Statement: Positive results from Buzwagi processing trial

I think this is a fake report!
Wamebanwa hawa katika suala la makenikia, and losses are piling up.
They are trying to find a way ot to maintain same level income as before.
For this , Big Up Magufuli.
 
Jidu, taarifa ni sahihi wanazima mitambo ya makinikia hivyo watakuwa wanachukua dhahabu tu, kopa na silver watatupa jalalani, kumbuka kopa ni kama chuma ukiweka maji inapata kutu na kuyeyuka kama pipa la maji au karai la chuma, kwahiyo sisi ndio tutakosa kodi na mapato mengine zikiwemo ajira za vijana wetu.
 
Doh. ulichokiandika hakiusiani kabisa na barua elezwa hapo juu..

Kwa kifupi haujasoma barua hiyo. Na kama umesoma basi haujaelewa...

Ni hivi hatua ya serikali ya kupiga marufuku uuzwaji wa makinikia nje. Utaleta matokeo chanya kwenye pato la serikali ...

Na kwa sasa mgodi utaendelea kuzalisha concentrates hadi 2020. Na sio 2018...

Saa nyingine vijana muwe na aibu. Si kila uzi ni lazima mtoe comment.
 
Tutakachookoa kama Taifa ni kikubwa kuliko hzo ajira elfu 2 hiyo ela itakayopatkana kwa kudhbti huo wizi itawekezwa sehemu nyingne kama Viwanda n.k na ajira zitatengenezwa zaidi ya hzo elfu 2...
 
Ur out of the Topic.. soma taarifa vizuri apo mnufaika ni serikali na Watanzania... wezi wameshikwa pabaya pia jtaid kuunga mkono ata jema la serikali /nchi yako usiwe negative kila kitu. ..
 
Pole tafakar inawezekana ni vise versa. ..si lazma ucoment kila kitu soma taarifa uielewe...pia Isome kwa jicho la tatu. ..mspinge kila jema la nchi ....hii Nchi ni yetu sote
Wewe ndio hujui ninachomaanisha mimi. Get a big picture u will understand what is behind my comment. Mimi ni zaidi ya unijuavyo hapa jf, nipo kwa ajili ya maslahi ya nchi na nipo pamoja na serikali yangu. Ongeza uelewa, utaelewa nini ninamaanisha.
 
Ushaanza kunyooka.
 
Sijui wewe nikuite fenesi? Sasa uwazi wa hiari unaosema uko wapi! Watu wamelazimishwa kuchenjua dhahabu au kama hawataki waondoke. Ninyi mkawatetea kuwa wanaonewa kwa sababu mikataba inawaruhusu kutuibia dhahabu kupitia makinikia. Hadi sasa hakuna sheria mala mkataba wowote uliobadilishwa. Badala ya kuelewa kuwa wameshika adabu wewe unawapongeza wezi hawa!
 
Ulisoma chemistry wapi?
 
Hasara nyingine kwa serikali. Ama kweli usicheze na mwenye akili.

Kilichofanyika hapa ni sawa na mtu mwenye shamba la mahindi (dhahabu) lililokuwa na mashina machache yaliyopo hapa na pale ya mbaazi (copper) na alizeti (silver). Alikuwa anavuna kwa kutumia combine harvester iliyokuwa inachambua mahindi punje kubwa na kuacha mahindi yenye punje ndogo, yakiwa yamechanganyika na mbaazi na alizeti.

Mchanganyiko wa mahindi punje ndogo, mbaazi na alizeti ulikuwa unapelekwa kwenye kiwanda chenye uwezo wa kutenganisha. Lakini katika mchanganyiko huo, katika thamani, 80% yalikuwa ni mahindi yenye punje ndogo.

Baada ya kuzuiwa kupelekwa mchanganyiko wa mahindi yenye punje ndogo, mbaazi na alizeti kwenye kiwanda, mvunaji ameamua kutafuta harvester mpya ambayo sasa itakuwa na uwezo wa kutambua mahindi yote hata kama yana punje ndogo kwa ufanisi wa 80%. Anaamua kuvuna mahindi tu, na kuacha mahindi ya punje ndogo 20% pamoja na mbaazi na alizeti, vyote viozee shambani.

Kwa sababu mchanganyiko wa mahindi yenye punje ndogo, alizeti na mbaazi, katika thamani, 80% yalikuwa mahindi ya pune ndogo, sasa alizeti na mbaazi haviwezi kuvunwa na kupelekwa kiwandani kwa faida.

Ikumbukwe kuwa silver na copper katika ile Au-Cu-Ag ore, concentration yake haifiki hata 0.1%. Ilikuwa inaongezeka baada ya kufanya concentration. Sasa haitakuwepo concentration. Hivyo Cu na Ag havitaweza kuwa extracted kwa faida.

Nini maana yake?
1) Ag itabakia kwenye tailings za mgodi, na haitachenjuliwa tena na kuuzwa
2) Cu itabakia kwenye tailings, haitachenjuliwa wala kuuzwa tena
3) Fine Au 20% itabakia kwenye tailings, na haitaweza kuchenjuliwa tena. Ifahamike kuwa mgodi wa Buzwagi average grade per tone ni 4g. Ina maana 20% ya average grade ni 0.8g/t.
4) Contractor wa usafirishaji makinikia na wafanyakazi wake, mambo yameishia hapo
5) Vituo vya mafuta mapato yake yatapungua
6) Mapato ya bandari yaliyohusiana na usafirishaji wa concentrates yameishia hapo
7) Kodi iliyokuwa ikitokana na mauzo ya concentrate ya Au-Cu-Ag, yameishia hapo.
8) Hakutajengwa kiwanda cha kuchenjua concentrates

Tulichoongeza ni royalty ya gold bar, na furaha ya moyo kuwa hatuibiwi kwa sababu sasa dhahabu inayozalishwa tutaiona kwa macho yetu, haipo katika mwonekano wa mchanga.

Nimeamini mwenye akili hakosi jibu. Wakati wote huwa na jibu la kukabiliana na mazingira yanayomzunguka. Mjinga unaweza kudhani umepata kumbe umepatikana
 
I think this is a fake report!
Wamebanwa hawa katika suala la makenikia, and losses are piling up.
They are trying to find a way ot to maintain same level income as before.
For this , Big Up Magufuli.
Subiri upate tafsiri sahihi ya hiyo taarifa!
 
Kutukana watu hakutawasaidia, wala kukurupuka hakuwezi kushindana na akili kubwa! Jiandaeni tu kisaikolojia maana kwa mara nyingine tena kukurupuka kunawaingiza cha kike!
 
Nyie ni wasaliti tu, hilo halitobadilika, mnazidi jiongezea vyeo, mlikuwa mafisadi 2015/ 2016. 2017/ 2018 mmekuwa wasaliti.
Endeleeni kukurupuka.
 
Kwa hiyo wewe ndio mjanja ha ha ha!
Mosi:Mapato yataongezeka kwa maradufu

Pili:Mabaki ya uchenjuaji yatabaki pembeni....kama ilivyo SA kuna mabaki ya kutosha ambayo yanapochenjuliwa yanaleta mshiko wa kutosha.

Tatu :Kama unakumbuka Barrick alivyosema ni kuwa ujenzi wa Smelter ni muhimu na itajengwa.


Nne :Ile hoja ya MIGA imeishia wapi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…