi kama mwanzo mpya wa ushirikiano baina ya Tanzania na Marekani na kuongeza kuwa Nchi yake ina nyenzo zote ikiwemo teknolojia ya kuoambana na maradhi ya seli mundu ili kuboresha Maisha ya watoto wanaozaliwa na ugonjwa huo.

Ameongeza kuwa katika siku za hivi karibuni Tanzania imekuwa ikipiga hatua chanya katika kuimarisha masuala mbalimbali ya afya za wananchi wake na kwamba ni azma ya Marekani kuona kuwa ugonjwa wa seli mundo unapata tiba.

Kwa upande wake Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi amesema utafiti na hatimae tiba ya maradhi hayo ya seli mundu kwa kiasi kikubwa itainufaisha Tanzania kutokana na kushika nafasi ya tatu katika Bara la Afrika na ya nne duniani kwa kuwa na wagonjwa wengi wa seli Mundu.

Ameongeza kuwa Tanzania na Marekani zitashirikiana katika kufundisha na kujengeana uwezo wa namna ya kupambana na maradhi ya seli mundu lakini pia kutafuta fedha zitakazowezesha upatikanaji wa dawa ya seli mundu kutokana na ukweli kuwa dawa za ugonjwa huo kwa Tanzania ni miongoni mwa dawa muhimu yaani essential drugs ili iweze kuwafikia wananchi wengi na kwa bei nafuu.

Amezitaja Nchi zilizo na idadi ya watoto wengi wanaozaliwa na ugonjwa wa seli mundu ambapo kwa Afrika Tanzania ni ya tatu baada ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Nigeria nay a nne duniani baada ya India.
Source : http://foreigntanzania.blogspot.com/2019/09/tanzania-kunufaika-na-dola-za.html?m=1
 
Tuesday, September 24, 2019
PROF. KABUDI AMUWAKILISHA RAIS DKT. JOHN POMBE MAGUFULI UNGA
Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba

Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akifuatilia Mkutano wa viongozi wa ngazi ya juu kuhusu upatikanaji wa huduma za afya kwa wote ambao unafanyika sambamba na mkutano wa 74 wa Baraza kuu la Umoja wa Mataifa New York, Marekani.
Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiwa katika Mkutano wa viongozi wa ngazi ya juu kuhusu upatikanaji wa huduma za afya kwa wote ambao unafanyika sambamba na mkutano wa 74 wa Baraza kuu la Umoja wa Mataifa New York, Marekani.
Baadhi ya wajumbe wanaoshiriki katika Mkutano wa viongozi wa ngazi ya juu kuhusu upatikanaji wa huduma za afya kwa wote ambao unafanyika sambamba na mkutano wa 74 wa Baraza kuu la Umoja wa Mataifa New York, Marekani. Katika Mkutano huo Tanzania inawakilishwa na Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb)
source : http://foreigntanzania.blogspot.com/2019/09/prof-kabudi-amuwakilisha-rais-dkt-john.html?m=1
 
September 26, 2019
New York UN HQ

Waziri Kabudi kuhutubia kikao cha 74 Baraza Kuu La Umoja Wa Mataifa (UN GENERAL ASSEMBLY - UNGA 74)

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Palamagamba Kabudi anatarajiwa kesho 27 Sept 2019 kuhutubia kwenye mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa unaoendelea nchini Marekani. Amefanya mahojiano na Ivona Kamuntu kuzungumzia ajenda atakayokwenda kuizungumzia katika Kikao Cha Baraza Kuu la 74 na shughuli zingine alizofanya tangu awasili jijini New York Marekani mwezi huu September 2019 kuiwakilisha Tanzania na kuelezea ushawishi na nafasi ya Tanzania kimataifa



Source: Azam TV
 
Prof. Palamagamba John Kabudi na story zake nyingi kuhusu masuala ya kimataifa pia kuhusu Julius Nyerere. Palamagamba Kabudi pia aliwahi kuwa mwandishi wa habari .

Hivyo kolamu / column ya kuzungumzia mapito yake toka zama hizo mpaka sasa hivi itakuwa nafasi murua kuangazia habari motomoto hususan za nafasi yake kama waziri katika serikali.

Leo Azungumzia nafasi ya Tanzania katika dunia na ushawishi wake na kwenda mbali zaidi Prof. Palamagamba Kabudi anafananisha nafasi ya Tanzania ni kama 'nyonga' ya Afrika ktk masuala ya kimataifa.

Source : Zanzibar Ni Kwetu



!
!
Huyu Profesa Ametokea Jalalani
 
Afadhali prof kabudi kuliko bwana yule
Shida ya huyu bwana ni kutokuzingatia jambo linalojadiliwa. Yeye kila mahali anaongelea historia tu.

China aliulizwa, 'what do you offer Chinese investors if they come to your country?'. Akaanza kuelezea kuwa Mwalimu Nyerere na Mao walikuwa marafiki, na yeye amekuja ... to cement that relationship.

Viongozi wa mataifa mengine walikuwa straight forward wakielezea vivutio mbalimbali ikiwa ni pamoja na mapunguzo ya kodi kwenye capital goods, VAT, etc.
 
2 Sep 2018
Seattle, the Pacific NorthWest USA

Prof. Palamagamba Kabudi akizungumza na Watanzania wanaoishi Ughaibuni katika Maendeleo ya Kijamii na Uchumi. Hotuba hiyo iliwasisimua watu wengi ktk diaspora na kuleta mjadala mpana JamiiForums worldwide.

Prof. Kabudi anakumbuka wanafunzi wenzake ktk darasa lao Chuo Kikuu cha UDSM limetoa watu 'mahiri' siyo yeye tu bali Balozi Wilson Masilingi, Dr. Harrison Mwakyembe, Major General Rwegasira mstaafu Judge Advocat jeshini , pia majaji 7 kati ya hao wako mahakama ya rufaa ya Tanzania

Mmoja wa wana -Diaspora Bw. Deus Rugemalira kwa kumnukuu maoni yake:

'' Hotuba hii ya Prof. Palamagamba Kabudi inafumbua macho ya wengi. Inatoa mwanga (walau kwa ufupi), kama Taifa
1. Wapi tumetoka,
2. Tumetoka vipi,
3. Wapi tumefika na changamoto zake
4. Wapi tunaenda.
Tusipoyajua Haya hatuwezi kujitambua na hatuwezi kuendelea. Ningependa kuona inachapishwa hata gazetini (kama ilivyo) ili wasio na namna ya kuiona, basi wakaisome".
Hotuba zake huwa hazina content yoyote ya maana kwa global current environment.

Yeye kila mahali utasikia, 'niwaambie tulikotoka', so what. Katika Dunia ya leo hakuna mjinga wa kukupa wewe chochote eti kwa sababu ya historia.

Kila mara Kabudi kuelezea tu historia huenda kunatokana na kukosa uelewa wa mambo ya wakati huu. Ili kuziba pengo hilo na ili asionekane hajui, kila mara huanza kusimulia historia hata mahali pasipohitajika.
 
Mkuu,huwa nashindwa kuelewa kwa nini Mahiga alitolewa kwenye hii wizara. Yaani huyu aliyewekwa ni hopeless kabisa,hajui diplomacy hata chembe anadhani na nchi za wenzetu wanahitaji praise songs za 'mtukufu',pathetic!!
Hotuba zake huwa hazina content yoyote ya maana kwa global current environment.

Yeye kila mahali utasikia, 'niwaambie tulikotoka', so what. Katika Dunia ya leo hakuna mjinga wa kukupa wewe chochote eti kwa sababu ya historia.

Kila mara Kabudi kuelezea tu historia huenda kunatokana na kukosa uelewa wa mambo ya wakati huu. Ili kuziba pengo hilo na ili asionekane hajui, kila mara huanza kusimulia historia hata mahali pasipohitajika.
 
4 Mar 2019
Dar-es-Salaam, Tanzania

Waziri wa Mambo ya Nje ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof Palamagamba Kabudi amewataka Watanzania kuwa wazalendo na nchi yao na kusema Tanzania hivi sasa sio nchi ya kusemwa na kudhihakiwa.


Source: Azam TV

Uzalendo ni kusimama kwa ajili ya nchi yako na siyo kwa ajili ya Rais aliye madarakani. Prof Kabudi ni mpotoshaji
 
Prof. Palamagamba Kabudi atoboa siri ya kimbilio lake pindi ajionapo dhaifu ili aweze kuinuka tena kuendelea 'kupambana' kama askari yule shujaa wa vita ya pili ya dunia WWII (1939 - 1945)


Muulize kwanza kwa nini alijidhalilisha kwa kusajiliwa kama Wakili wa Mahakama Kuu kupitia 'viti maalum'

Hajawahi kufanya mtihani wa Mawakili au kwa mfumo wa zamani au kwa mfumo wa sasa wa Law School. Aliogopa kupigwa "supplementary" na Maprofesa wa kiukweli.

Kama anabisha akupe ushahidi uulete hapa
 
Prof. Palamagamba John Kabudi na story zake nyingi kuhusu masuala ya kimataifa pia kuhusu Julius Nyerere. Palamagamba Kabudi pia aliwahi kuwa mwandishi wa habari .

Hivyo kolamu / column ya kuzungumzia mapito yake toka zama hizo mpaka sasa hivi itakuwa nafasi murua kuangazia habari motomoto hususan za nafasi yake kama waziri katika serikali.

Leo Azungumzia nafasi ya Tanzania katika dunia na ushawishi wake na kwenda mbali zaidi Prof. Palamagamba Kabudi anafananisha nafasi ya Tanzania ni kama 'nyonga' ya Afrika ktk masuala ya kimataifa.

Source : Zanzibar Ni Kwetu

Huyu Prof Kabudi naye yupo kwenye orodha ya Dr Vicensia Shule ya wale Lecturers wa UDSM wa "marks for sex". Nakujulisha tu ulielewe, siyo kukaa hapa mnapambana bure.
 
Hotuba zake huwa hazina content yoyote ya maana kwa global current environment.

Yeye kila mahali utasikia, 'niwaambie tulikotoka', so what. Katika Dunia ya leo hakuna mjinga wa kukupa wewe chochote eti kwa sababu ya historia.

Kila mara Kabudi kuelezea tu historia huenda kunatokana na kukosa uelewa wa mambo ya wakati huu. Ili kuziba pengo hilo na ili asionekane hajui, kila mara huanza kusimulia historia hata mahali pasipohitajika.

Bams,
Mrejesho wako una kweli , natumai Prof. Palamagamba atausoma na kuutumia kujisahihisha maana dhamana ya kuiwakilisha nchi kimataifa ni kubwa sana.
 
Prof. Dr. John Kabudi, Ph.D. talks on the role of strategic communication, folktales, folk - media. A former journalist himself and board member of Nation Media Group NMG.

Source : American University of Sovereign Nations
Dr. Paul White : Jungle Doctor Operates Australian missionary doctor in Tanzania
🚮🚮🚮🚮🚮🚮🚮🚮
 
UN: Asante Tanzania kwa ulinzi wa amani
image1024x768.jpg

Picha ya UN/ Evan Schneider
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres (kulia) na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba John Kabudi baada ya mazungumzo yao jijini New York, Marekani.

27 Septemba 2019
Amani na Usalama
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa aendelea kuwa na mazungumzo na viongozi wanaowakilisha nchi zao kwenye mjadala mkuu wa UNGA74 na miongoni mwao ni kutoka Tanzania na Burundi.

Mjadala mkuu wa mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA74 ukiendelea kwenye makao makuu ya umoja huo jijini New York, Marekani, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amekuwa na mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba John Kabudi ambapo wamejadili masuala mbalimbali yanayohusu pande mbili hizo.

Taarifa ya msemaji wa Umoja wa Mataifa iliyotolewa New York, alhamisi usiku imesema kuwa Guterres na Kabudi wamejadili hali inavyoendelea kwenye ukanda wa Maziwa Makuu ikiwemo Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC.

Katibu Mkuu ameishukuru Tanzania kwa mchango wake wa kipekee kwenye ulinzi wa amani na kusisitiza utayari wa Umoja wa Mataifa wa kusaidia juhudi za kitaifa za kukabiliana na misimamo mikali.
Source : https://news.un.org/sw/story/2019/09/1069402
 
Back
Top Bottom