STARTV: Maamuzi ya NEC-CCM kuelekea 2015

STARTV: Maamuzi ya NEC-CCM kuelekea 2015

CCM na Serikali yake imefika hapo ilipo kwa sababu ya kuwa na watu kama NAPE ambao hawana kweli ndani yao na au hawajui wanapashwa kufanya nini zaidi ya kushika madaraka. Hivi NAPE anajua nini kuhusu KILIMO KWANZA? NAPE anajua nini kuhusu hali ya maisha ya wananchi wa kawaida?

Hivi NAPE anafahamu kuwa 20 yrs ago maisha ya Mtanzania (in all wise) yalikuwa bora zaidi kuliko leo hii? Badala ya kuwa na mawazo ya kuendeleza CHama na Nchi kwa ujumla bado anakuwa na mawazo ya kutetea mapungufu yanaonekana wazi.

TZ nchi pekee ambayo

Inawezekana vipi kiwanda cha matairi kinakufa wakati soko linaongezeka (idadi magari yanaongeza)!
Huduma za reli zimeyumba kuliko maelezo!
Bei ya sukari inashindwa kuwa managed wakati kuna chombo husika!
Mfumuko wa bei!
.....

NAPE ukweli ni kwamba CCM na Serikali wako mbali sana na wananchi....CCM na Serikali haikubaliwi na wananchi walio wengi isipokuwa tu kwa mujibu wa udikteta.
 
Hivi NAPE anafahamu kuwa 20 yrs ago maisha ya Mtanzania (in all wise) yalikuwa bora zaidi kuliko leo hii? Badala ya kuwa na mawazo ya kuendeleza CHama na Nchi kwa ujumla bado anakuwa na mawazo ya kutetea mapungufu yanaonekana wazi.

I feel sorry for you!

So in 20yrs ago, Tanzanians had better access to water, health, education, information (like you do now), demokracy, freedome of speech, movement, association, transport services etc than today!!!!

Ama kweli sijui tumelishwa nini vile?
 
Kwa kuanzia ningependa jina NEC LA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI libadilishwe kuleta utofauti na ile NEC YA CCM. NEC iwe TEC (Tanzania Electoral Commission). Kuhusu maadhimio ya NEC wala sina shaka, CCM ni mavuvuzela, sina imani nao hata kidogo, kifupi wamedandia hoja kwa kuogopa upepo wa kisiasa usiwadhuru. Then inakuwaje wao waruhusu? Kwani nchi chini ya mfumo wa chama kimoja?

Acha utani wewe. Unataka kuwapa wale jamaa hoja. TEC = Tanzania Episcopal Council = Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania.
 
hakika hili la kuanzishwa kanda maalum vyuo vikuu ccm ni lazima litaighalimu, sasa wasilaumu, chadema hiyo itakuwa ni fursa yao, subiri...

Kivipi Mkuu? Hebu fafanua kidogo.
 
Leo ktk kipindi cha tuongee asubuhi star tv nimemusikiliza sana nape nakugundua kuwa viongozi walio wengi wa chama cha mapindizi huwa hawaishi tanzania tunayoishi sisi bali wao wanatanzania yao,maana ukimsikiliza kwa undani utajua kama ndohivi itakuwavigumu sana tanzania kupata maendeleo.Vijana wote wa Tanzania na waomba michango yenu ktk hili(hivi tukiondoa maDC,RC,NAIBU WAZIRI,POSHO ZISIZONALAZIMA,KUPUNGUZA SAFARI ZA VIONGOZI,VIONGOZI WOTE KUTUMIA MAGARI YA AINA MOJA ILIKUPUNGUZA GARAMA) kwa miaka mitano tutaokoa kiasi gani cha pesa?
 

Acha utani wewe. Unataka kuwapa wale jamaa hoja. TEC = Tanzania Episcopal Council = Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania.

Tutafute jina lolote litakalo itofautisha NEC ya Magamba na NEC ya Uchaguzi.
 
mie hata sikutizama hicho kipindi, kwa nini unashangaa kuwa Nape anaishi hapa Tanzania?Yes Nape anaishi Tanzania, hebu funguka vizuri ueleweke..
 
Ndiyo anaishi Tanzania ila alizaliwa katika familia iliyolishwa vema na Kodi ya Walalahoi akashiba vizuri sana na kudharau walalahoi mpaka jukumu iliyomtuma akasahau .... na ndiyo maana mpaka leo anakula Bata kwenda mbele kupitia dola.
 
Badosija amini kama yanayotokea kwenye madani za kisiasa hapa tanzania anayaona,hikikimbunga siyo kama upepo wa mlema yule alikuwa mtu mmoja,hikikimbunga hakina mfano kaka nape.ushauri leo tanganza kujiuzulu nyazifa zote ndani ccm na kujiunga na upinzani waacha hao wasio ona watumbukie nacho.
 
Mkuu ritz unakumbuka wakati wanahitimisha kipindi kule dar nape kama kawaida yao ccm alijinasibu kuwa atajibu hoja zote hapa jf na fb,kwa kuendeleza kasumba yao kuwa ni upepo tu watu hapa wanaendelea kutoa maswali hamna wa kujibu.na hamjashituka kama mmeachwa stendi
 
Mkuu ritz unakumbuka wakati wanahitimisha kipindi kule dar nape kama kawaida yao ccm alijinasibu kuwa atajibu hoja zote hapa jf na fb,kwa kuendeleza kasumba yao kuwa ni upepo tu watu hapa wanaendelea kutoa maswali hamna wa kujibu.na hamjashituka kama mmeachwa stendi

Tatizo la Nape maneno mengi sana hata mie nimemsikia akasema atakuja humu JF kujibu hoja zote na akasema anatumia ID yake wala ajifichi sasa mpaka mida hii hatumuoni kama sio uhuni ni nini?
 
I feel sorry for you!

So in 20yrs ago, Tanzanians had better access to water, health, education, information (like you do now), demokracy, freedome of speech, movement, association, transport services etc than today!!!!

Ama kweli sijui tumelishwa nini vile?

Nimeshindwa kuona hivyo ulivyovitaja vimebadilisha vipi maisha yetu? Maana maisha bado ni magumu, ukienda hospitali dawa hakuna, vijijini hata mijini maji bado ni shida tena sio salama, vyakula bei juu ingawa unasema transportation services good. Tulitaraji hivyo vyote kwa pamoja vitutoe kwenye huu umaskini lakini wapi ndio kwanza umaskini unaongezeka, huduma za jamii sio za uhakika.
 
mimi naona JK kaleta suala la mgombea binafsi kwa sababu anataka kutimiza ahadi yake na Lowasa. Anajua Lowasa hawezi kupitishwa na CCM hivyo anampa mwanya wa yeye kuwa mgombea binafsi.
 
Nape hawezi kuja humu sa hv, Yupo kempisk anapiga lunch 2. Gosh....
 
Tatizo la Nape maneno mengi sana hata mie nimemsikia akasema atakuja humu JF kujibu hoja zote na akasema anatumia ID yake wala ajifichi sasa mpaka mida hii hatumuoni kama sio uhuni ni nini?

Mkuu Ritz Ni-PM nikakununulie soda!
 
Back
Top Bottom