Jamal Bakhresa: TFF imeharibu mpira wa Tanganyika. Azam FC nitaihamishia Zanzibar

Jamal Bakhresa: TFF imeharibu mpira wa Tanganyika. Azam FC nitaihamishia Zanzibar

figganigga

Platinum Member
Joined
Oct 17, 2010
Posts
27,459
Reaction score
61,726
Mmiliki wa Azam FC, Jamal Bakhresa, amesema yupo tayari kuiondoa timu hiyo katika Ligi Kuu Tanzania Bara na kuihamishia Zanzibar, akidai kuwepo kwa ukosefu wa haki katika uendeshaji wa ligi.

Bakhresa amesema uamuzi huo
unatokana na kile alichodai kuwa ni waamuzi kutotenda haki katika baadhi ya mechi za timu hiyo.

Amedai kuwa iwapo hali hiyo itaendelea, Azam FC ipo tayari kuondoka kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara na kuhamia Zanzibar
 
Tatizo siyo waamuzi wa mpira au TFF au bodi, tatizo ni mfumo mzima wa Tanzania uliojaa rushwa, dhuluma, na upendeleo.

Zamani sana nezi za TANU na FAT tulikuwa na marefa wasiokuwa na beji za FIFA, kama vile Manyoto Ndimbo, walikuwa wanachezesha mpira kwa haki bila malalamiko yoyote. Leo enzi za CCM na TFF mambo yamekuwa shaghla baghla.

Timu pendwa ya TFF ni Simba tu
 
Na mdomo wake kama kajaza mate mashavuni. Anaongea kama bwabwa
Sasa hapa kati yako na yeye nani anaonekana bwabwa? Acha ujuaji usio na maana na kuongea vitu vya ajabu mbele za watu.

Mzee yupo sawa, na watu wenye uelewa wameshaona huo upuuzi wa TFF na sasa hawafuatilii tena mpira wa Tanzania na ndio maana mahudhurio ya watu uwanjani ni machache sana siku hizi
 
Back
Top Bottom