Storm water has the right of way, Maji ya mvua yana haki zote kupita!

Lole Gwakisa

JF-Expert Member
Nov 5, 2008
4,728
2,259
Kama kuna funzo tunalolipata kila mvua kubwa tunapoipata ni hili la maji ya mvua.

Tatizo kubwa huwa hatujifunzi somo hilo.
Tuna vichwa vigumu!

Mimi ni mhandisi, na najua fika kuwa Water has the right of way.
Maji ya mvua hatuna namna, tuyapishe tu.

Serikali haina mamlaka ya kushughulikia kikamilifu maji na mitaro ya maji ya mvua.
Na hii ni kuanzia kutunza mapito ya asili kisheria, kudesign mapito hayo na kuyafanyia matengenezo.

Kwa sasa mapito ya maji ya mvua hayalindwi kisheria.
Hakuna mamlaka ya kuyashughulikia kama TANROADS, TARURA au hata kwenye Halmashauri zetu.

Kitengo kidogo kwa mfano DSM chenye mhandisi mmoja au wawili kwenye taasisi zetu zote is all we can do.

Tunajenga mabarabara mazuri kwa gharama kubwa lakini ikija mvua kubwa, maji yanazoa kila kitu bila kuacha ushahidi.

TUJIFUNZE, TUJIFUNZE, TUJIFUNZE.
Water has the right of way!
 
Nakubaliana kabisa mhandisi.
We must change our urban management way of thinking.

Na bado masika yaja bada ya miezi 4 au mitano.
 
Mkuu

ku design open channels, undeground piping, storm water storage tanks na robust storm water control facilities zinaweza kuzuia tatizo

hydrology data zinapikwa na haziko realistic

unawezaje kwa mfano ku design na kujenga barabara bila mitaro?? upuuzi huu

tuache ujenzi wa barabara kabisa, tuanze na njia za maji, kisha ndio zije barabara, ni logical..common sense haihitaji uwe injinia kama wewe na mimi

kuna uzembe mahali, donors wanatoa hela kila siku kuna miradi wanaita majina mazuri DMDP, TSCP, .n.k aibu hii

honestly siyo wanasiasa hapa ni wahandisi

unless aje mhandisi kutoka serikalini, tanroads au tarura aseme...inakuwaje unajenga barabara kiwango cha lami ili hali haujui maji yataenda wapi?

angalia kibarabara cha ccbrt ..lami ile, maji hakuna kwa kwenda ,wakati ingekuwa rahisi yaingilie ccbrt kama undeground pipes na hivyo hivyo yaende baharini

wanadai hela hakuna, hela?? kwa nini phase zilizopita tusingekomaa kwenye kuyaelekeza maji yanakotakiwa kwenda!?? kisha ndio tujenge barabara....ni akili gani inatumika kujenga barabara 1km sh 800m ambayo mvua ikija inaharibu? au kuleta premature maintenances issues? Makonda akiwafokea anaonekana mbaya kweli??


ku design maji kwa uweledi wake you " GIVE RIGHT OF WAY"
 
Mkuu

ku design open channels, undeground piping, storm water storage tanks na robust storm water control facilities zinaweza kuzuia tatizo

hydrology data zinapikwa na haziko realistic

unawezaje kwa mfano ku design na kujenga barabara bila mitaro?? upuuzi huu

tuache ujenzi wa barabara kabisa, tuanze na njia za maji, kisha ndio zije barabara, ni logical..common sense haihitaji uwe injinia kama wewe na mimi

kuna uzembe mahali, donors wanatoa hela kila siku kuna miradi wanaita majina mazuri DMDP, TSCP, .n.k aibu hii

honestly siyo wanasiasa hapa ni wahandisi

unless aje mhandisi kutoka serikalini, tanroads au tarura aseme...inakuwaje unajenga barabara kiwango cha lami ili hali haujui maji yataenda wapi?

angalia kibarabara cha ccbrt ..lami ile, maji hakuna kwa kwenda ,wakati ingekuwa rahisi yaingilie ccbrt kama undeground pipes na hivyo hivyo yaende baharini

wanadai hela hakuna, hela?? kwa nini phase zilizopita tusingekomaa kwenye kuyaelekeza maji yanakotakiwa kwenda!?? kisha ndio tujenge barabara....ni akili gani inatumika kujenga barabara 1km sh 800m ambayo mvua ikija inaharibu? au kuleta premature maintenances issues? Makonda akiwafokea anaonekana mbaya kweli??


ku design maji kwa uweledi wake you " GIVE RIGHT OF WAY"
Kweli kabisa, wahandisi wanalo lakini bado kila mtu anatupia mpira mwingine.
 
Mkuu

ku design open channels, undeground piping, storm water storage tanks na robust storm water control facilities zinaweza kuzuia tatizo

hydrology data zinapikwa na haziko realistic

unawezaje kwa mfano ku design na kujenga barabara bila mitaro?? upuuzi huu

tuache ujenzi wa barabara kabisa, tuanze na njia za maji, kisha ndio zije barabara, ni logical..common sense haihitaji uwe injinia kama wewe na mimi

kuna uzembe mahali, donors wanatoa hela kila siku kuna miradi wanaita majina mazuri DMDP, TSCP, .n.k aibu hii

honestly siyo wanasiasa hapa ni wahandisi

unless aje mhandisi kutoka serikalini, tanroads au tarura aseme...inakuwaje unajenga barabara kiwango cha lami ili hali haujui maji yataenda wapi?

angalia kibarabara cha ccbrt ..lami ile, maji hakuna kwa kwenda ,wakati ingekuwa rahisi yaingilie ccbrt kama undeground pipes na hivyo hivyo yaende baharini

wanadai hela hakuna, hela?? kwa nini phase zilizopita tusingekomaa kwenye kuyaelekeza maji yanakotakiwa kwenda!?? kisha ndio tujenge barabara....ni akili gani inatumika kujenga barabara 1km sh 800m ambayo mvua ikija inaharibu? au kuleta premature maintenances issues? Makonda akiwafokea anaonekana mbaya kweli??


ku design maji kwa uweledi wake you " GIVE RIGHT OF WAY"

Nakubaliana mkuu, kwamba wahandisi wana play part katika blame game.
Na wangekomaa huu upuuzi wa maji kukata barabara jijini na kwingineko isingetokea.
Hako kapicha hapo juu, ni wazi hakuna daraja, kuna ka culvert, ikija mvua kama ya jana hiyo barabara nzuri inabebwa.

Lakini argument yangu ni katika STORM WATER POLICY.
Mitaro asili ya maji kwanza itambulike kisheria , kama ilivyo katika Roadways Ordnance.

Katika hili hata designer wa barabara atalazimika kudesign si tu culvert tudogo bali daraja kamili lenye kufikiria miaka 100 au Zaidi mbele.
 
Kwenye mada kama hizi wale jamaa wa mihemuko hutawakuta.
Lkini naamini watu kama Mkuu wa Mkoa Makonda ana nafasinzuri kuliweka sawasawa suala hili, maana yeye kifikra na kiutendaji anaenda against the grain lakini matokeo yake ni chanya.
 
Hivi pale Jangwani kwa mfano ilishindikana nini kunyanyua ile barabara moja kwa moja kutoka pale Mapipa hadi Mataa ya Fire? Engineer Mleta Mada; hata hili nalo mlishindwa kushauri? Yaani mkaamua kabisa kuipitisha barabara "baharini"? Kwamba leo "manyunyu" ya masaa 36 tu mnaingiza vikosi vya traffic pale ku-divert magari? Hivi siku Catrina ikibadili uelekeo japo kwa masaa matatu itakuwaje? Kabisa na Kambi na Karakana Kuu ya mradi mkaidumbukiza "baharini"! Mlichemka vibaya sana pale!
 
Hivi pale Jangwani kwa mfano ilishindikana nini kunyanyua ile barabara moja kwa moja kutoka pale Mapipa hadi Mataa ya Fire? Engineer Mleta Mada; hata hili nalo mlishindwa kushauri? Yaani mkaamua kabisa kuipitisha barabara "baharini"? Kwamba leo "manyunyu" ya masaa 36 tu mnaingiza vikosi vya traffic pale ku-divert magari? Hivi siku Catrina ikibadili uelekeo japo kwa masaa matatu itakuwaje? Kabisa na Kambi na Karakana Kuu ya mradi mkaidumbukiza "baharini"! Mlichemka vibaya sana pale!
Sijui kama mtoa mada utalaam wake wa kihandisi ni tofauti na mainjinia walioko Wizara ya Ujenzi au TANROADS au kwenye MAJIJI/MANISPAA na Halamashauri za miji na Vijiji! Na kama utalaam wao ni sawa, tatizo liko wapi? Mawazo yao hupuuzwa na watawala; au mawazo yao hushindwa kutekelezwa kwa sababu ya ukosefu wa SERA; au kwa sababu ya ukosefu wa fedha?
Na mnajisikiaje pale ambapo taaluma yenu inaposhindwa kutoa matokeo sahihi kiasi cha kufanya nchi kupiga mark time?
 
Sijui kama mtoa mada utalaam wake wa kihandisi ni tofauti na mainjinia walioko Wizara ya Ujenzi au TANROADS au kwenye MAJIJI/MANISPAA na Halamashauri za miji na Vijiji! Na kama utalaam wao ni sawa, tatizo liko wapi? Mawazo yao hupuuzwa na watawala; au mawazo yao hushindwa kutekelezwa kwa sababu ya ukosefu wa SERA; au kwa sababu ya ukosefu wa fedha?
Na mnajisikiaje pale ambapo taaluma yenu inaposhindwa kutoa matokeo sahihi kiasi cha kufanya nchi kupiga mark time?
Inasikitisha sana Mkuu. Halafu Mwenyezi Mungu alivyopatengeneza vizuri pale Jangwani; mwinuko huku na mwinuko kule; hapakuwa hata na gharama kubwa. Ilikuwa kupanga makalavati ya diameter kubwa na kumwaga kifusi na hatimaye lami. Very easy.
 
Hivi pale Jangwani kwa mfano ilishindikana nini kunyanyua ile barabara moja kwa moja kutoka pale Mapipa hadi Mataa ya Fire? Engineer Mleta Mada; hata hili nalo mlishindwa kushauri? Yaani mkaamua kabisa kuipitisha barabara "baharini"? Kwamba leo "manyunyu" ya masaa 36 tu mnaingiza vikosi vya traffic pale ku-divert magari? Hivi siku Catrina ikibadili uelekeo japo kwa masaa matatu itakuwaje? Kabisa na Kambi na Karakana Kuu ya mradi mkaidumbukiza "baharini"! Mlichemka vibaya sana pale!
Mkuu unavosema ni sawa sawa na kufikiri mradi wewe ni waziri basi kila tatizo ni lako.
La mapolisi lako, la maji lako, la maji machafu lako na la hali ya hewa lako!!!!

Hata hao wahandisi walio kaika sehemu hizo kuna taratibu za kufuata.
Hata hivyo ni kweli kuna uzembe mkubwa katika kubuni,kushauri na hata kufanya usanifu(design)

Suala la barabara ya Jangwani halihitaji kuwa na degree ya uhandisi kuona kuwa catchment area(sehemu yote inayohusika kukusanya mmaji ya mvua), inazidi kutema maji mengi kutokana na watu kujenga nyumba .
Hivyo maji hayaingii ardhini.

Haihitaji degree kwa hata hao watu wa DART kujua kuwa sehemu waliyoweka karakana ni hatarishi kutokana na kujaa maji.
Nakubaliana nawe kwamba wakati mwingine hawa wahandisi tulionao hawatumii akili sana pamoja na wao kujua uzoefu wa mvua zetu kw mfano Dar es saaam.
 
Inasikitisha sana Mkuu. Halafu Mwenyezi Mungu alivyopatengeneza vizuri pale Jangwani; mwinuko huku na mwinuko kule; hapakuwa hata na gharama kubwa. Ilikuwa kupanga makalavati ya diameter kubwa na kumwaga kifusi na hatimaye lami. Very easy.
Inafaa wale waliosimamia usanifu(design) wajibu haya maswali.
 
Hivi pale Jangwani kwa mfano ilishindikana nini kunyanyua ile barabara moja kwa moja kutoka pale Mapipa hadi Mataa ya Fire? Engineer Mleta Mada; hata hili nalo mlishindwa kushauri? Yaani mkaamua kabisa kuipitisha barabara "baharini"? Kwamba leo "manyunyu" ya masaa 36 tu mnaingiza vikosi vya traffic pale ku-divert magari? Hivi siku Catrina ikibadili uelekeo japo kwa masaa matatu itakuwaje? Kabisa na Kambi na Karakana Kuu ya mradi mkaidumbukiza "baharini"! Mlichemka vibaya sana pale!
Ni majanga!
 
wahandisi tutaumiza kichwa bure, sisi kama engineers huwa tuna mawazo mazuri ila shida ni pale wanasiasa wanapo hodhi michakato yooote,
myself i have been designing so many government owned infrastructure lakini vikwazo unavyokutana,inabidi useme bora liende.
 
wahandisi tutaumiza kichwa bure, sisi kama engineers huwa tuna mawazo mazuri ila shida ni pale wanasiasa wanapo hodhi michakato yooote,
myself i have been designing so many government owned infrastructure lakini vikwazo unavyokutana,inabidi useme bora liende.
Msichoke kushauri yale yaliyokaa kitaaluma zaidi, huo ndo wito wa kazi.

Maana hata wachungaji na mashehe hawaachi kuhubiri kwa vile watenda dhambi bado wanaendelea kutenda dhambi.
 
Kama kuna funzo tunalolipata kila mvua kubwa tunapoipata ni hili la maji ya mvua.

Tatizo kubwa huwa hatujifunzi somo hilo.
Tuna vichwa vigumu!

Mimi ni mhandisi, na najua fika kuwa Water has the right of way.
Maji ya mvua hatuna namna, tuyapishe tu.

Serikali haina mamlaka ya kushughulikia kikamilifu maji na mitaro ya maji ya mvua.
Na hii ni kuanzia kutunza mapito ya asili kisheria, kudesign mapito hayo na kuyafanyia matengenezo.

Kwa sasa mapito ya maji ya mvua hayalindwi kisheria.
Hakuna mamlaka ya kuyashughulikia kama TANROADS, TARURA au hata kwenye Halmashauri zetu.

Kitengo kidogo kwa mfano DSM chenye mhandisi mmoja au wawili kwenye taasisi zetu zote is all we can do.

Tunajenga mabarabara mazuri kwa gharama kubwa lakini ikija mvua kubwa, maji yanazoa kila kitu bila kuacha ushahidi.

TUJIFUNZE, TUJIFUNZE, TUJIFUNZE.
Water has the right of way!
Tatizo jingine ni watu wa mipango miji,kutoa viwanja Na Vivaldi vya ujenzi kwenye njiani Za maji.
Sasa Kwa kuwa wewe ni mwana taaluma ni vizuri mambo hayo kwenye mikutano yenu ya kitaaluma Na kikazi.
Lakini nashukuru kuona barabara zinazojengwa sasa Kama pale stand ya makumbusho, Na Kati ya bodi ya mikopo kwenda Shule ya mapambano wanajenga barabara nzuri Na drainage system
 
Back
Top Bottom