Story: Graduates

Story: Graduates

Hakudhamiria?? Dhamira ni nn??

"The smartest one" kwa sababu alitumia hela alizopata kwa kujishusha hadhi yake na familia yake kufungulia saloon, haya bhana mi ngoja nii-enjoy story nipite zangu
Tunaongelea kwenye kua mke, nadhani hoja yako ilikua hapo nami nimeijibia hapo, kuhusu alipita kona gani za kimaisha hayo yake mwenyewe Sarah, tutakutana siku ya mwisho na Ile hukumu kuu broo, Kama ipo
 
LEAH:

Huyu binti nitamsimulia mimi story yake maana hatupo nae tena, :Rest Easy beautifully...gone too soon'....

TONY akisimulia...

Nilimfahamu Leah siku ya udahili wa chuo, alikua amekaa chini kinyonge, mie tena na watoto wazuri , nikamfata nikamuuliza mbona kinyonge mama, akanambia hajisikii poa, na hapo bado hajafanya usajiri, nikiangali hiyo foleni sio poa, maana Kuna watu wa udoso , sijui mawadern , sijui adminstration , sijui wahasibu yaani tafrani, wote hao umalizane nao ndio upewe room, ikabidi niende nikaongee na viongozi wa udoso kwamba pana mwanafunzi anaumwa na hajasajili , yule kiongozi alikua na utu akaja akanisikiliza, akamchua Leah akaenda msajilia...

Alipomaliza kule ndani akaja kunishukuru akaomba namba angu, mie tena sikuvunga...baadae tukaja kua marafiki sana, katika huo urafiki nikaja kugundua kua Leah anaishi na virusi vya Ukimwi, alinambia baada ya kuona namsumbua sana, alinambia tu kwa upendo kua makini Tony pana mabinti wengi tu hapa tuliokuja kwa udhamini wa Mama Salma foundation, sio rahisi kuwatambua kwaio kua makini. Nilipata na hofu maana kwa ule uzuri wa Leah mbona angetaka kuusambaza angetuua wengi.

Leah alikua mrembo jamani daaah, Kuna mda unalaumu maradhi ila unakua hamna namna, nachomsifia Leah alijitunza sana, nilijaribu kumdodosa jinsi alipata maambukizi akanambia kua alizaliwa na hiyo hali, aliupata toka tumboni kwa mama, I felt sorry for her, na hio ikafanya awe rafiki angu sana, Leah alikua ananiasa mara kwa mara kuhusu tabia zangu za kupenda watoto wazuri, nadhani Ile story ya Leah ilichangia sana kua makini na kutouza mechi.

Maisha ya chuo kwa Leah hayakua na mambo mengi sana, alikua ni mfano wa binti anaejitambua sana, alikua anasali mnooo, anasoma kwa juhudi , niliumia tu safari yake haikua ndefu. Angalau Mungu angempa nafasi ya kufurahia juhudi yake ya kusoma. Alikuja kupata mwenza ambae alikua na maambukizi kama yeye, walifunga ndoa punde tu baada ya kumaliza chuo.

Miaka miwili baada ya kumaliza chuo Warda ananipigia simu ananambia Leah amefariki, Ile taarifa ilikua ngumu sana kuipokea, yule binti alikua na juhudi ya kusaka maisha, alikua anafanya biashara mtandaoni tangu tukiwa chuo, anaagiza vitu dar kimtandao anawauzia wanafunzi wenzie na watu wengine mtaani, she was smart and very hard working. Mungu alimchukua mapema mnoo hakumuacha afurahie matunda ya juhudi yake.

Leah Kama angeamua kuingia kwenye mfumo wa Dullah alikua anapata soko sana, she was beautifully indeed, ila alichagua kujiheshimu, hakutaka kuambukiza wengine, kwangu anabaki kua shujaa sana.

Tulimzika Leah nyumbani kwao Morogoro, Ile siku ilinifanya nijitafakari sana, kuna nyimbo zinaimbwa kipindi cha msiba unaweza sema naokoka leo, wale kinamama siijui wanakua wamejipanga kabisa kua tutaanza na wimbo huu tutamalizia na huu, nyimbo zinachoma hadi moyoni. Nikamwambia Dullah nikitoka hapa natafuta kanisa lilipo ndugu angu, Dullah alinicheka balaa ...tukampumzisha Leah na maisha mengine yakaendelea.
 
DULLAH:

Naona kama nimetajwa sana na hawa ndugu zangu, kuna mtu hajanizungumzia kweli, like am the monster eeeh, maisha magumu ukiyapitia yanakupa usugu na ujasiri, kulelewa na mama wa kambo halafu mzee haeleweki, kutwa kushinda kwenye pombe ' you have to toughen up'...nilikua na majukumu ya kulea wadogo zangu nikiwa mdogo sana, nilimtandika stuli yule mama wa kambo ikapelekea akimbie hakurudi tena, nilikamatwa nikawekwa ndani kwa siku saba, kwa msaada wa mwalimu mkuu nikafanikiwa kutoka sero.

Mwalimu mkuu alikua ananipenda sana, alinisaidia kuniweka sawa nikamaliza shule ya msingi. Kwa kuunga unga nikafanikiwa kumaliza sekondari na kuingia chuo, nimeanza kupiga dili chafu tangu nipo kidato cha pili, nimeuza sana mirungi na kuisafirisha hadi nchi jirani, kuna njia za panya unapita unatokea Kenya, nimesafirisha sana abiria wanaotaka kuvuka boda kienyeji kwa njia ya baiskeli, wilaya yetu ilikua inapakana na mpaka wa Kenya na Tanzania.

Kwahiyo mi polisi nimekimbizana nao sana, hadi naingia chuo wadogo zangu nilikua nimeshawasogeza kielimu, sasa unategemea nikae kizembe kama Tony, nina raha gani kwa mfano, ilibidi nipambane kutimiza malengo yangu, halafu wale watoto wa kike mi sikuwateka bwana, si fursa tu ile mi niliwasogeza karibu na wateja wao.

Kitu ambacho hamjafahamu hadi sasa, katika maisha yangu nilimpenda mwanamke mmoja tu, Warda. Ile kutaka kumuunganisha kwa mfumo wangu ni katika kumpima tu kama na yeye ana tamaa au vipi, Warda proved me wrong...that girl alikua anajiheshimu sana. Nilikua nafahamu kua Warda anapitia maisha magumu kiasi cha kutaka kuahirisha mwaka wakati wa kuingia mwaka wa pili, ila nikawaza huyu akiachia hatomudu kumaliza maana atasimishiwa mkopo, na kuja kufatilia wamrudishie tena itasumbua sana.

Nikamwambia Ton nitalipa Ada ya Warda iyo asilimia 20 kwa miaka hii miwili iliyobaki, maana alipata mkopo asilimia 80...yaani laki mbili ilikua inamkalisha Warda nyumbani daaah, ila nikampa sharti ajifanye yeye ndio anamsaidia, Warda hajawahi kunikubali kabisa, na hizi dhambi zangu ndio kabisaaaa.

Kwahiyo nilisimamia elimu ya Warda wapendwa, hivi hicho kigezo hakiwezi nifikisha mbinguni kweli? yule mtoto alinimaliza alipoamua kufanya biashara, nilimpa big up sana, imagine pisi kama ile inapambana kwenye daladala na fuko lake la mikate na masoseji, kweli daaah.

Hakuna siku niliumia kama siku ambayo Warda aliolewa, only Tony knew how much I was in love with that woman...Tony akanambia broo mwambie Warda kua ulimsaidia chuo na sio mimi, nikamwambia acha haina maana, nilitaka tu aone umuhimu wangu kwa namna nyingine na sio kwa sababu nilimsaidia, huyu mwanamke hakuwahi nipenda hata robo. Nachukulia tu Kama sadaka kwa mtu alie na uhitaji, and I'm glad nilifanikisha sehemu ya mafanikio yake, kuna karoho fulani ivi kakishetani kakawa kananiambia nimvizie bwana harusi akiingia maliwato nimkabe afie huko, yaani yule boya ndio anaenda kula ule utam daaah.
 
SARAH:

Nilikua najua madhara ya njia niliyochagua kupita, ila kuna mda maisha hayakupi kuchagua sana, kuishi na baba wa kambo ambae anakuingilia na mama yupo anaona na hakutetei inafika mahala unaona tupu yako ni kama bidhaa tuu, imagine mama mzazi anakwambia Sarah mwanangu tufanye kila liwezekanalo huyu baba afurahi, akitufukuza tunaenda wapi? kwaio kuuza mwili sijaanza jana wala juzi, sikua napenda ila mazingira yanakufanya uone haramu ni halali.

Nilipofika kidato cha pili mama alinipeleka kwa kungwi bi Sandra, huko nilifundishwa kila aina ya somo kuhusu kumuhudumia mwanaume, kwenye hiyo idara nikawa nimekomaa. Mama akaanza kuniuza kwa wanaume mbalimbali, sikua mrembo lakini umri ulinibeba, si unajua wanaume wanapenda vitoto vidogo, baba wa kambo akisafiri mama ananiuza kwa wanaume mbalimbali.

Ambacho nimejaaliwa ni uwezo mkubwa darasani,nikasema nitasoma nijikomboe, hata kama nitafanya ufuska basi iwe kwa manufaa yangu na sio kulipa madeni ya mama yasiyoisha, hadi hapo mama ameshanitoa mimba tatu, sina nilichobakisha ,ilikua afe kipa afe beki lazma nifanikiwe.

Nilipambana kujiweka kwa wabunge holaaa, nina hiyo sura sasa ya kuwatega, kuna lecturer nilimtega akaishia kunila na kua ananipa viofa vya hapa na pale, sikuridhika, I needed something big...katika kufatilia wala bata wenzangu ndio nikakutana na kina Tony, kuna ile bond inatokeaga tu mkiwa mnafanana hobby, kupitia Tony nikamfahamu Dullah, 'there he is, my dream boat...'

Ndoa ni kitu sijawahi fikiria kabisa, kwanza nani wa kunioa Sarah mie, yule mheshimiwa mwanzo nilijua anatania, heeee...kumbe yuko serious, hadi nawaalika kina Tony kwenye harusi wananiuliza dogo upo serious unataka kuolewa, usiende kutuaibisha hukoo...

Katika vitu sikuvihitaji na nilipambana visitokee ni kurudi tena nyumbani, maana ningemaliza shule kiboya ilikua narudi tena kwa yule bazazi...I said never on Earth, nitarudi ndani ya jeneza sio nikiwa natembea na miguu yangu miwili, kwaio hio ilikua my last card, sikufanya masihara, nilimsumbua yule baba anitafutie ajira , kupitia connections zake nikapata ajira bank, niliwekeza kama sina akili nzuri, Dullah anajua sana biashara alinisaidia sana ni wapi nifanye investment nitoke.

Nimemsamhe mama angu, na Namuombea heri, nilijaribu kumwambia aachane na yule baba nimnunulie nyumba , alikataa, kwahiyo alichagua yale maisha ya kunyanyasika. Nilishiriki mazishi ya Leah na nikapata fursa ya kuonana na ndugu zangu hawa watano kwangu hawa mimi ni familia...maisha mafupi sana, najua sina mwanzo mema ila napambana kua na mwisho bora, nasali sana na natoa sana sadaka kwa yatima na wale wenye uhitaji....

Naitwa Sarah...na hii ndio story yangu...
 
TONY:

Sababu mi ndio nilianza acha nifunge dimba, katika watu walinishangaza ni Sarah, she is a woman of steel, maisha aliyopitia ya kua abused na baba ake mlezi ata a young age yalikua yanamfanya awe nunda sana, kitu pekee nilichojaaliwa na mwenye enzi ni kuishi na kila mtu jinsi alivyo, ili mradi hayo unayoyafanya hayaniathiri ...go with it...

Sarah alisimama katika ndoa yake, she is now a mother to a beautifully baby girl, she is very protective kwa mwanae, na najua atakua mama bora sana...

Warda anaishi Mbeya na mumewe, she is doing okey, nilikuja kumwambia kua aliekua anakulipia zile ada ni Dullah na sio mimi. Alimpigia Dullah kumshukuru na walau wamekua marafiki, maana Leah hakutaga kabisa ukaribu na dullah.

John kisomo huyu mwanangu daah, kwa sasa ni lecturer chuo fulani hivi Iringa, mtu makini sana, ana watoto wawili pia, kaoa kabinti karembo kanyalukolo , wako poa sana...

Dullah alifanikiwa kufungua garage kubwa pale mjini, akawa anaitumia kama yard ya kuhifadhi magendo yake, kipindi cha utawala wa Jiwe Kuna mamwela wapenda sifa walimuotea akasota jela kwa zaidi ya miaka mitatu, kwa sasa ametoka ila ameacha zile mishe za magendo , anatafuta kihalali, ila Dullah hatabiriki sana ,usishangae siku ukisikia jina lake Al Jazeera kalipua jengo huko Pakistan kisa kapewa dili na Taleban...

Mimi nimeoa, nimekua mkubwa jamani, niko na mtoto mkale nyumbani , kanizalia watoto wawili, mmoja wa kike nimemuita Leah...

This was my crew, my family , my people...

Wasalaaam,

Just Nana...
 
Story zako nzuri, I want to make a film out of these stories, nina ruhusa yako🤣
 
...nimependa upambanaji wa "john kisomo"... Wachache wanaweza
 
...nimependa upambanaji wa "john kisomo"... Wachache wanaweza
 
Vijana ya udom MNA kitu Msipuuzwe,,,Mtafika mbali!!
 
Tofauti yangu na john kisomo mimi nilikuwa na t-shirt tatu 😅 miaka minne yote
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom