Stendi ya Nyegezi Mwanza kulazimishwa Kubaki Nyegezi Badala Ya Kuhamishiwa Usagara "Ni Kosa Jingine la Mipango Miji na Siasa"

Nyamsusa JB

JF-Expert Member
Jul 9, 2015
568
1,562
Habari Wanabodi.

Kuna kinachoendelea hapa Mwanza katika Mradi wa Ujenzi wa Stendi Mpya Kubwa na ya Kisasa Nyegezi Stendi hakika ni Makosa mengine Makubwa ya Kimpango Miji na Taaluma Yake..

Kama inavyo Fahamika kua Mwanza ni kati ya Majiji yanayokua kwa kasi sana Africa na hivyo Kuhitaji Mpango Miji Madhubuti ili kuondoa Misongamano Isiyokua ya Lazima ya Watu na Magari hapo baadae.

Awari ili kuanza kudhibiti Hali hii ya Msongamano kulikua na Mipango ya Kuzihamisha Stendi Kuu Mbili za Jijini Mwanza yaani Stendi ya Buzuruga na Stendi ya Nyegezi na kuzipeleka nje kidogo ya Jiji.

Ambapo stendi ya Buzuruga ingehamishiwa Kisesa ( Hii haina shida kwani mpango wake bado upo palepale)
Shida inakuja hapa kwenye hii Standi ya Nyegezi ambayo ndio stendi kubwa kabisa kwa hapa Mwanza kuendelea kulazimishwa kubaki hapa Nyegezi japo kiuharisia hii Sehemu imekua ndogo sana kuhudumu kama Stendi Kuu ya Mwanza.

Ili Kuipanua Stendi Hii Serikali itahitaji Bilioni nyingi za fedha kama Fidia kwa kulipia mejengo mbalimba ambayo yamejengwa kuizunguka Stendi.
Lakini pia hata Ikilazimishwa Kupanuliwa bado haitaweza kupata Eneo kubwa la Kukidhi Mahitaji yatakayotekea Miaka Miwili baadae.
Pia Hatua hii ya Kuipanua Stendi hii ya Nyengezi haitalisaidia Jiji la Mwanza kuanza kudhibiti Msongamano wa Magari na Watu mapema iwezekanavyo kabla Tatizo la Msongamano halijawa kubwa kama katika Majiji mengine Africa.

Stendi hii ya Nyegezi ilikua Ihamishiwe Usagara ambapo bado kuna Maeneo ya Mashamba ambapo Fidia yake ingekua ndogo sana kulinganisha na Mabilioni ya Kufidia Majengo Nyengezi.

Faida Nyingine ya kuhamishia Stendi Usagara ingekua ni Upatikanaji wa Eneo kubwa kabisa kwa Ujenzi wa Stendi Kubwa Kabisa na ya Kisasa ambayo Ingehudumu kwa Miongo kadhaa tofauti na Stendi kuwepo Nyegezi.

Pia kwa Jiografia ya Usagara ni Sehemu Muafaka kwa Stendi kubwa ya Mkoa kwani ipo njia Panda, Hapa kuna Njia Kuu Kuelekea Mkoa wa Geita, Shinyanga na hata Mkoa wa Mara via Usagara to Kisesa Road. Ni Njia Panda Muafaka kabisa kwa Abiria Kufanya Connection Kirahisi.

Faida nyingine Ilikua ni Kudhibiti Msongamano wa Mabasi na Maroli kwani Ujengwaji wa Standi Usagara ungesababisha Mabasi yote yasipite au kufika Katikati ya Jiji na hivyo kupunguza Msongamano wa Watu.

Lakini pia Ujenzi wa Stendi ungefanyika Usagara ungeongeza Kasi ya Upanuaji wa Jiji kua kubwa zaidi na Miradi mingi ingeanzishwa Usagara tofauti na Stendi kubaki Nyegezi ambapo kwa sasa ni Pafinyu kwa Maendeleo Mapya.

Sababu Kubwa inayosemekana na kusababisha Kung'ang'ania Stendi ya Nyengezi kulazimishwa kubaki hapo ilipo ni Hofu ya Halimashauri ya Nyamagana kupoteza Mapato kutokana kwamba Usagara ipo Wilaya Nyingine ya Halimashauri ya Misungwi.

Sababu Nyingine kuna Tetesi kua Matajiri walio wekeza Mahotel na Vituo vya Mafuta wamecheza Rafu ili kushinikiza Jiji, Stendi hii ya Nyegezi ibaki hapo ilipo japo ni wazi kua Eneo Hilo halina Sifa wala Uwezo wa kubeba Stendi kubwa na ya Kisasa kwa wakati huu.

Sababu Nyingine ni ya Kisiasa na Hofu alioyonayo Mbunge wa sasa wa Jimbo la Nyamagana kupoteza Kula kama hatofanya jitihada za kuzuia kuhamishwa kwa Stendi hii.

Hitimisho.

Naliomba Jiji na Utawala wa Mkoa wa Mwanza liangalie zaidi Faida na Hasara za Sasa na za Baadae za Kung'ang'aniza Stedi hii Nyengezi Kubaki Nyegezi Na Walinganishe na Faida zitakazopatikana Sasa na Baadae kwa Stedi Hiyo Kuhamishiwa Usagara kama ilivyo kwa Stendi ya Buzuruga Kuhamishiwa Kisesa.

Sababu za Kitaalamu na Gharama kwa Serikali zizingatiwe zaidi kuliko hizo sababu za Mapato ya Kiwilaya, Siasa na Watu Binafsi.

Atakae weza Aufikishe Uzi Huu kwa Serikali Kuu au hata Kwa Magufuli Ili Mwanza ipate Kupona Dhidi ya Msongamano Unaokuja Mbeleni.
 
Wanasiasa na wafanyabiashara si watu wazuri kabisa mkuu.
Naibu waziri mama Mabula si anatokea huko kwanini asilivalie njuga hili jambo!?
 
Habari Wanabodi.

Kuna kinachoendelea hapa Mwanza katika Mradi wa Ujenzi wa Stendi Mpya Kubwa na ya Kisasa Nyegezi Stendi hakika ni Makosa mengine Makubwa ya Kimpango Miji na Taaluma Yake..

Kama inavyo Fahamika kua Mwanza ni kati ya Majiji yanayokua kwa kasi sana Africa na hivyo Kuhitaji Mpango Miji Madhubuti ili kuondoa Misongamano Isiyokua ya Lazima ya Watu na Magari hapo baadae.

Awari ili kuanza kudhibiti Hali hii ya Msongamano kulikua na Mipango ya Kuzihamisha Stendi Kuu Mbili za Jijini Mwanza yaani Stendi ya Buzuruga na Stendi ya Nyegezi na kuzipeleka nje kidogo ya Jiji.

Ambapo stendi ya Buzuruga ingehamishiwa Kisesa ( Hii haina shida kwani mpango wake bado upo palepale)
Shida inakuja hapa kwenye hii Standi ya Nyegezi ambayo ndio stendi kubwa kabisa kwa hapa Mwanza kuendelea kulazimishwa kubaki hapa Nyegezi japo kiuharisia hii Sehemu imekua ndogo sana kuhudumu kama Stendi Kuu ya Mwanza.

Ili Kuipanua Stendi Hii Serikali itahitaji Bilioni nyingi za fedha kama Fidia kwa kulipia mejengo mbalimba ambayo yamejengwa kuizunguka Stendi.
Lakini pia hata Ikilazimishwa Kupanuliwa bado haitaweza kupata Eneo kubwa la Kukidhi Mahitaji yatakayotekea Miaka Miwili baadae.
Pia Hatua hii ya Kuipanua Stendi hii ya Nyengezi haitalisaidia Jiji la Mwanza kuanza kudhibiti Msongamano wa Magari na Watu mapema iwezekanavyo kabla Tatizo la Msongamano halijawa kubwa kama katika Majiji mengine Africa.

Stendi hii ya Nyegezi ilikua Ihamishiwe Usagara ambapo bado kuna Maeneo ya Mashamba ambapo Fidia yake ingekua ndogo sana kulinganisha na Mabilioni ya Kufidia Majengo Nyengezi.

Faida Nyingine ya kuhamishia Stendi Usagara ingekua ni Upatikanaji wa Eneo kubwa kabisa kwa Ujenzi wa Stendi Kubwa Kabisa na ya Kisasa ambayo Ingehudumu kwa Miongo kadhaa tofauti na Stendi kuwepo Nyegezi.

Pia kwa Jiografia ya Usagara ni Sehemu Muafaka kwa Stendi kubwa ya Mkoa kwani ipo njia Panda, Hapa kuna Njia Kuu Kuelekea Mkoa wa Geita, Shinyanga na hata Mkoa wa Mara via Usagara to Kisesa Road. Ni Njia Panda Muafaka kabisa kwa Abiria Kufanya Connection Kirahisi.

Faida nyingine Ilikua ni Kudhibiti Msongamano wa Mabasi na Maroli kwani Ujengwaji wa Standi Usagara ungesababisha Mabasi yote yasipite au kufika Katikati ya Jiji na hivyo kupunguza Msongamano wa Watu.

Lakini pia Ujenzi wa Stendi ungefanyika Usagara ungeongeza Kasi ya Upanuaji wa Jiji kua kubwa zaidi na Miradi mingi ingeanzishwa Usagara tofauti na Stendi kubaki Nyegezi ambapo kwa sasa ni Pafinyu kwa Maendeleo Mapya.

Sababu Kubwa inayosemekana na kusababisha Kung'ang'ania Stendi ya Nyengezi kulazimishwa kubaki hapo ilipo ni Hofu ya Halimashauri ya Nyamagana kupoteza Mapato kutokana kwamba Usagara ipo Wilaya Nyingine ya Halimashauri ya Misungwi.

Sababu Nyingine kuna Tetesi kua Matajiri walio wekeza Mahotel na Vituo vya Mafuta wamecheza Rafu ili kushinikiza Jiji, Stendi hii ya Nyegezi ibaki hapo ilipo japo ni wazi kua Eneo Hilo halina Sifa wala Uwezo wa kubeba Stendi kubwa na ya Kisasa kwa wakati huu.

Sababu Nyingine ni ya Kisiasa na Hofu alioyonayo Mbunge wa sasa wa Jimbo la Nyamagana kupoteza Kula kama hatofanya jitihada za kuzuia kuhamishwa kwa Stendi hii.

Hitimisho.

Naliomba Jiji na Utawala wa Mkoa wa Mwanza liangalie zaidi Faida na Hasara za Sasa na za Baadae za Kung'ang'aniza Stedi hii Nyengezi Kubaki Nyegezi Na Walinganishe na Faida zitakazopatikana Sasa na Baadae kwa Stedi Hiyo Kuhamishiwa Usagara kama ilivyo kwa Stendi ya Buzuruga Kuhamishiwa Kisesa.

Sababu za Kitaalamu na Gharama kwa Serikali zizingatiwe zaidi kuliko hizo sababu za Mapato ya Kiwilaya, Siasa na Watu Binafsi.

Atakae weza Aufikishe Uzi Huu kwa Serikali Kuu au hata Kwa Magufuli Ili Mwanza ipate Kupona Dhidi ya Msongamano Unaokuja Mbeleni.
Mambo hayaendi mpaka JPM aingilie....sijui ni nan aliyetuloga watz?!!! Alooh
 
Tatizo haiwafikii wahusika.
Kuhusu eneo lipo la kutosha tuu kuanzia barabara kuu ya kuelekea Mkolani na Nyuma ya stendi upande wa magharibi kuna eneo kubwa tuu la wazi

Lakini point ya Msingi ni kuhusu Msongamano na Location ya Usagara kua Njia panda.

Otherwise umewaza vyema sanaa
 
Wazo lako ni fyatu chief, unataka stendi ya jiji ipelekwe wilayani like seriously??

Wazo lako halijazingatia athari za abiria kuifuata stendi umbali mrefu, huko USAGARA ni mbali mno na mji mtatutesa sisi watu wa igombe
 
Umeshasema jiji la Mwanza halafu unataka stendi iende usagara misungwi...are u serious kweli
Chief Mwanza inakua kwa kasi sana Usagara soon itakua ndani ya jiji na hata miji mingine iliyopo kandokando kama kisesa hata mpaka Magu hivyo Mipango miji wanatakiwa wewe na broad vision plan ya miaka hata angarau 50 years to come.
 
Chief Mwanza inakua kwa kasi sana Usagara soon itakua ndani ya jiji na hata miji mingine iliyopo kandokando kama kisesa hata mpaka Magu hivyo Mipango miji wanatakiwa wewe na broad vision plan ya miaka hata angarau 50 years to come.
Usagara inaongoza kwa mapato Misungwi....Kisesa inaongoza kwa mapato Magu....we unafikir hayo maeneo yataachiwa na hizo halmashauri kirahisi?..
 
Umeshasema jiji la Mwanza halafu unataka stendi iende usagara misungwi...are u serious kweli
Pia hii Stand ni ya Kiimkoa au Kikanda kabisa sio stand ya daladala inahitaji Mipango madhubuti otherwise kila baada ya miaka mitano haitatosha na itahitaji Upanuzi ndio maana this time ilitakiwa plan Mdhubuti ya mara moja kwa Miongo Kadhaa ijayo.
 
Usagara inaongoza kwa mapato Misungwi....Kisesa inaongoza kwa mapato Magu....we unafikir hayo maeneo yataachiwa na hizo halmashauri kirahisi?..
Ni Mipango tu Mapato ya Stendi yanaweza yakaingia Mkoani moja kwa moja na Misungwi na Magu wakapewa asilimia fulani au wasipewe kabisa.

Mwanza sasa inahitaji Mipango Madhubuti ili kulifanya liwe jiji la maana kimiundombinu lisiponzingatiwa hili litaleta shida sana miaka michache ijayo. Jiji linakua kwa kiasi ya ajabu Afrika.
 
Pia hii Stand ni ya Kiimkoa au Kikanda kabisa sio stand ya daladala inahitaji Mipango madhubuti otherwise kila baada ya miaka mitano haitatosha na itahitaji Upanuzi ndio maana this time ilitakiwa plan Mdhubuti ya mara moja kwa Miongo Kadhaa ijayo.
Mkuu ni ngumu stendi kutoka nje ya jiji....pia si rahisi usagara kutoka misungwi.....Mwanza city council(Nyamagana) ilipewa miradi miwili...,soko kuu la kisasa mjini kati na stendi ya basi.....kuna watu wengi tu wana mapendekezo kama yako lakini jambo hili si rahisi kama unavyofikiri sababu jiji litapoteza mapato yake badala ya kuyapandisha..
 
Wazo lako ni fyatu chief, unataka stendi ya jiji ipelekwe wilayani like seriously??

Wazo lako halijazingatia athari za abiria kuifuata stendi umbali mrefu, huko USAGARA ni mbali mno na mji mtatutesa sisi watu wa igombe
Sio kweli utateseka. Mbona Station ya Standard gauge inawekwa Fera. Je ukija kwa treni ukishukia hapo Fera utafikaje Igombe. Toa wasiwasi mpaka sasa Usagara ipo connected vizuri na jiji kuna daladala zinaanzia hapo Usagara moja kwa moja kwenda Igoma, Airport, Seketule nk nk.

So stand kuwepo Usagara automatically kutatengeneza route nyingi za daladala straight to your destination from Usagara.
 
Mkuu ni ngumu stendi kutoka nje ya jiji....pia si rahisi usagara kutoka misungwi.....Mwanza city council(Nyamagana) ilipewa miradi miwili...,soko kuu la kisasa mjini kati na stendi ya basi.....kuna watu wengi tu wana mapendekezo kama yako lakini jambo hili si rahisi kama unavyofikiri sababu jiji litapoteza mapato yake badala ya kuyapandisha..
Hii issue ya Mato isipoangaliwa vizuri italeta hasara kwa Taifa. Mtang'ang'aniza Miradi leo mpate mapato baada ya Miaka kadhaa Miradi hiyo haitoshi na haifai tena mnaomba fungu jingine kwa serikali kwa Mradi huohuo tena kwa gharama kubwa zaidi. Kwa nini tusipange vitu vikadumu hata angarau kwa 30 years bila kurudiarudia.

Kurudiarudia Miradi hiyohiyo ni hasara kubwa kwa Taifa kuliko hayo Mapato unayoyasema.
 
Back
Top Bottom