Stori ya kusisimua - Taxi

Bishop asante

Sijapenda Sammy anavyomficha mkewe kufukuzwa kazi wanaume sijui mpoje jamani mwambie ukweli mkeo hata kama unaumiza jamani
Ana uoga fulani kwa mke wake. Maybe suala la kazi anaona kama atamfanyia mke awe na mawazo. Anavyozidi kukaa kimya ndio unavyozidi kupalilia tatizo
 
kuna mafile yamechanganywa hapa
 
Wakuu nimerudi, laptop yangu imezingua lakini siyo sababu ya kuukosa uhondo wa safari hii ya kusisimua ndani ya Taxi. Tuendelee...

CC the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater Bigjahman moneytalk marybaby nipo2 ram kisukari Smart911 Madame S carbamazepine Astelia culture gal Prisoner of hope Mine eyes kuku mweus Thad hearly Shunie moneytalk Tumosa Mine eyes Kudo swahiba92 ludist Toyota escudo Clkey macson3 boga la kiangazi LEGE Smart911 Richard irakunda skfull popie Krizy Beat hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Mlenge Kacheda mjasiliamali Laki Si Pesa cocochanel kinusikwetu big jambo mludego Shupavu Kacheda mjasiliamali Mweweso Songa Heri esiankiki

Taxi - (55)

ILIPOISHIA

Sammy alimfuata yule bibi akionekana kuchangamka, akapokea lile begi dogo na ule mfuko wa plastiki, akafungua mlango wa nyuma wa gari lake na kuviweka kwenye siti. Kisha alimshika mkono yule bibi kwa upole na kumsaidia kuingia ndani ya lile gari, akaketi kwenye siti ya nyuma. Yule bibi alimtazama Sammy kwa jicho la shukrani.

“Asante sana mjukuu wangu,” yule bibi alisema huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani.

“Usijali bibi… natakiwa kuwatendea wateja wangu kwa namna ambayo ningependa mama yangu atendewe,” Sammy alisema huku akifungua mlango wa dereva, akaingia na kuketi.

SASA ENDELEA NAYO...

“Wewe ni kijana mwema… sasa unaweza kunipeleka Karakata,” yule bibi alisema huku akiachia tabasamu.

“Hakuna tatizo bibi, shilingi elfu tano tu,” Sammy alimwambia yule bibi huku akigeuza shingo yake kumtazama.

“Sawa, lakini tupitie barabara inayoelekea Mnazi Mmoja,” yule bibi alisema huku akijiegemeza kwenye siti.

“Huko tutakuwa tunazunguka sana, bibi… ipo barabara rahisi ya kupitia Mnyamani halafu Vingunguti kisha tunakwenda kutokea Karakata…”

“Sijali kama tutakuwa tunazunguka, sina haraka,” yule bibi alisema huku akiachia tabasamu.

“Lakini gharama inaweza kuwa kubwa zaidi.”

“Usijali kuhusu gharama, wewe fuata maelekezo yangu.”

Sammy alimtazama yule bibi kwa makini kupitia kioo cha katikati cha gari kinachotumika kuangalia nyuma na kushusha pumzi za ndani kwa ndani. Yule bibi alitulia tuli huku akiwa amejiegemeza kwenye siti, alionekana kuchoka sana.

“Daktari wangu ameniambia kuwa ninahitaji kufurahi zaidi ili niweze kuishi muda mrefu kidogo, vinginevyo sina muda mrefu wa kuishi,” yule bibi alimwambia Sammy huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani.

Sammy hakusema neno, alibaki kimya huku akimtupia jicho yule bibi kupitia kile kioo cha katikati cha gari kinachotumika kuangalia nyuma, alibana taya zake na kuwasha injini ya gari, akaliondoa gari lake taratibu akiingia katika barabara ya lami iliyokuwa ikienda kutokea hospitali ya Amana.

Walipita kwenye ile barabara iliyokatisha katikati ya majumba mazuri na makazi ya kisasa ya watu wenye ukwasi yaliyozungukwa na kuta zenye usalama wa uhakika. Na baada ya mwendo mfupi wa safari yao waliyafikia makutano ya barabara ile na barabara iliyoelekea Hospitali ya Amana.

Sammy alikata kona na kuingia upande wa kulia akaenda kuungana na barabara ya Uhuru katika eneo la Amana Vijana, kisha akakunja tena kuingia upande wa kushoto akiifuata barabara ya Uhuru.

Katika barabara ile ya Uhuru kulikuwa na msongamano mkubwa wa magari, hivyo safari yao ilikuwa ya taratibu. Yule bibi alikuwa hasemi kitu badala yake alikuwa amezama kwenye kutazama mandhari ya ile barabara ya Uhuru.

Ule mwendo wa wastani ulimruhusu yule bibi kuona vizuri mandhari ya nje. Alikuwa anaona vitu vikiwa vinapita mbele ya macho yake na kurudi nyuma taratibu wakati lile gari likiwa linakwenda, mara wakayapita mabanda yaliyotumika kama vyumba vya wasusi wa Kimasai.

Akiwa bado anayatazama yale mabanda ya wasusi wa Kimasai kwa makini wakaikuta barabara ya Mafao iliyokuwa ikiingia kushoto, wakaivuka na kulipita jengo refu zaidi maarufu kama Mafao House. Yule bibi alilitazama lile jengo kwa makini na kuminya midomo yake.

Baada ya safari fupi hatimaye wakalifikia jengo la ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, eneo la Ilala Boma. Yule bibi aliliangalia kwa makini lile jengo la ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam na kukohoa ili kusafisha koo lake, kisha akamuonesha Sammy jengo hilo.

“Enzi za ujana wangu nilifanya kazi hapo kama Katibu Muhtasi,” yule bibi alisema. Sammy alilitupia jicho lile jengo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam na kubaki kimya.

Muda huo walikuwa wamefika katika makutano ya barabara ya Kawawa na Uhuru kwenye taa za kuongozea magari barabarani. Bahati nzuri walimkuta askari wa usalama barabarani aliyekuwa akiruhusu magari na kuwaruhusu wapite.

Gari la Sammy likapita huku watu wakilisindikiza kwa macho yaliyoonesha kulishangaa na baadaye wakazipita daladala zilizokuwa zimesimama katika kituo cha daladala cha Karume. Kisha wakaikuta barabara ya Shaurimoyo upande wao wa kulia na kuipita, na hapo Sammy aliongeza mwendo na kuyapita majengo ya kiwanda cha bia (TBL).

Lile gari lilizidi kwenda mbele na kuvuka taa za kuongozea magari barabarani katika makutano ya barabara za Msimbazi na Uhuru, eneo la Kariakoo. Sammy aliendelea kuendesha gari kimya kimya akiifuata barabara ile ya Uhuru hadi walipozifikia taa za kuongozea magari barabarani katika makutano ya barabara za Uhuru na Lumumba.

“Endelea mbele hadi utakapofika Mtaa wa Indira Gandhi, kisha uingie kushoto kuufata mtaa huo,” yule bibi alimwambia Sammy huku akitupa macho yake nje na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.

Sammy alitii na kuendesha akizivuka taa za kuongozea magari barabarani za makutano ya barabara za Uhuru na Lumumba, akakivuka kituo cha daladala cha Mnazi Mmoja, kisha akazivuka taa nyingine za kuongozea magari barabarani katika makutano ya barabara za Uhuru na Bibi Titi Mohammed.

Baada ya mwendo mfupi hatimaye wakaufikia Mtaa wa Indira Gandhi, Sammy akakata kuingia kushoto akiufuata ule mtaa hadi mbele kidogo walipoukuta Mtaa wa Aggrey uliokatiza mbele yao.

“Umeiona hiyo hoteli hapo mbele, ni hoteli ambayo mimi na marehemu mume wangu tulikuja kwa ajili ya fungate mara tu tulipotoka kufunga ndoa,” yule bibi alimwambia Sammy huku akimwonesha kwa kidole. Sammy aliiangalia ile hoteli akiwa hajui aseme nini.

“Unaweza kusimama hapo kando?” yule bibi alimuuliza Sammy, na bila kuchelewa alisimamisha gari lake kando ya barabara ya mtaa ule. Yule bibi alibaki kimya kabisa akilitazama lile jengo la hoteli kwa kitambo kirefu.

Sammy alionekana kukerwa kidogo lakini hakuwa na namna ya kufanya. Aliwaza: kama kazi ya kuendesha teksi ilikuwa na usumbufu kiasi kile ni heri angetafuta kazi nyingine ya kufanya. Alikuwa amepatikana! Kutoka Meneja Matukio katika hoteli kubwa yenye hadhi ya nyota tano hadi kazi ya kuendesha teksi! Haiaminiki kabisa!

Alitaka amweleze ukweli yule bibi kuwa hakupendezwa na kile kilichokuwa kikiendelea na ikibidi amtake atafute gari nyingine lakini alipokumbuka maneno ya yule bibi kuwa, “daktari wake alimtaka kufurahi zaidi ili aweze kuishi muda mrefu kidogo…” alishindwa kusema chochote.

Inaendelea...
 
Taxi - (56)

Alimtupia jicho yule bibi kupitia kile kioo cha katikati cha gari kinachotumika kuangalia nyuma huku akijilaumu kukubali kumchukua, aliamua kuwa mvumilivu na hakutaka kumkera bibi wa watu. Yule bibi aliendelea kuliangalia lile jengo la hoteli kwa kitambo kirefu kisha alionekana kuridhika, akashusha pumzi ndefu.

“Ahsante sana mjukuu wangu, kwa kunikumbusha enzi za ujana wangu, nimeridhika. Sasa tunaweza kwenda Karakata,” yule bibi alisema huku akijiegemeza kwenye siti yake, akafumba macho.

Sammy alimtupia jicho yule bibi na kushusha pumzi kisha akaondoa gari lake taratibu akiendesha kimya kimya kuelekea Karakata. Aliufuata Mtaa wa Aggrey hadi alipoikuta barabara ya Bibi Titi Mohammed, akakata kuingia kushoto akiifuata ile barabara.

Safari yao iliendelea kimya kimya, muda ule yule bibi alikuwa amepitiwa na usingizi. Sammy alikwenda hadi alipoikuta barabara ya Nkrumah, akaifuata barabara ile hadi kwenye makutano ya barabara za Nkrumah, Msimbazi, Nyerere na Gerezani.

Sammy aliitazama saa yake ya mkononi na kugundua kuwa ilikuwa imekwishatimu saa sita mchana, akashusha pumzi akiifuata barabara ya Nyerere iliyokuwa na magari machache muda ule, akaongeza mwendo.

Baada ya safari ya takriban dakika arobaini walifika eneo la Jet Club, Sammy akaamua kumwamsha yule bibi na kumuuliza uelekeo wake. Yule bibi alimweleza aingie kulia na kuifuata barabara nyembamba ya vumbi iliyopita katikati ya viwanda na kwenda kutokea reli ya kati kisha akakunja kushoto akiifuata ile barabara nyembamba.

Walipovuka reli waliikuta barabara nyingine ya vumbi iliyopita mbele ya shule za Majani ya Chai na Ilala, yule bibi akamwelekeza kuwa aelekee upande wa kushoto akiifuata ile barabara na baadaye aingie upande wa kulia kabla hajayavuka majengo ya Veta Kipawa.

Aliingia akiifuata barabara nyingine nyembamba ya vumbi akayavuka majengo ya Veta kipawa yaliyokuwa upande wake wa kushoto, na baada ya safari ya takriban dakika tano yule bibi alimwonesha Sammy nyumba moja iliyokuwa mbele yao.

Ilikuwa nyumba ndogo lakini ya kisasa ikiwa imezungushiwa ukuta mfupi na ilikuwa na geti kubwa la rangi ya damu ya mzee mbele yake. Sammy alisimama mbele ya ile nyumba, kisha alifungua mlango na kushuka, akazunguka kumfungulia mlango yule bibi.

Wakati yule bibi akishuka, Sammy alishusha begi lake dogo na ule mfuko wa plastiki. Muda ule ule alijitokeza binti mmoja aliyekuwa na umri wa miaka isiyozidi ishirini, akapokea lile begi huku akimsalimia Sammy kwa adabu.

“Ubarikiwe sana kijana wangu, leo umempa bibi yako furaha isiyo na kifani, furaha itakayoniongezea siku za kuishi. Ahsante sana,” yule bibi alisema huku akifungua pochi yake, akatoa noti tatu za shilingi elfu kumi kumi na kumpa Sammy. Kisha akaanza kupiga hatua kuelekea ndani kabla Sammy hajasema chochote.

* * * * *

Saa sita mchana kwenye ukumbi mkubwa wa kisasa wa burudani wenye jukwaa la kisasa lililotazamana na viti vingi kwenye ghorofa ya saba ya jengo la kituo cha runinga, Nuru TV, kulikuwa na warembo kadhaa waonesha mitindo ya mavazi waliokuwa wakifanya mazoezi jukwaani.

Jengo lile la ghorofa saba la kituo cha Nuru TV lilimilikiwa na Madame Norah, lilikuwa katika Barabara ya Bagamoyo eneo la Makumbusho.

Ndani ya ule ukumbi Joyce alikuwa amesimama akiwatazama wale warembo jinsi walivyokuwa wakipita jukwaani kwa miondoko ya aina yake wakionesha ubunifu wake. Walikuwa katika hatua za mwisho za kufanya, mazoezi yaliyochukua takriban wiki mbili, kabla ya tukio rasmi lililopangwa kufanywa na Joyce.

Joyce alikuwa amevaa gauni refu la kitenge cha wax la mikono mirefu lililoshonwa kwa ubunifu wa hali ya juu, mtindo wa pencil dress, likiwa limedariziwa kwa nyuzi za dhahabu na kuushika mwili wake huku likilichora vyema umbo lake maridhawa.

Mkononi Joyce alikuwa ameshika picha za warembo wakiwa katika mitindo tofauti na michoro mingine mbalimbali ya mitindo ya mavazi. Joyce alikuwa makini zaidi akifuatilia mazoezi ya wale warembo pale jukwaani

Kando yake alisimama msaidizi wake, Nyaso Gilbert Nyaso aliyevalia blauzi nyepesi ya pinki na suruali ya jeans ya rangi ya bluu mpauko yenye matobo maeneo ya mapajani na iliyombana na kulichora vyema umbo lake refu maridhawa lenye tumbo dogo.

Mkononi alikuwa amevaa bangili nyingi za pembe, miwani myeusi ya jua usoni, viatu vyenye vikanyagio virefu vya mchuchumio miguuni na wigi la nywele ndefu kichwani lililomfanya aonekane mrembo hasa. Pia kulikuwa na mpiga picha mmoja aliyekuwa akipiga picha za video za mazoezi hayo kwa maelekezo ya Nyaso.

Madame Norah akiwa ameongozana na msaidizi wake, Jessica waliingia mle ukumbini na kusimama wakiwaangalia kwa makini wale warembo walivyokuwa wakifanya mazoezi. Joyce alimuona Madame Norah na kuachia tabasamu pana kisha akamfuata pale alipokuwa amesimama, walisalimiana kwa bashasha zote.

Madame Norah alifika hapo kutaka kujua maendeleo ya Joyce na ule mradi wake mkubwa na wa kwanza kufanywa na Joyce tangu aingie kwenye tasnia ya mitindo.

Madame Norah hakuwa akijua kilichokuwa kinaendelea kwenye ule mradi, hasa tangu alipomkabidhi Nyaso kuwa msaidizi wa Joyce na yeye akasafiri kwenda nchini Ghana kumuona mdogo wake Zuena, mke wa Balozi wa Tanzania nchini Ghana, Balozi Mafuru.

Ilikuwa ni safari ya ghafla iliyoibuka baada ya kukutana na Zainab, waliyepotezana miaka mingi na wasijue alikokuwa amekimbilia baada ya kutuhumiwa kwenye mauaji ya mumewe Hemed Kimaro, miaka kumi na mbili iliyokuwa imepita.

Ni baada ya safari ile ya Ghana walikokutana ndugu watatu, wakaongea na kupeana ahadi ya kuendelea kuwasiliana na kushirikiana kwa kila kitu, ndipo Madame Norah alipoanza kuhisi ile furaha iliyokuwa imetoweka miaka mingi maishani kwake ikianza kurejea.

Alikuwa mtu mwenye furaha kiasi na Joyce aliweza kubaini mara moja ingawa hakumuuliza. Madame Norah na Joyce waliongea kwa kitambo kirefu wakipeana mikakati ya namna ya kufanikisha mradi ule mkubwa wa Joyce.

Jambo ambalo Madame Norah hakulijua na aliendelea kujiuliza bila majibu ni kwamba: kwa nini aliamua kumsaidia Joyce aliyemhesabu kama mmoja wa washindani wake kwenye tasnia ya mitindo? Tena hakumsaidia tu kwa kumtafutia msaidizi, ukumbi au kulipia gharama za maandalizi, bali alifikia hadi kumpa mikakati na mbinu mbalimbali za kufanikisha mradi ambao ungekuja kuwa tishio kwake!

Inaendelea...
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…