StarTV na Azam FC.

StarTV na Azam FC.

Jacobus

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2011
Posts
4,707
Reaction score
1,729
Hivi karibuni tumeona mechi zinazoihusu Azam FC zikioneshwa moja kwa moja na StarTV lakini ilipokuja mechi kati ya Azam na Yanga hatukuoneshwa moja kwa moja kwa nini?
Sasa huu ni mkataba au ni mambo ya 'kibongo bongo'?
 
StarTV walinunua signal ya mchezo huo toka tv station ya Juba,Sudani Kusini ambao ndio walikuwa na haki za kurusha huo mchezo.
 
StarTV walinunua signal ya mchezo huo toka tv station ya Juba,Sudani Kusini ambao ndio walikuwa na haki za kurusha huo mchezo.
Ingawa wewe ni Yanga na mimi ni Simba lakini nimefurahi kukuona umejiunga JF tuna hitaji wana michezo zaidi mjiunge maana soka letu limelala sana na kuna mambo mengi huwa yana kosa ufafanuzi....
 
Hivi karibuni tumeona mechi zinazoihusu Azam FC zikioneshwa moja kwa moja na StarTV lakini ilipokuja mechi kati ya Azam na Yanga hatukuoneshwa moja kwa moja kwa nini?
Sasa huu ni mkataba au ni mambo ya 'kibongo bongo'?

kutokana na azam ilikuwa ugenini ndio maana haikuoneshwa..
 
StarTV walinunua signal ya mchezo huo toka tv station ya Juba,Sudani Kusini ambao ndio walikuwa na haki za kurusha huo mchezo.
Aksante mkuu lakini mbona walituonesha mechi za ligi takriban mbili hivi moja kwa moja? Yawezekana wanamkataba hawa, kama ni hivo sisitizo langu ni KUUHESHIMU huo mkataba.
 
kutokana na azam ilikuwa ugenini ndio maana haikuoneshwa..
Kama wana mkataba basi watueleze upo vipi sio kutuonesha mechi tu za Ruvu JKTs na kuacha za Yanga na Simba!!!!!!
 
Ingawa wewe ni Yanga na mimi ni Simba lakini nimefurahi kukuona umejiunga JF tuna hitaji wana michezo zaidi mjiunge maana soka letu limelala sana na kuna mambo mengi huwa yana kosa ufafanuzi....

Nitajitahidi niwe nachangia mara kwa mara.
 
Aksante mkuu lakini mbona walituonesha mechi za ligi takriban mbili hivi moja kwa moja? Yawezekana wanamkataba hawa, kama ni hivo sisitizo langu ni KUUHESHIMU huo mkataba.

Tatizo hadi sasa hatujapata kampuni ya television ya kuingia mkataba na TFF/bodi ya ligi ya kurusha moja kwa moja mechi za premier league yetu. Hii ingewezekana vilabu vyetu vingepata mapato mazuri kuliko viingilio vya milangoni. Kumbuka maximum uwanja wa taifa wanaoingia na kuangalia mpira ni watu elfu sitini,ukirusha mechi "live" wataangalia watu takriban milioni kumi (kutegemea umuhimu wa mechi) hivyo hata advertiser anaangalia mileage.Muhimu jitihada zifanyike tuwe na live coverage za mechi zetu kama ilivyo nchi nyingi duniani.
 
Tatizo hadi sasa hatujapata kampuni ya television ya kuingia mkataba na TFF/bodi ya ligi ya kurusha moja kwa moja mechi za premier league yetu. Hii ingewezekana vilabu vyetu vingepata mapato mazuri kuliko viingilio vya milangoni. Kumbuka maximum uwanja wa taifa wanaoingia na kuangalia mpira ni watu elfu sitini,ukirusha mechi "live" wataangalia watu takriban milioni kumi (kutegemea umuhimu wa mechi) hivyo hata advertiser anaangalia mileage.Muhimu jitihada zifanyike tuwe na live coverage za mechi zetu kama ilivyo nchi nyingi duniani.
Sasa kwa nini haya hayafanyiki wakati nchi yetu imekuwa na vituo vya TV miaka mingi? Kwa nini vilevile vilabu haviruhusiwi kuwa na wafadhili wao binafsi? Mfano ni sakata la Africa Lione walipotaka kufadhiliwa na Zantel mwaka jana?
 
mechi ya juzi ya Yanga na Azam, Azam walikuwa ugenini isingekuwa rahisi kwako kuingia mikataba na Star tv kurusha huo mchezo
 
Star tv imeingia mkataba wa kuonysha game za azam za lig kuu inapokua Azam kama mwnyeji pamoja na game zake za kimataifa.. Sio kwmba startv haitak kuonysha game za simba au yanga ila makubaliano hayakuafikiwa
 
Star tv imeingia mkataba wa kuonysha game za azam za lig kuu inapokua Azam kama mwnyeji pamoja na game zake za kimataifa.. Sio kwmba startv haitak kuonysha game za simba au yanga ila makubaliano hayakuafikiwa
Kama ni hivo sawia ila nilidhani mwana JF mwenzetu, Yahya Mohamed, angeweka sawa hii lakini (kama ilivo tabia ya waandishi/watangazaji wa habari) hajajitokeza.
Nimesikia kuwa Shafii Dauda, kupitia mtandao wake, kaanza UMBEA (kama kawaida yake) kuhusu StarTV kuonesha mechi za Azam moja kwa moja, akihoji timu pinzani kupata mgao. Hii inamuhusu nini yeye? Au anaona kukaa kwenye radio na kubwabwaja mambo ya soka ndio utaalam? AMENIKERA mno.
 
Kama ni hivo sawia ila nilidhani mwana JF mwenzetu, Yahya Mohamed, angeweka sawa hii lakini (kama ilivo tabia ya waandishi/watangazaji wa habari) hajajitokeza.
Nimesikia kuwa Shafii Dauda, kupitia mtandao wake, kaanza UMBEA (kama kawaida yake) kuhusu StarTV kuonesha mechi za Azam moja kwa moja, akihoji timu pinzani kupata mgao. Hii inamuhusu nini yeye? Au anaona kukaa kwenye radio na kubwabwaja mambo ya soka ndio utaalam? AMENIKERA mno.

hata mie nimeona alichoandika ni wivu 2 unaowasumbua media nying za dar zinapoona star tv wanapewa mashavu.. Wao wenyewe cloudz walionysha game ya yanga na zamalek ina maana cloudz iliwapa sh ngap zamalek? Uzur wa Azam wanataka kuwa profesinal hawatak siasa za mpira ndo maana bakhresa haon hatar kutoa pesa ili game za Azam zilushwe live bila kujali ataingza sh.ngap. Anajua lengo ni wachezaj kuonekana mbal ili auze nje ya nchi vilevle soka le2 bdo lina siasa nying ndo mana maswala ya haki ya kurusha game live linasuasua sasa ndo maana bakhresa kaona hamna haja ya kuwasubili yeye kaamua kuuza game zake startv. Halaf shaffi dauda atambue hakuna tv yenye vifaa bora Tanzania ka startv ndo maana hata w2 wa supaspot wakijaga bongo wanashare vifaa vyao.
 
Hivi karibuni tumeona mechi zinazoihusu Azam FC zikioneshwa moja kwa moja na StarTV lakini ilipokuja mechi kati ya Azam na Yanga hatukuoneshwa moja kwa moja kwa nini?
Sasa huu ni mkataba au ni mambo ya 'kibongo bongo'?

Tembelea tovuti ya Shaffih Dauda {www.shaffihdauda.com} utapata habari kamili kuhusu Star TV na Azam na kwa nn mechi ya Yanga na Azam haikurushwa Live.
 
Kama wana mkataba basi watueleze upo vipi sio kutuonesha mechi tu za Ruvu JKTs na kuacha za Yanga na Simba!!!!!!

Simba na yanga walishakataa mechi zao kurushwa live mpaka na vitisho wakatoa, sasa kama mechi inawahusu sidhani kama Azam wanaweza kutumia muda wao kwenye malumbano....!
 
Simba na yanga walishakataa mechi zao kurushwa live mpaka na vitisho wakatoa, sasa kama mechi inawahusu sidhani kama Azam wanaweza kutumia muda wao kwenye malumbano....!
Tatizo la timu hizo (bolded) tunalifahamu kuwa ni KAMATI ZAO ZA UFUNDI kuwakataza mechi zao kuoneshwa moja kwa moja kuepuka mmoja wao kumfanyia kinyume wakati wa mechi na kutegemea mapato ya mlangoni tuu. Sasa wasiingilie Azam mipango yake kwani kuna bwana mmoja ajiitae Shafii Dauda keshaanza UMBEA wake.
 
Tembelea tovuti ya Shaffih Dauda {www.shaffihdauda.com} utapata habari kamili kuhusu Star TV na Azam na kwa nn mechi ya Yanga na Azam haikurushwa Live.
Si Yanga tu hata Simba nao haitarushwa kwa sababu za kipuuzi. Hebu tujiulize wanapotutangazia mechi za Englang na fixture yake hulipwa pesa ngapi??????????
Kutangaza chetu nongwa ila cha England..............
 
Back
Top Bottom