Stephen Wassira: CUF hawaitaki Serikali ya Mapinduzi

Stephen Wassira: CUF hawaitaki Serikali ya Mapinduzi

Lakini pia cuf wanaodai serikali tatu wote ni wale wenye uraia wa oman kwa kificho hata paspoti zao za kusafiria wanamiliki za omani.

Serikali tatu haidaiwi na cuf,serikali tatu inadaiwa na wananchi waliotoa maoni yao kwenye tume ya warioba.

Uraia wa oman?alafu mnawajua na kuwaacha wawe viongozi?hii nchi imewashnda.

Mmeishiwa hoja,mara warioba kaleta maoni yake ya serikali 3,baada ya warioba kujb hicho kiloja,sasa mnasema cuf ndio wanataka serikali 3.
 
spinning za kijinga, CUF wanakubali mapinduzi na serikali ya mapinduzi na ndio maana wakawa sehemu ya serikali hio.

suali la kusema isiwekwe kwenye katiba ilikua pamoja na kuondosha tarehe ya uhuru wa tanganyika, ila hili halitamki kwa kuwa linamchoma.

nchi washirika ndio washerehekee na kuweka kwenye katiba zao siku zao za uhuru na katiba ya muungano ibaki na siku ya muungano. ipo wazi na clear
Kwa hiyo kama "watanganyika" wanasherehekea siku ya uhuru. serikali ya Muungano kuanzia Rais, wizara na idara za Muungano na Bunge la Muungano watakuwa kazini. Zanzibar nayo watakuwa kazini?.

Kwa nini hakutaka ziwe ni sherehe zinazotambuliwa kitaifa na nchi "washiriki wa Muungano" kuonyesha mshikamano kama taifa.

Badala ya kujenga mtazamo wa kitaifa, unachofanya ni kujenga mtazamo wa kiserikali.
 
Kero za Tanganyika ipi?.

Hahahaaa leo umepaniki broo.
Tanganyika ile iliyodai Watanganyika Wasiulizwe paspoti wanapoingia Zanzibar kwani ni mshirika mwenza ktk Tanzania miaka ya 90+
Historia ni mwalimu
 
Kwani Rasimu imewasilishwa na Ukawa?
Naona mnataka Ukawa waimbe wimbo wa serikali 2
Tunataka watu wanaosimamia maoni yetu tuliyotoa kwa Tume ya Warioba.

Kama kuzungumzia kero hata Jussa ni kero.

Kama ulikuwa na maana ya kero za Muungano, Mh. Wassira alisema,

Ukitaka maelezo zaidi kuhusu ufafanuzi wa kile alikisema, unaweza kupata kupitia video au fuatilia kitakachojiti katika Bunge la Katiba

Ntafurahi siku CCM wakipata akili ya kutuambia namna ya waTanganyika kumpata Rais/kiongozi wao asiyetokana na kura za waZanzibar....!

Pili, ni namna ambayo waTanganyika watashiriki kumchagua Rais/kiongozi wa waZanzibar!
 
Serikali tatu haidaiwi na cuf,serikali tatu inadaiwa na wananchi waliotoa maoni yao kwenye tume ya warioba.

Uraia wa oman?alafu mnawajua na kuwaacha wawe viongozi?hii nchi imewashnda.

Mmeishiwa hoja,mara warioba kaleta maoni yake ya serikali 3,baada ya warioba kujb hicho kiloja,sasa mnasema cuf ndio wanataka serikali 3.

wananchi gani kwani wewe ni mwananchi au warioba ndiyo amekuwa wananchi.
 
Ntafurahi siku CCM wakipata akili ya kutuambia namna ya waTanganyika kumpata Rais/kiongozi wao asiyetokana na kura za waZanzibar....!

Pili, ni namna ambayo waTanganyika watashiriki kumchagua Rais/kiongozi wa waZanzibar!

wewe unazungumzia tanganyika gani ambayo haipo?
 
Kwa hiyo kama "watanganyika" wanasherehekea siku ya uhuru. serikali ya Muungano kuanzia Rais, wizara na idara za Muungano na Bunge la Muungano watakuwa kazini. Zanzibar nayo watakuwa kazini?.

Kwa nini hakutaka ziwe ni sherehe zinazotambuliwa kitaifa na nchi "washiriki wa Muungano" kuonyesha mshikamano kama taifa.

Badala ya kujenga mtazamo wa kitaifa, unachofanya ni kujenga mtazamo wa kiserikali.


hio ni hoja yake, mm si kua nnaunga mkono hoja yake la hasha. nnachopinga mm hii spinning kuwa CUF hawatambui mapinduzi na SMZ.

yy ana hoja zake na si lazima sote tuziamini na wengine wanahoja zao na watapambana kwa hoja ila tukatae kujenga fitna kwenye jamii na kugawa watu
 
Ni kweli kabisa MwanaDiwani, hizi kero za Muungano zitatatuliwa na Wassira & nduguze wakiwa kaburini wamekufa kwa sababu wakiwa hai kero ndiyo zinazidi kila kukicha.

Wassira mwenyewe ni kero kwa watoto wadogo wadogo!
Lazima arudishwe "kwao"!
 
Last edited by a moderator:
Ntafurahi siku CCM wakipata akili ya kutuambia namna ya waTanganyika kumpata Rais/kiongozi wao asiyetokana na kura za waZanzibar....!

Pili, ni namna ambayo waTanganyika watashiriki kumchagua Rais/kiongozi wa waZanzibar!
Ndugu, Watanganyika ndiyo kina nani?.

Naomba vile vile uelewe kuwa, Rais ameridhia Mchakato wa Katiba na bunge la Katiba kwa sasa limeishapewa madaraka ya kuweka hata hicho unachokipenda kifanyike na kama hakitawekwa, basi una uhuru kisheria wa kusema NO kupitia kura ya Maoni na kuwaambia wabunge waweke hicho kipengele.
 
wewe unazungumzia tanganyika gani ambayo haipo?

Tanganyika haipo eeh?!
Akili kama hii utaipata CCM peke yake?
Tanganyika ni jina peke yake au mipaka-territory?!
Lakini kwa kukusaidia angalia kwenye kalenda yako tarehe 9/12 Kuna tukio gani!
Acha kujivua nguo wewe!
 
Nmeangalia zle clips za vdeo sasa ccm wanatetea serikal 2 au wanamtukana maalim sefu tu? eti SUK isiwepo kwan suk imeletwa na ccm au wananchi hawa jamaa ciwaelewi kabsaaa
 
Huwezi kuwa na Mzanzibar halafu ukamkosa mTanganyika!
Rasimu ishataja Tanganyika ambayo hata isipotajwa IPO palepale!

Swali langu kwenu CCM, kero ya waZanzibar kumchagua Rais wa waTanganyika wakati waTanganyika hawamchagui Rais wa waZanzibar hamjaiona kwenye darubini la skins Wassira?
Au Tanganyika haisumbuki na Muundo wa Muungano tulionao?!
 
Hakuna kitu hatari sana katika siasa na mstakabali wa taifa kama nchi kuwa na wanasiasa ambao wanatumia ndimi zaidi ya moja katika kufikia malengo yao.

Mchakato wa Rasimu ya Katiba unazidi kuwaibua wanasiasa walaghai ambao kwao wanachokisema leo siyo hicho watakachokisema kesho.

Ngozi walizokuwa wamezivaa viongozi wa CUF zinazoitwa kutaka serikali ya Mkataba baadaye walivua na kuvaa ngozi nyingine ya kutaka serikali tatu lakini ndani ni simba wanaotaka kuvunja Muungano ili iwe ni rahisi katika kufanikisha nia yao ya kuhakikisha hakuna kitu kinachoitwa Mapinduzi ya Zanzibar ya Mwaka 1964.

CHADEMA nao kwa kukosa mwerekeo na hoja endelevu za kisiasa kwa mstakabali wa taifa kutokana na siasa zao za ubaguzi wa fikra, kabila, dini na maeneo. Wananchi waliwapa angalizo kwa kuwanyima kura kupitia chaguzi mbali mbali za taifa, kwa sasa neno CHADEMA wameanza kulifuta katika vitabu na ndimi zao ili angalau warudishe mwamko kupitia njia ya kilaghai kwa kutumia jina linaloitwa UKAWA.

Walioingia kwenye mkenge wa kudhani CUF na CHADEMA wako katika siasa kwa maslahi ya taifa endelevu haitachukua muda kufahamu kuwa wao wanatengenezwa kuwa ni daraja watakalopitia CUF na CHADEMA katika kufikia malengo yao binafsi ya kutaka kupata madaraka na kuligawa taifa.

There's a general rule in Tanzania politics. Huwezi kuuvunja Muungano bila kupambana na hoja za Mwl. Nyerere na Abeid Amani Karume zilizosababisha Muungano kuwepo na kuimarika. Baada ya kujaribu kila njia bila mafanikio ili kuvunja Muungano huku wakiogopa kupambana na nguvu za hoja za kiunganishi kikuu cha Muungano ambacho ni Waasisi wetu wa Taifa na Muungano. Kwa sasa wameamua kuvua ngozi waliyokuwa wameivaa.

Kabla ya kuanza kwa bunge Maalum, Viongozi wakuu wa vyama vya CHADEMA, CUF na NCCR-Mageuzi walikuwa wanaonekana kwa nje wako mbele kukienzi kile Waasisi wetu wa Taifa walikisimamia kwa nguvu zao zote (Muungano), lakini haikufahamika vizuri kama dhamira yao kwa ndani ilikuwa ni kuvunja Muungano kwa njia ya kilaghai.

Baada ya kugundua hili, ndiyo maana tuliwaona na kuwasikia baadhi ya viongozi kama Tundu Lissu wakianza kuwatukana waasisi wa Muungano wetu na kuwasema kuwa ni waongo na matapeli wa kisiasa in order to manipulate, deceive, and destroy Mwl. Julius Nyerere and Amani Karume reputations as the founding fathers of our Nation.

Hawawezi kufanikiwa katika satanic political mission.
Unalipwa sh. Ngap maana unijahidi sana kuwa mbea hap jf kueneza propaganda..


Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums
 
Unalipwa sh. Ngap maana unijahidi sana kuwa mbea hap jf kueneza propaganda..


Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums
Ndugu, Kama wewe una bei katika kichwa chako kwa kile unachokifanya, lazima pia uelewe kuwa, kuna watu wengine hawana bei kwa kile wananchokifanya.
 
Anatakiwa arudi huko porini kwa jamaa zake..
 
kulikuwepo sababu gani kutengeneza kitu chenye kero na mkakikalia miaka 50?. Ccm wao ndio kero ya kwanza kwa kusimamia ulaghai kwa makusudi .
 
Back
Top Bottom