Stephen Hawking's Final Book Says There's 'No Possibility' of God in Our Universe

Angalau nilichogundua ni kwamba, watu wengi, sio wewe tu hawana philosophical background ya hilo swali (Alilouliza Kiranga hapo juu)

"Je Mungu anaweza kuumba ulimwengu usio na mabaya?"

Hapa Kiranga anarejea "Logical Problem Of Evil" kwenye falsafa, kama ungeisoma hii hoja ungejijibu baadhi ya maswali uliyojiuliza mwenyewe.

Hoja yako ni kwamba, kwakua huwezi fikiria (kwa kutumia akili yako ya kibinadamu) au kuvuta picha ya ulimwengu usio na mabaya.

Basi unahitimisha kuwa kwakua haiwezekani kuufikiria (comprehend) ulimwengu wa namna hiyo, basi ulimwengu wa namna hio hauwezekani kuwepo, hivyo huu tulionao ni ulimwengu bora zaidi unaowezekana.

Hitimisho lako ni "total nonsense", huwezi kufikiria au kubuni ulimwengu usio na mabaya kwa sababu wewe sio mwenye "Maarifa yote", wewe sio mwenye "Nguvu zote" na wewe sio mwenye "Upendo wote"

Msingi wa hii hoja ni kwamba, kama kuna kiumbe (au vyovyote utakavyopenda kukiita) chenye hizo sifa tatu (Maarifa yote, Nguvu zote, Upendo wote) na kikataka kuumba ulimwengu, basi hitimisho pekee la kimantiki ni kwamba, "Kingeumbaa ulimwengu usio na mabaya",

kwa sababu tofauti na wewe, kinauweza wa ku "comprehend", "plan", "design", "desire" na nguvu ya ku "create" ulimwengu wa namna hio.

Huwezi kataa hilo hitimisho hapo juu bila angalau kukataa sifa mojawapo ya huyo kiumbe kati ya "Maarifa yote", mfano wenda hajui jinsi ya kuumba huo ulimwengu, ila alitaka na nguvu alikua nazo,

au "Nguvu zote", mfano wenda alikua anajua jinsi gani ya kuumba, na alitaka ila hakua na nguvu za kutosha,

au "Upendo wote" mfano alikua anajua, na alikua na nguvu ya kuumba pia ila hakua na upendo wa kutosha kufanya hivyo

Sasa wewe unakataa sifa ipi kati ya hizo?

Huwezi elezea kwanini Mungu wako (mwenye sifa hizo tatu by definition) aliumba ulimwengu wa namna hii bila angalau kukataa sifa mojawapo kati ya zile tatu, otherwise hatutakua na mjadala wowote wenye maana.

Usilete hoja ya "Freewill" ya kuwa Mungu aliumba ulimwengu usio na mabaya ila akampa binadamu maamuzi binafsi, then binadamu akatumia hayo maamuzi binafsi kuleta maovu

Huo utetezi haujibu hilo swali, kwasababu kuu mbili za haraka haraka

1. Sio kila maovu yanasababishwa na maamuzi ya binadamu, Tsunami, Mafuriko, Magonjwa, Matetemeko ya ardhi n.k

Baadhi ya uovu upo ndani ya DNA zetu, kitu ambacho kipo nje ya utashi wetu, hisia kama chuki, hasira, wivu, tamaa
Hivi sio vitu "unavyoamua" kuwa au kutokua navyo, mtoto mdogo anazaliwa navyo vyote, na kama huamini kwenye Evolution, hizi hisia ni useless na hazina maana yoyote kwenye Creationism.

Fikiria maisha ya mwituni, angalia jinsi gani viumbe vinavyoishi kwa "kulana", Simba haamui "kumla au kutomla swala mwenye mimba", huo ukatili upo kwenye DNA yake.

2. Hakuna Freewill kwenye ulimwengu wa Mungu anayepanga kila kitu kabla, Je Mungu "alishangaa" shetani alipoasi? au alijua kabla? kama alijua kwanini aliumba malaika mwenye mbegu ya uasi?

Unaweza toa utetezi kuwa Mungu anasababu yake nzuri tusiyoijua ya kuumba ulimwengu wa namna hii, lakini swali litakuja, kama hatuijui hio sababu, tumejua vipi ni nzuri? (The greater good argument)

So awali la "Kwanini Mungu aliumba dunia yenye mabaya" ni swali lililoshindikana.
Mkuu,

Asante sana. Bora wewe umeisoma na kuielewa "Problem of Evil".

Hapa watu wengi ninaojibizana nao hawajaisoma, na nikijaribu kuwaelewesha kwa falsafa wanajibu kwa ubishi wa imani zao za kidini, bila hata kujifunza kitu katika falsafa.

That is very disappointing.
 
Angalau nilichogundua ni kwamba, watu wengi, sio wewe tu hawana philosophical background ya hilo swali (Alilouliza @Kiranga hapo juu)

"Je Mungu anaweza kuumba ulimwengu usio na mabaya?"

Hapa Kiranga anarejea "Logical Problem Of Evil" kwenye falsafa, kama ungeisoma hii hoja ungejijibu baadhi ya maswali uliyojiuliza mwenyewe.

Hoja yako ni kwamba, kwakua huwezi fikiria (kwa kutumia akili yako ya kibinadamu) au kuvuta picha ya ulimwengu usio na mabaya.

Basi unahitimisha kuwa kwakua haiwezekani kuufikiria (comprehend) ulimwengu wa namna hiyo, basi ulimwengu wa namna hio hauwezekani kuwepo, hivyo huu tulionao ni ulimwengu bora zaidi unaowezekana.

Hitimisho lako ni "total nonsense", huwezi kufikiria au kubuni ulimwengu usio na mabaya kwa sababu wewe sio mwenye "Maarifa yote", wewe sio mwenye "Nguvu zote" na wewe sio mwenye "Upendo wote"
Hadi hapo umenielewa kabisa, kile nimekiri kutokiweza. Sina maarifa yote.

Ndio maana nikasema ninajibia tu kile ninachofahamu, yaani ulimwengu wetu kama tunavyoutambua.

Akili yangu haielewi uwepo usiohusisha muda wala utofauti wa hali. Kwa maana mazuri na yaliyo bado sio mazuri yet (kimlinganisho yayoitwa mabaya).

Kama kuna ulimwengu wa namna hiyo upo basi walioko huko ndio watakaojua wamewezekanaje kuumbwa bila concept ya mazuri na mabaya. In fact unaweza kuliuliza jiwe ulimwengu wake linauonaje labda litatupa picha ya ulimwengu as jiwe knows it.

Kimsingi, mtu anayetamani ulimwengu huu tulio nao uwe usio na mazuri wala mabaya anatamani kutokuwa hai. Anakichumbia kifo yaani hali ya kutokuwepo wala kujihangaisha (doesnt matter and doesnt bother) hata.

Sasa wewe unakataa sifa ipi kati ya hizo?

Huwezi elezea kwanini Mungu wako (mwenye sifa hizo tatu by definition) aliumba ulimwengu wa namna hii bila angalau kukataa sifa mojawapo kati ya zile tatu, otherwise hatutakua na mjadala wowote wenye maana.
Sikatai hata sifa moja kati ya hizo.

Mungu ni Baba bora, mambo ayawekavyo yana kusudi ametumia maarifa makubwa na kwa upendo wa dhati kabisa.

Basi mimi ninamuamini kwamba haya yote ni mema ili maisha na uwepo uwepo.

Hata baba wa kawaida wa familia, haruhusu wanae kushiriki ngono wakiwa bado nyumbani hata kama kwa akili ya watoto wanaweza kujadili kwamba hizo sheria hazina maana. Sasa anatulisha ili tukue tuoe na kuolewa. Kwa nn asingeruhusu tukaanza mazoezi tayari maana mwishowe ni yaleyalee.
 
Kama jibu ni ndiyo, kwa nini Mungu hakuumba ulimwengu huo ambao mabaya hayawezekani?
Kiranga, nielekeze namna unahisi uwepo unaweza kuwepo bila ya muda?

Kwa uelewa wangu hata sasa ni: tofauti wa sifa na hali ndio unatokeza muda maana unaruhusu mabadiliko.

Wewe unafikiri muda unatokezwa vipi kwanza? Enlighten me
 
Sio kila maovu yanasababishwa na maamuzi ya binadamu, Tsunami, Mafuriko, Magonjwa, Matetemeko ya ardhi n.k

Baadhi ya uovu upo ndani ya DNA zetu, kitu ambacho kipo nje ya utashi wetu, hisia kama chuki, hasira, wivu, tamaa
Hivi sio vitu "unavyoamua" kuwa au kutokua navyo, mtoto mdogo anazaliwa navyo vyote, na kama huamini kwenye Evolution, hizi hisia ni useless na hazina maana yoyote kwenye Creationism.

Fikiria maisha ya mwituni, angalia jinsi gani viumbe vinavyoishi kwa "kulana", Simba haamui "kumla au kutomla swala mwenye mimba", huo ukatili upo kwenye DNA yake
Jibu ni moja tuhapo : Kusudi

Mfano kwenye hizo 'maovu' zinazotokea bila mwanadamu kuhusika ni suala dogo tu. Kuondoa ujinga, maana tupo hapa kwa ajili ya kujifunza kuwa watawala pamoja. Ikitokea tsunami jifunze kuikabili, itawale using'anganie upumbavu kila siku ikuendeshe kama mjinga.

Ujinga ni makosa makubwa na upumbavu ndio dhambi kabisa.

Unaweza toa utetezi kuwa Mungu anasababu yake nzuri tusiyoijua ya kuumba ulimwengu wa namna hii, lakini swali litakuja, kama hatuijui hio sababu, tumejua vipi ni nzuri? (The greater good argument)
Ooh there you are! Hakika, kuna sababu ama kusudi la kila jambo.


Hakuna Freewill kwenye ulimwengu wa Mungu anayepanga kila kitu kabla, Je Mungu "alishangaa" shetani alipoasi? au alijua kabla? kama alijua kwanini aliumba malaika mwenye mbegu ya uasi?
Ona hii logic. Mungu alimuumba huyo kiumbe mwenye maamuzi na uwezo wa kutii ama kuasi ili awe na uelewa na kuchukuliana vizuri yaani empathy na viumbe wa chini yake na hata juu yake wenye uwezo wa kutii na kuasi pia.

Kuna kusudi kwa kila jambo. Na ni jema hata kama akili zetu finyu ukilinganisha zitawezashindwa kung'amua
 
Kiranga, nielekeze namna unahisi uwepo unaweza kuwepo bila ya muda?

Kwa uelewa wangu hata sasa ni: tofauti wa sifa na hali ndio unatokeza muda maana unaruhusu mabadiliko.

Wewe unafikiri muda unatokezwa vipi kwanza? Enlighten me
Kwani unaamini kuna Mungu muweza yote na mjuzi wa yote ambaye hawezi kuumba ulimwengu usio na muda?

Huoni contradiction hapo? Huoni kwamba ukisema unakubali Mungu hawezi kuumba ulimwengu ambao hauna muda atakuwa si muweza yote, na ukisema Mungu anaweza kuumba ulimwengu huo, basi ulimwengu huo utawezekana kuwepo?
 
Kwasababu nipo ,napumua na ninaishi...basi lazima kuna chanzo changu ..sikutokea kwa bahati mbaya ....hicho kilichofanya niwepo hapa duniani basiie ndio naota MUNGU
 
Hadi hapo umenielewa kabisa, kile nimekiri kutokiweza. Sina maarifa yote.

Ndio maana nikasema ninajibia tu kile ninachofahamu, yaani ulimwengu wetu kama tunavyoutambua.

Akili yangu haielewi uwepo usiohusisha muda wala utofauti wa hali. Kwa maana mazuri na yaliyo bado sio mazuri yet (kimlinganisho yayoitwa mabaya).

Kama kuna ulimwengu wa namna hiyo upo basi walioko huko ndio watakaojua wamewezekanaje kuumbwa bila concept ya mazuri na mabaya. In fact unaweza kuliuliza jiwe ulimwengu wake linauonaje labda litatupa picha ya ulimwengu as jiwe knows it.

Kimsingi, mtu anayetamani ulimwengu huu tulio nao uwe usio na mazuri wala mabaya anatamani kutokuwa hai. Anakichumbia kifo yaani hali ya kutokuwepo wala kujihangaisha (doesnt matter and doesnt bother) hata.


Sikatai hata sifa moja kati ya hizo.

Mungu ni Baba bora, mambo ayawekavyo yana kusudi ametumia maarifa makubwa na kwa upendo wa dhati kabisa.

Basi mimi ninamuamini kwamba haya yote ni mema ili maisha na uwepo uwepo.

Hata baba wa kawaida wa familia, haruhusu wanae kushiriki ngono wakiwa bado nyumbani hata kama kwa akili ya watoto wanaweza kujadili kwamba hizo sheria hazina maana. Sasa anatulisha ili tukue tuoe na kuolewa. Kwa nn asingeruhusu tukaanza mazoezi tayari maana mwishowe ni yaleyalee.
Wewe hujaelewa hata point muhimu kwamba issue si nani anatamani nini.

Issue si nani anatamani ulimwengu gani.

Issue ni kwamba Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote ambaye kaumba ulimwengu huu unaoweza kuwa na mabaya anakosa logical consistency, dhana ya Mungu huyo kuwapo ina contradiction.

Contradiction hiyo inaonesha Mungu huyo hayupo, ni Mungu wa hadithi tu ambazo watu wanajipigia.

Umeelewa somo hilo?
 
Kwasababu nipo ,napumua na ninaishi...basi lazima kuna chanzo changu ..sikutokea kwa bahati mbaya ....hicho kilichofanya niwepo hapa duniani basiie ndio naota MUNGU
Chanzo chako ni baba yako na mama yako, je, baba yako na mama yako ni Mungu?
 
Kwani unaamini kuna Mungu muweza yote na mjuzi wa yote ambaye hawezi kuumba ulimwengu usio na muda?

Huoni contradiction hapo? Huoni kwamba ukisema unakubali Mungu hawezi kuumba ulimwengu ambao hauna muda atakuwa si muweza yote, na ukisema Mungu anaweza kuumba ulimwengu huo, basi ulimwengu huo utawezekana kuwepo?
Sijasema kuwa hawezi, nimesema mimi ndio nimeshindwa kung'amua.

Na nimesema nimeridhika na kuwapo 'mabaya' katika ulimwengu ninaoufahamu mimi kwa sababu ninaliona kusudi lake. Ninaona vile ambavyo ili muda uwepo kutakuwa na tofauti ya hali na michakato ya mabadiliko. Na nimeshakubaliana na ukweli kwamba viumbe wenye akili na hekima wataweza kuamua hiki ni kibaya kile ni kizuri.

Sasa huyo ni mimi.

Turudi kwako wewe unayetaka ulimwengu wako huo usio na mabaya.

Unafikiri muda unatokezwa vipi? Na je kunawezekana kuwepo muda bila mabadiliko? Na je kunaweza kuwapo mabadiliko bila tofauti ya hali?
 
Sijasema kuwa hawezi, nimesema mimi ndio nimeshindwa kung'amua.

Na nimesema nimeridhika na kuwapo 'mabaya' katika ulimwengu ninaoufahamu mimi kwa sababu ninaliona kusudi lake. Ninaona vile ambavyo ili muda uwepo kutakuwa na tofauti ya hali na michakato ya mabadiliko. Na nimeshakubaliana na ukweli kwamba viumbe wenye akili na hekima wataweza kuamua hiki ni kibaya kile ni kizuri.

Sasa huyo ni mimi.

Turudi kwako wewe unayetaka ulimwengu wako huo usio na mabaya.

Unafikiri muda unatokezwa vipi? Na je kunawezekana kuwepo muda bila mabadiliko? Na je kunaweza kuwapo mabadiliko bila tofauti ya hali?
1. Unafanya suala hili liwe la kuhusu wewe, hili si suala la kuhusu wewe.This is not about you.

2. Unaelewa kwamba hapa hoja si kwamba mimi nataka ulimwengu usio na mabaya?

Unaelewa kuwa, hoja ni kwamba, dhana ya kuwapo Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote ambaye kaumba ulimwengu ambao mabaya yanawezekana, haina logical consistency, ina contradiction, contradiction hiyo inaonesha Mungu huyo hayupo.

Hii hoja si "ulimwengu wangu usio na mabaya", ni hoja ya logical consistency na contradiction kwenye dhana ya kuwepo Mungu.

Hoja hii wala si yangu, ni ya ukweli tu. Ilikuwepo miaka mingi kabla mimi sijazaliwa na itaendelea kuwepo nikifa.

Achana na habari za muda, zitakuchanganya kwa sababu huwezi kufanya hesabu zinazotakiwa kuelewa ulimwengu usio na muda unaweza kuwepo vipi. Time is basically how we and the universe tell/ go from low entropy to high entropy per the second law of thermodynamics. If you stop all movement, you stop the flow of entropy, you stop time, time ceases to exist.

Umeelewa kwamba huyo Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote aliyeumba ulimwengu huu unaoweza kuwa na mabaya hayupona hawezi kuwepo? Unaelewa contradiction iliyopo katika dhana ya uwepo wake?

Unaielewa hii flow ya Epicurean Paradox?

epicurean_paradox.jpg
 
Issue ni kwamba Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote ambaye kaumba ulimwengu huu unaoweza kuwa na mabaya anakosa logical consistency, dhana ya Mungu huyo kuwapo ina contradiction.
Kiranga hujaelewa tu kwamba ni kusudi uhai na maisha viwepo?

Ulitaka mambo yote yaumbwe katika ukamilifu ili kusiwepo na ukuaji kabisa au vipi?

Inconsistency gani, au kwa sababu dhana ya kusudi haunaga kabisa?
 
Achana na habari za muda, zitakuchanganya kwa sababu huwezi kufanya hesabu zinazotakiwa kuelewa ulimwengu usio na muda unaweza kuwepo vipi.
Usitishie kuwa hesabu ngumu. Wewe soma hizo hesabu mwenyewe, elewa kisha andika katika sentensi.

Nataka kujua wewe kimsingi unachukuliaje muda kwanza.

Ndiyo it is not about you wala about me...... it is about my understanding vs your understanding of the subject in question. Sasa leta uelewa wako hapa
 
Kiranga hujaelewa tu kwamba ni kusudi uhai na maisha viwepo?

Ulitaka mambo yote yaumbwe katika ukamilifu ili kusiwepo na ukuaji kabisa au vipi?

Inconsistency gani, au kwa sababu dhana ya kusudi haunaga kabisa?
Kwa nini mimi nikikupa hoja za kimantiki, unashindwa kujadili mambo kwa muktadha wa hoja za kimantiki, una personalize mambo kwa kuniambia "ulitaka..."?

Yani, mimi nakwambia hivi, kimantiki, katika hii frame of reference yetu, haiwezekani binti mdogo wa miezi 6 leo akawa mama mzazi wa kibaiolojia wa mwanamme mwenye miaka 30 leo.

Hii si habari ya mimi kutaka, huu ndio ukweli wa kimantiki. Ili mtu mke awe mama wa mtu, inabidi huyo mtu mke kwanza awe kamzidi huyo mtoto, pia inabidi awe amemzidi kwa umri ambao anaweza kumzaa.

Sasa mimi nakwambia, binti wa miezi 6 leo hawezi kuwa mama mzazi wa kibaiolojia wa mwanamme mwenye miaka 30 leo. Hii si hoja yangu, huu ni ukweli wa kimantiki.

Wewe unakuja kinijibu "Kiranga ulitaka kinamama wote wawe wakubwa kuliko watoto wao?".

Hapa suala si mimi nilitaka nini, hapa suala ni ukweli unaofuata logical consistency unataka nini.

Kusudi ni nini? Na unajuaje kuna kusudi? Kusudi la nani? Kusudi la nini?
 
Usitishie kuwa hesabu ngumu. Wewe soma hizo hesabu mwenyewe, elewa kisha andika katika sentensi.

Nataka kujua wewe kimsingi unachukuliaje muda kwanza.

Ndiyo it is not about you wala about me...... it is about my understanding vs your understanding of the subject in question. Sasa leta uelewa wako hapa
Time is basically how we and the universe tell/ go from low entropy to high entropy per the second law of thermodynamics. If you stop all movement, you stop the flow of entropy, you stop time, time ceases to exist.

Soma flow ya Epicurean Paradox halafu niambie kama umeielewa au unaweza kuipinga.
 
Time is basically how we and the universe tell/ go from low entropy to high entropy per the second law of thermodynamics. If you stop all movement, you stop the flow of entropy, you stop time, time ceases to exist.
Hata mimi nakubaliana na hii tafsiri ya muda. Nilitaka kwanza kusimamisha ardhi ambayo angalau tunaweza kusimama pamoja tukaongea.
Soma flow ya Epicurean Paradox halafu niambie kama umeielewa au unaweza kuipinga
Ni paradox ndugu, ukiielewa kama ilivyo na ukakiri hivyo basi unakuwa umechanganyikiwa. So nnaomba niseme nimeiappreciate tu.

Kuhusu suala la kuielewa au kuitatua ndio itabidi kuingiza muktadha mbalimbali na maana na tafsiri. Ndio mambo ya kusudi na nini yanaingia huko
 
Hata mimi nakubaliana na hii tafsiri ya muda. Nilitaka kwanza kusimamisha ardhi ambayo angalau tunaweza kusimama pamoja tukaongea.

Ni paradox ndugu, ukiielewa kama ilivyo na ukakiri hivyo basi unakuwa umechanganyikiwa. So nnaomba niseme nimeiappreciate tu.

Kuhusu suala la kuielewa au kuitatua ndio itabidi kuingiza muktadha mbalimbali na maana na tafsiri. Ndio mambo ya kusudi na nini yanaingia huko
1.So, umekubali kwamba inawezekana kukawa na ulimwengu ambao hauna muda.

2.Kimsingi umeshindwa kutatua hiyo paradox, kwa sababu huyo Mungu hayupo.

Ukimpima huyo Mungu kwenye mizani ya kimantiki, anaonekana hayupo.

3.Kusudi ni nini? Kwa nini kusudi? Kusudi la nani? Kusudi la nini?
 
Kusudi ni nini? Kwa nini kusudi? Kusudi la nani? Kusudi la nini?
Mmh naona hii swali na majibu yake kwa misingi ya mantiki yetu hayatafika mwisho. Futile

Kusudi au no kusudi ni uchaguzi tu. Ambao pia utaukataa. Freewill or no freewill ni uamuzi ambao vyovyote utakavyoamua utakuwa umeshautumia hata kama utakataa achana nalo tu.
 
Mmh naona hii swali na majibu yake kwa misingi ya mantiki yetu hayatafika mwisho. Futile

Kusudi au no kusudi ni uchaguzi tu. Ambao pia utaukataa. Freewill or no freewill ni uamuzi ambao vyovyote utakavyoamua utakuwa umeshautumia hata kama utakataa achana nalo tu.
Kusudi umeshindwa hata ku define!

Umekubali kwamba huyo Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo, ni Mungu wa hadithi za uongo tu za kupigwa na watu?
 
Kwa nini mimi nikikupa hoja za kimantiki, unashindwa kujadili mambo kwa muktadha wa hoja za kimantiki, una personalize mambo kwa kuniambia "ulitaka..."?

Yani, mimi nakwambia hivi, kimantiki, katika hii frame of reference yetu, haiwezekani binti mdogo wa miezi 6 leo akawa mama mzazi wa kibaiolojia wa mwanamme mwenye miaka 30 leo.

Hii si habari ya mimi kutaka, huu ndio ukweli wa kimantiki. Ili mtu mke awe mama wa mtu, inabidi huyo mtu mke kwanza awe kamzidi huyo mtoto, pia inabidi awe amemzidi kwa umri ambao anaweza kumzaa.

Sasa mimi nakwambia, binti wa miezi 6 leo hawezi kuwa mama mzazi wa kibaiolojia wa mwanamme mwenye miaka 30 leo. Hii si hoja yangu, huu ni ukweli wa kimantiki.

Wewe unakuja kinijibu "Kiranga ulitaka kinamama wote wawe wakubwa kuliko watoto wao?".

Hapa suala si mimi nilitaka nini, hapa suala ni ukweli una
Umependekeza mifano ya kimantiki, basi na tuende hivyo.

Kwa hekima yake mtu anaweza kuamua asizae na akaona ni vizuri, lakini kwa walio wengi wanaona utasa, ugumba na namna zote za kukosa uzazi kuwa ni 'mabaya'

Sasa kama kuwa na watoto ndio kitu kizuri ambacho watu wanafurahia, ni kwa nini Mungu hakuumba watu wote wawe na watoto wao tayaritayari?

Wasipitie michakato ya kupevuka
Wasipitie michakato ya utungu
Wawe tu na watoto wao tayaritayari🤔

Lakini hata hilo likiwezekana bado kutakuwa na mabaya.
Watoto wadogo wanalialia
Kulea ni kazi
Mara chanjo, mara waugue
Wasubiriwe wakue ni usumbufu tu. Kwa nini Mungu asingewaumba wakiwa watu wazima.

Sasa hao watu wazima nao (ambao ni watoto) sio vema wangekuwa na watoto wao wakiwa watu wazima tayari? Vivyo hivyo hadi mwisho.... Basi angeumba tu watu wote wanaohitajika mara moja tukaachana na shida. Hapo ndio tutajua kuwa ana upendo wote na uwezo wote eeeeh!?

Sasa bro, huoni kama kwa kufanya hivyo atakuwa effectivelly amefuta kabisa kipengele cha maisha kinachohusisha ukuaji, sex, utoto, utu uzima. Na tayari maisha yamepungua uwanda wake pakubwa tu?.

Vivyo hivyo kama ukienda kwenye 'mabaya' mengine yote yakafutwa moja baada ya jingine ndiyo mwishowe tunakuwa hatuna maisha kama tunavyoyafahamu sie maana hakutakuwa na muda tena.

Maana utauliza kwamba sasa taabu yote ya nini ya milipuko na kujisongasonga kwa nyota, magalaxy na sayari na mavolkano na matetemeko. Si angeumba tu yakiwa mwishoni bila usumbufu huu wenye mabaya mengi. Yaani iwe tu kila kitu kilishasambaa na entropy iwe kamili 100%. Je kutakuwa na uhai tena?
 
Back
Top Bottom